Wednesday, December 9, 2015

SOMO: MAOMBI YA CHUMVI YA KUVUNJA LAANA NA MAAGANO YA UKOO


Jinsi ya kuvunja Roho za laana na maagano kwenye ukoo wenu, maana watu wengi wameshindwa kufikia malengo na hata kukata tamaa kwa sababu ya maagano na laana za kabila zao, leo hii Mungu anakwenda kukuvusha, chumvi uliyoishika enaenda kukugeuza na kuangalia familia yako wapi imetoka na wapi inaelekea.
Habari ya ukoo ni sawa na lugha ya kabila bali siyo lugha ya Taifa, Mungu hakuumba msomi aliumba kabila ndio maana hata baadhi ya mapepo hayawezi kutoka mpaka ya sikie lugha ya kabila la kwenu.usiangalie wapi umetoka maana Mungu wetu hahukumu umefanya dhambi ngapi, bali wewe upo kwenye nafasi gani?
UFUNUO WA YOHANA 7:1 ‘’Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wowote.’’
Maandiko yanasema Malaika walisimama pande nne wakizuia upepo usivume kwa ajili ya makabila kumi na mbili na kila pembe alisimama malaika mmoja.
kwa hiyo uwe na uhakika kwenye ukoo wa kwenu, hiyo nafasi ambayo alitakiwa asimame Malaika lakini sasa yamesimama mapepo ambayo yamezuia pande nne za ukoo wenu kusitokee upenyo wa maendeleo ya fedha na uchumi.
Kwa maana nyingine kusimamishwa kwa ukoo wa kwenu halafu tunashuhudia mnazika watu kuanzi miaka themanini na kuendelea na naghafla mkaanza kuzika kuzika chini ya kiwango hicho mjue kuna Roho nyingine zimewaingilia kati na zinauwa mmoja baada ya mwingine, na hata wale walioendelea bado hawajakufa kiroho lakini fedha zao zinaendelea kutumika na wale wanaendelea kifedha na watoto wao wamekufa, jua kuna matatizo kwenye familia nzima na unajaribu kutoa sadaka , kwenda kwenye maombi lakini tatizo bado linaendelea.
Mwanangu maombi ya siku moja hayawezi kubadilisha jahazi lililokuwa limezama, lazima ujipange sawasawa na kanuni ya Bwana inayosema natafuta mtu atakaekuwa mlango wa mimi kupita ili nipige na nisizuru ukoo iliyo baki nyuma.
Tunapo ongelea pepo haimaanishi ukoo wenu umefungwa bali kuna roho ambayo ni mlango unaokaribisha mapepo,maana kama roho ya Yuda ilijiunganisha na shina la Daudi na shina la Daudi likajiunganisha na Yesu, Uwenauhakika roho ya nyumbani kwenu itajiunganisha na mapepo.
UFUNUO 7,9,10 “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila Taifa, na kabila,na jamaa na lugha wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za mwana –kondoo,wamevikwa mavazi meupe,wana matawi ya mitende mikononi mwao. wakilia kwa sauti wakisema Wokovu una Mungu wetu aketiye katika keti cha enzi, na mwana kondoo.’’
Mungu anayasikia maombi yako usifikili wingi wa dhambi zako, maandiko yana sema, Adamu pamoja nakufanya dhambi lakini alimsikia Mungu alipo mwita Adamu uko wapi? Mungu hajishuhulishi na dhambi ulizo fanya bali atakuuliza nafasi yako ipo wapi? aliyokuweka kama Habakuki , maana atasimama katika zamu yake na atamuona Bwana atakacho mjibu.
UFUNUO 5:2 “Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu,Ni nani astahiliye kukifungua kitabu, na kuzivunja muhuri zake? Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi,wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu,wala kukitazama.’’
Maandiko ya natuambia kisha nikamuona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma,kimetiwa muhuri saba.
Kwa niaba ya F.J Kilawa
Max Shimba Ministries

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW