Monday, October 28, 2013

YESU ANASEMA: MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!


Leo nitajibu haya madai ya Upanga.

Waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya kidini wamekuwa na tabia ya kutumia aya YA UPANGA iliyopo katika Mathayo 10: 34 inayo sema ''MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA! Waislam wanadai kuwa, katika aya hii, Yesu alikuja kuleta UPANGA na si Habari Njema kama tufundishavyo sisi Wakristo.

Kwa kuwa Waislam kazi yao ni kutoa kashfa na kuutukana Ukristo, wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu hufundisha jamii kwa kutumia Qurani na Biblia na kusema kuwa eti Yesu alikuja kuleta UPANGA  na Hivyo Basi Ukristo ni dini ya UPANGA. Fundisho hili la "MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA! " wanalieneza kwa kupitia Mitandao mbalimbali kama ya  Radio, Vijarida, Mihadhara, vitabu na Kanda (cassettes) za Video na Audio. Na hivyo kuwafanya baadhi ya Wakristo kuingiwa na wasiwasi kutokana na jinsi hawa Wahadhiri wa Dini ya Uislamu wanavyo toa kashfa chafu kwa Yesu Kristo ambaye ni Masiah. Na baadhi ya Wakristo wengine ingawa hawajabadili dini wanaamini hivyo. Swali la muhimu la kujiuliza kwa kila Mkristo, je, ni kweli Yesu alikuja kuleta UPANGA? Nakusihi fuatilia somo hili kwa makini ili kujua Ukweli wa aya hii:

Ngoja niiweke hiyo aya:
Mathayo 10:34''MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!

Ukitazama na kusikiliza kwa haraka haraka namna wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu wanavyoifunda hii aya ya Biblia unaweza ukashawishika kuamini hicho wanachokifundisha, lakini ni vyema tukajifundisha kwa undani kadiri maneno ya Yesu kuwa "MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!" kisha tuone kama kuna ukweli juu ya hayo mafundisho yao, ya kusema kuwa Yesu alikuja kuleta Upanga na si kutangaza Habari Njema kwa Mataifa yote. 

Haya tuanze utafiti wetu.
Kwanza tujiuluize, Je, Yesu analeta Upanga wa ainga gani? Yesu anazungumzi Upanga ambao ni “Neno la Mungu”.  Neno la Mungu linagawanya na au kukata Mabaya na kuacha mazuri.  Hebu kwanza tuyasome maagizo yake kwa wanafuzi. Mathayo 10 aya 16: Inasema: Sasa, mimi nawatuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Muwe na busara kama nyoka, na wapole kama njiwa. Katika hii AYA, Yesu anawaambia Wanafunzi wake wawe na Busara na Wapole, Hatusomi katia hii aya kuwa anawaambia wabebe Upanga. Je, Yesu alipo sema Upanga, alimaanisha nini? Hebu tuendelee na somo letu.

Sasa tuangalie aya ya 1 inasema:  “Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote”. Upanga unao zungumziwa hapa ni uwezo ambao Yesu aliwapa Wanafunzi wake. Unaweza kuniuliza uwezo huo ni nini?

Hebu tusome Kitabu cha Waefeso ili tuweze kuelewa nini hasa maana ya Upanga na Uwezo wa kutoa Pepo na Kuponya kama alivyo wapa Wanafunzi wake.

Waefeso 6:17
17 Vaeni wokovu kama kofia ya vita vichwani na chukueni UPANGA wa Roho ambao ni neno la Mungu.
Kutokana na ayah hii ya Waefeso, tumeweza kufunguliwa macho yetu ya Kiroho na kuelewa kuwa UPANGA NI NENO LA MUNGU.
Kwasabau Waislam wanakubali kuwa Yesu kaleta Upanga ambao sasa tunaelewa nini maana yake kutoka na Ushaidi wa Waefeso. Basi leo hii hawa Waislam hawatakuwa na jinsi ya kujitetea bali kukubali kuwa Upanga ambao ni Neno la Mungu ni wa kufuatwa kama alivyo sema Yesu katika Mathayo 10: 34.
Ni matumaini yangu kuwa leo hii umeweza kujua kwa undani maana ya "MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI (UPANGA) NENO LA MUNGU!" na Yesu alipo sema hayo alikuwa anatufahamisha kuwa neon La Mungu ni Sawa na Upanga Mkali unao tenganisha na au toa Mabaya yote kwa Binadamu.

Mungu awabariki sana

Katika Huduma Yake

Max Shimba 


Copyright © Max Shimba Ministries 2013

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW