Thursday, February 7, 2019

MUNGU, MWANDISHI WA BIBLIA

No photo description available.


“kila andiko limeandikwa kwa upako wa Mungu”

Kama mtu anaweza kuangalia ukubwa wa mbingu ama ulimwegu atashangazwa na ubunifu na muundo msingi wa uumbaji. Kila upande wa jinsi dunia ilivyoumbwa ni ushahidi kimya kuwa yupo Muumbaji. Mbali na kitabu tunachojua kama Biblia, Binadamu atazidi kubaki mjinga na ashindwe kuelewa asili na hatima ya dunia. Biblia ndio ufunio wa Mungu kwa binadamu. Inaonyesha ukweli dhahiri kuhusu Mungu na binadamu. Inaonyesha kusudi kuu la uumbaji, asili ya dhambi na kifo, kuendelea na hatima ya mataifa na kisha ufalme wa Mungu unaokuja. Lakini Biblia pia ina dhamani ya kibinafsi. Na huwapa vijana na wazee matumaini. Inatuonyesha sababu halisi ya kuishi na pia kufunua ujinga ufuatao wa dunia ambayo imejitenga na Mungu na Uumbaji wake. Kwa kifupi,biblia inaweza kubadilisha maisha yetu.

Lengo la hili somo ni kuonyesha kwamba kuna Muumbaji mmoja mkuu ambaye aliongoza kuandikwa kwa Biblia ili kuonyesha tabia zake na kusudio lake kwa mwanadamu.


2 Timotheo 3:14-17; 2 Pet 1: 19-21

BIBLIA: UFUNUO WA MUNGU KWA BINADAMU

Ijapokuwa Biblia imegawanywa katika sehemu sitini na sita ina ujumbe mmoja dhabiti. Inadai kuwa Neno la Mungu. Kwa vitabu vitano vya kwanza imetajwa mara zaidi ya mia tano “Bwana akasema” au “Bwana akanena” tena kwa mara 300 inarudia maneno hayo kutoka kwa kitabu cha Yoshua hadi Wimbo wa Solomon. Vitabu za manabii zinarudia maneno hayo kwa mara 1200.

Waandishi wa Biblia walikua wanatimiza jukumu kama waalimu wa sheria wa Mungu aliyekua mwandishi Mkuu. Alionyesha mafunzo yake kupitia kwa wanadamu. Waliandika kutokana na upako wake (Hebrania:1:1-2; Nehemia 9:20) Aliwaelekeza jinsi watakavyosema ijapokua lugha waliotumia ilikua yao. Kwa kusudi hili Mungu aliwachagua wanaume kutoka kila tabaka la jamii. Wafalme, viongozi, makuhani, wasomi, wachungaji na pia wavuvi walikua kati ya waliochaguliwa. Aliwagawanya kulingana na hadhi, watkat na mahali walikotoka. Mwandishi mmoja akiwa Syria wa pili alikua Uarabuni, wa tatu Italia, wa nne Ugiriki, wa tano Babelli na wasita palestina. Hii inaaanisha walikumua na masasiliano machache sana. Musa ndiye aliyekua mwandishi wa kwanza na aliandika vitabu vitano nya kwanza vya BIblia miaka 1600 kable ya Yohana kuandika kumbukumbu ya ufunuo.

Licha ya tofauti hizi kubwa kuna uwiiano wa ajabu kwa yale yalionadikwa yanavyounganisha vitabu hivi vyote 66 na kuwa moja ili kufanya Biblia kitabu cha kipekee katika ulimwengu wa fasihi. Mungu amempa mwanadamu kitabu hiki ili kumpa matumaini (Warumi 15.4) Biblia pekee ndio inaweza onyesha njia ya wokovu (2Timotheo 3:15). Kukataa ujumbe huu ni kumaanisha kifo. (Kumbukumbu la Torati 30:17-20, Mithali 14:12.)

