Wednesday, December 9, 2015

MAOMBI YA KUPINGA MAGONJWA, VIFO, AJALI NA UHARIBIFU KATIKA MAISHA YAKO

1. Baba, katika jina la Yesu, naangusha kila mbinu za kishetani zinazozuia mafanikio yangu, katika jina la Yesu.
2. Nakataa na kupinga magonjwa ya kila aina katika nyumba yangu na familia yangu, kwa jina la Yesu.
3. Imeandikwa katika Zekaria 2:8 ya kwamba “Yeye anayenigusa mimi anagusa mboni ya jicho la Mungu”, hivyo, ninalisimamia Neno hili na kupinga kila nguvu inayosababisha magonjwa na upotevu wa fedha zangu katika jina la Yesu.
4. Nasimama kinyume na ajali na vifo katika familia yangu na ndugu zangu katika jina la Yesu.
5. Nawafunika watu wa familia yangu, kijiji changu na nje ya kijiji kwa damu ya Yesu. Ninawalinda na kuwaongoza kila mmoja kwa jina la Yesu.
6. Ninaamuru kila kinachoharibu mtaji na biashara yangu kufa mara moja katika jina la Yesu.
7. Ninaificha fedha yangu yote katika damu ya Yesu na kamwe adui hawezi kuigusa.
8. Baba, katika jina la Yesu, nasimama katika Neno kama mtoto wa Mungu niliyeketishwa mahali pa juu pamoja na Kristo, na ninatangaza kuwa mikutano ya kipepo juu ya maisha yangu na fedha yangu haitafanikiwa, katika jina la Yesu.
9. Namfunga kila anayeharibu fedha yangu nyumbani na sehemu yangu ya kazi katika jina la Yesu.
10. Wewe pepo uliyetumwa kuharibu biashara na fedha zangu, ninakufunga na kukutupa kwenye shimo la giza katika jina la Yesu.
11. Ninaamuru moto wa Roho Mtakatifu kumlamba kila mmoja aliyesimama kinyume na biashara na mafanikio yangu katika jina la Yesu.
12. Ewe mlima uharibio, ninakuangusha na nianaamuru usambaratike, katika jina la Yesu. 13. Ninaificha biashara, ofisi, fedha na miradi yangu yote katika damu ya Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai. Amen.
14. Bwana, ninaomba upendeleo wako katika maisha yangu ili niweze kufanikiwa.
15. Upendeleo wako unizunguke kadiri ya Neno lako, katika jina la Yesu.
16. Bwana, naomba kuunganishwa na watu watakaonisaidia kufikia ndoto zangu kwa jina la Yesu.
17. Oh, Bwana, naomba ufanye njia kwa ajili yangu hata pale pasipo na njia katika jina la Yesu.
18. Baba, naomba niunganishe na mtu ambaye atakuwa msaada mkubwa katika kuyafikia mafanikio yangu katika jina la Yesu. 19. Baba ninaamini ya kwamba kila ninapokanyaga ninapamiliki sawasawa na na Neno lako, hivyo naomba univike vazi lako la upendeleo katika jina la Yesu.
20. Asante Bwana Yesu kwa kuwa umefanya sawasawa na nilivyokuomba katika jina la Yesu.
Amen.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW