Msomaji wangu,
Tumesha zisoma aina tatu za Sabato katika Sehemu Ya Sita, sasa, tuangalie malengo ya Sabato.
Wanao jiita Wasabato wa karne hii, hawafamu lengo la kushika sabato kwa wana wa Israeli. Kwa kifupi, lengo la kushika Sabato kwa Wana wa Israeli lilikuwa ni kupumzika kazi na kustarehe tu na wala si vinginevyo.
Kitu cha kushanganza, wanaojiita Wasabato katika karne ya leo, wameigeuza sheria aliyo pewa Musa na wana Waisraeli ya kushika sabato kama ni siku ambayo Mungu ameamuru wafanye ibada, kinyume kabisa na kusudi zima na maana halisi ya neno sabato. Watu hawa wamekuwa na tabia ya kuwashutumu wakristo wengine na kusema kuwa, Jumamosi ndiyo siku halali ya kufanya ibada, lakini Jumapili, ni siku ambayo haikuamriwa na Mungu, watu kukusanyika kufanya ibada. Zaidi ya hapo, wanasema kuwa eti Jumapili ni siku ya kipagani. Wasabato hawa wanaihusisha siku ya Jumapili na waabudu JUA, kwa kufanya tafsiri ya neno la Kiingereza ‘Sunday’ – WANALIGAWA NENO “SUNDAY” KWA KUTENGANISHA SUN AND DAY, SUN = JUA NA DAY = SIKU Na kuja na jibu kuwa wale wote wanao abudu Jumapili basi wao wanamwabudu Mungu JUA, ingawa tuna uthibitisho tosha kuwa Wakristo wa kwanza walimwabudu Yesu ambaye alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na SIO MUNGU JUA kama wanavyo dai. Ili kufahamu kwanini kuna siku hizi za wiki na maana yake, ni vyema kuangalia msingi wa hizi siku na jinsi walivyo ziweka. MFANO: Tuiangalie siku ya JUMAMOSI ambayo kwa Kiingereza ni SATURDAY, je, hili jina walilipataje? Kutokana na Warumi siku hii ya SATURDAY iliitwa kutokana na SAYARI YA ZOHALI yaani (dies Saturni) kwa sababu Warumi wa wakati huo waliheshimu sayari Zohali. SASA KAMA TUKITUMIA UTAALAMU HUO HUO WA KUHUSISHA SIKU NA IMANI AU DINI, JE, INAMAANISHA KUWA WASABATO “SDA” WAO WANAAMINI NA AU ABUDU SAYARI YA ZOHALI?
Kitu ambacho hawa Wasabato hawakifahamu ni hiki: Agizo la kushika sabato na siku ya kukusanyika ni vitu viwili tofauti na ni maagizo mawili tofauti ambayo wana wa Israeli walipewa kuyatekeleza.
AGIZO LA KUKUSANYIKA KUFANYA IBADA:
Katika agizo la kukusanyika kwa wana wa Israeli, Mungu alitoa siku mbili yaani Jumapili na Jumamosi, ingawa wasabato karibu wote hawalijui jambo hili, maana hao wamekaririshwa siku ya sabato tu yaani Jumamosi.
UTHIBITISHO:
Tunaweza kuthibitisha ukweli huu katika kitabu cha Kutoka 12:16 Biblia inasema, “SIKU YA KWANZA kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na SIKU YA SABA kutakuwa na kusanyiko takatifu, haitafanywa kazi yoyote katika SIKU HIZO, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu.”
Mungu aliwaamuru wana wa Israeli wakusanyike siku ya kwanza ya juma yaani Jumapili na siku ya saba yaani Jumamosi kwa kalenda ya kwetu. Pia Mungu hakuwaagiza kukusanyika tu, bali aliwaagiza wasifanye kazi pia. Lakini wanaojiita wasabato nyakati za leo, wanapinga kukusanyika Jumapili sawasawa na maagizo ya torati wanayodai kuifuata.
1. Swali ni kwamba, mafundisho yao ya kukusanyika siku ya sabato yametoka wapi?
2. Kama ni kwenye Biblia mbona siku moja hii wameiacha?
3. Je aliyetoa agizo la siku ya sabato ni Mungu mwingine na aliyetoa agizo katika kitabu cha Kutoka 12:16 (yaani kukusanyka siku ya Jumapili) ni Mungu mwingine?