Kwa kawaida Biblia imegawanya katika sehemu mbili; Agano la kale (vitabu 39) na Agano jipya (vitabu 27). Mgao huu umefanywa na mwanadamu kwa sababu Biblia inastahili kuchukuliwa kama kitabu kimoja cha ufunuo wa Mungu kwa binadamu. Agano la kale lilikua limeandikwa kwa kiebrania na Agano jipya na Kigiriki. Mfumo wa kuandika Biblia na Kiingereza ulioidhinishwa na hutumika leo ulichapishwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 1611. Pia ilitafsiriwa na Kiswahili kama Biblia Muungano. Ilijulikana kama mfumo ulioidhinishwa kwa sababu mamlaka ya kutasfri kwa kizungu ilipewa Mfalme James wa Uingereza. Kutoka wakati huo tafsiri nyingi zimetolewa zingine zina manufaa na zingine zina manufaa kidogo sana. Nakala rasmi haina makosa lakini hakuna toleo lisilo na makosa. Kwa miaka iliyopita kumekua na makosa ya kutafsiri kwa waandishi kuiga nakala rasmi na kutafsiri kutoka kwa lugha asili kwa lugha nyingine. Lakini makosa haya ni kidoga na hayana umuhimu mkubwa kwa sababu kila toleo lina mafunzo muhimu ya Biblia yanayoeleweka.

BIBLIA: UPAKO NA UKWELI

Petro aliweka kanuni za msingi kwamba Biblia imechaguliwa (2 Petro 1:20-21). Alitangaza kwamba “ hakuna nabii wa andiko alikuwa na tafsiri ya kibinafsi; kwa sababu unabii wa kale haukuletwa na mapenzi ya binadamu bali ni wanaume watakatifu walioteuliwa na Mungu kuongeo kama wananvyoongozwa na Roho Mtakatifu.

Kwa hivyo ukweli unaweza patikana kwenya Biblia na hakuna yeyote anaweza kuonyesha uwongo kwenye matokeo ya kihistoria. Wanaopiga Biblia wamelazimika kukubali kwamba kuna ukweli ndani yake. Mashahidi wa manabii wanaonyesha kwamba kuna ukweli dhahiri kwamba Mungu ndiye Mwandishi kwani yeye pekee ndiye anaweza kutabiri siku zijazo. Utabiri wa kushangaza katika Biblia umetimia jinsi ulivyo tabiriwa. Mfano:

Ukuta wa Babelli bado ni vifusi (Isaya 13:19-21, Yeremia 51:37).
Ninevehe bado ni tupu na imejaa taka ((Nahumu 2:10).
Misri ni moja kati ya mataifa duni (Ezekiel 29:15).
Tiro iliyokua bandari imemezwa na bahari (Ezekiel 26:5).
Taifa la Israel limesambaa katika mataifa yote (Kumbukumbu la Torati 28:64) na sasa wanakusanywa tena Yeremia 30:11; Ezekiel 37:21-22)
Nguvu za Kaskazini zina uadui na taifa la Israel kama Urusi iliyoendelea.

MUNGU KATIKA BIBLIA

Biblia inaaza kwa kuongelelea mtu mmoja ambaye ni Mungu (Mwanzo 1:1). Na ufunuo unamalizia kwa kuonyesha jinsi Mtu huyu mmoja atakavyo wekwa wazi kwa viumba vyote. “Mungu awe yote katika wote” (1 Wakorintho 15:28). Inatuonyesha jinsi kila mmoja wetu anaweza kushiriki katika kukamilisha utukufu wa Mungu. Injili inatuita kila mmoja wetu tujitenge kutokana na wanaume na wanawake ambao wanajitengenezea njia ya kuelekea kuzimu milele. Mungu anachukua watu wake kutoka kwa Gentiles (Matendo. 15).

Jambo la kwanza muhimu ni kuelewa kwa usahihi Mungu ni nani (Yohana 17:3; Waebrania 11:6) lazima tukubali umoja wa Mungu.

TABIA ZA MUNGU

Kuna pande mbili katika tabia za Mungu tunapaswa kufikiria. Paulo alisema “ fikirieni kuhusu wema na ukali wa Mungu (Warumi 11:22. Pande hizi mbili za tabia ya mungu zilidhihirishwa na Musa katika Mlima Sinai(Kumbukumbu la Torati 34:6-7) na zote zilidhihirika katika uhusiano wake na mwanadamu. Kwa mfano kipindi kile Mungu alimtuma Musa kuwokomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Aliwaokoa kutoka kwa bahari ya Shamu lalini aliangamiza majeshi ya Faraoh. Yesu Bwana anakuja kuhukumu dunia kwa haki. Hii inammanisha kutakuwa na huruma na ukombozi wa wateule wake na pia kifo na uharibifu kwa wale waovu.

Sababu ya haya ni uasi wa binadamu” hata neema ionyeshwe walio waovu hawatajifunza haki (Isaya 26:10-11) Mungu anafunza binadamu kwa wema wake na wokovu wa milele.

Biblia Inatufundisha kwamba Mungu ni asiyebadilika kwa lengo lake (Mal. 3:6) Yeye ni mwenya kujua yote (Zaburi 139:1-6) Yupo kila mahali (vv.7-12); na ni mwenya nguvu (vv. 13-18).

Ni ukweli kwamba Mungu anayajua yote (Waebrania 4:13; Jeremia 23:24) na anaweza kutelekeza mapenzi yake ili kutuonyesha jinsi tunavyostahili kuishi mbele zake. Hata hivyo yeye hutawala kwa maenzi na wala sio woga. Madhumuni ya ufunuo wake ni kubadili tabia zetu ili tupate kuendana na njia zake, na tuwe tunafaa kiakili na kimaadili ili tuweze kupewa uzima wa milele na Kristo anarudi tena ( Wafilipi 3:20-21.).

KUSUDI LA MUNGU

Kusudi kuu la Mungu imeelezwa kwa kimsingi katika Hesabu 14:21- kama kweli ninavyoishi dunian yote itajazaa utukufu wa Bwana.” Hii inamaanisha nini? Dunia nzima itangaa kwa nguvu an utukufu wa Mungu lakini utukufu wa Mungu ni zaidi ya haya. Inagusia tabia zake. Wakati Musa alimwomba Mungu amwonyeshe utukufu wake, Kwa kumjibu Mungu alimwonyesha tabia zake, mwenye huruma, neema na mwingi wa rehema na ukweli. Kutoka 33:18; 34:6-7)

Utukufu wa Mungu utadhihirika kwa wote humu duniani wakati wanaume na wanawake watakoa uonyesha katika maisha na tabia zao. Yesu alituonyesha maisha yake ya "utukufu wa Baba yake" kwa kuwa alikuwa "amejaa neema na kweli" (Yohana 1:14).

Mungu anawaita wanaume na wanawake kwa lengo hili kama tunaweza kuelewa madhumuni ya Mungu na kuonyesha tabia ya Mungu katika maisha yetu, wakati Kristo atakaporudi, tutapewa asili ya Mungu (1 Petro 1:04.), Na kuonyesha tabia za Mungu katika ukamilifu wa uzima wa milele.

Wacha tuangalie Masomo yetu ya Biblia ili tuweze kupata “hekima na hata kupata wokovu” na ili tustahili kuingia katika ufalme wa mbiguni wakati Yesu ataporudi.

MASOMO KWETU

Ni kwa kusoma Biblia tu ndio tunaweza kujua hatima ya mwisho ya dunia na mwanadamu Mungu anataka tujue Ukweli Kumhusu Kusoma Biblia kunaweza kubadili maisha yetu Jinsi gani kijana kubali njia zake na kutii na kulifuata neon lako? (Zaburi 119:9).

Msimkatae yeyote anayeongea (Ebrania 12:25)
Hakikisheni kila jambo huku mkizingatia yaliyo mema. (1 Wathesalonike 5:21.).

Shalom,

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW