Wednesday, March 9, 2016

MAJINI MACHAFU NA MASHETANI YANAMWABUDU ALLAH

1. QURAN INASEMA KUWA MAJINI YANAZALIANA NA KUFA KAMA BINADAMU
2. ALLAH AYARUHUSU MAJINI KUZAA NA WAISLAMU
3. QURAN INAKIRI KUWA MAJINI NI MAISLAM NA YALISILIMU PALE QURAN ILIPO TEREMSHWA KWA MUHAMMAD.
4. MAJINI MACHAFU YANAMWABUDU ALLAH
5. KILA MUISLAM AMEPAGAWA NA MAJINI KATIKA MWILI WAKE
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu Majini au Mashetani katika Uislam.
JINI NI NINI?
Katika lugha ya kiarabu, neno Jini linamaanisha kitu kilichofichwa au kisichoonekana QURAN 1:71 Neno hili hutumiwa na Waarabu kwa ajili ya kutaja jina fulani. Kwa Waarabu, Jini anayevaa sura ya kike humwita Jinivya, hivyo majini Ghul/Ghilan, nao hujifunua kwa sura ya kike.
Katika imani ya Kiislamu, wao huamni kwamba Majini hutofautiana na Mashetani. Majini waliosilimu wao huitwa majini mazuri na hawa wakiwa katika hali kujionyesha kwa wanadamu, hao huitwa AJINU na wale walioacha kusilimu mwaka 610 AD (Baada ya Kristo) katika safari ya mtume Muhamad alipotoka Taif , wao wanaitwa Mashetani . Hivyo, wao wanapokuwa katika hali ya kutoonekana huitwa ALBAHATWA lakini pia Majini wote wanapokuwa katika hali ya kutoonekana waweza kuitwa ALBAHATWA, yaani PEPO.
QURAN INASEMA KUWA MAJINI YANAZALIANA NA KUFA KAMA BINADAMU
Muislamu huamini kwamba kuna majini ya kike na kiume. Lakini pia , huamini kuwa Majini huoana na kuzaliana QURAN 55:56 na kuwa Majini huzaa sana kuliko binadamu na kwamba, Jini mmoja anaweza kuzaa watoto 300, na kuwa Jini huzaa watoto 3 hadi 4 kwa mkupuo. Somo QURAN 55:26-28 na kuwa Majini wanaweza kuishi miaka 400-1,000 kisha wanaweza kufa. Tofauti yao na binadamu ni kwamba wao wanaishi miaka mingi kuliko binadamu. Lakini pia, huamini kuwa wapo Majini wanaokula, wanaomeza, wanaokunywa, ila tofauti yao na wanadamu ni kwamba wao hula kwa kutumia mkono wa kushoto.
ALLAH AYARUHUSU MAJINI YANAZAA NA WAISLAMU
Pia hiamini kuwa Majini wana uwezo wa kuzaa na Wanadamu. Soma QURAN 17:64. Waislamu huamini kwamba mtu anauwezo wa kuoa au kuolewa na Jini bila kujua, na mwanadamu anauwezo wa kumuua Jini. Soma QURAN 57:14-15
SURATULJINN
Ndani ya QURAN pia imo sura inayoitwa Suratuljinn (QURAN 72). Sura hiyo huitwa hivyo kwa sababu ni sura ya Majini (Mapepo).
Kwa nini wanatajwa Majini katika imani ya Kiislamu?
QURAN INAKIRI KUWA MAJINI MACHAFU NI MAISLAM NA YALISILIMU PALE QURAN ILIPO TEREMSHWA KWA MUHAMMAD.
Majini wanatajwa sana katika dini ya Kiislamu kwa kuwa ni waislam kwa kusilimu, kwa kuiamini Quran tukufu aliyopewa mtume Muhamad.
Majini walisilimu na kuwa Waislamu mwaka 610 AD(Baada ya Yesu) SOMA 72:1-14 QURAN. Hivyo basi, unapotumia neon jinni maana yake unatumia lugha ya Kiarabu ukimaanisha Pepo mchafu. Ni kama Spoon/kijiko, vyote ni kitu kimoja. Ndani ya Quran, neon “PEPO” limetumika kama Paradiso, mbinguni. Lakini pia, tunapata neon jingine liitwalo AKHERA ila neno hilo halimaanishi PARADISO, bali kwa lugha ya Kiarabu neno hili “AKHERA” lina maana ya KUZIMU.
Lakini pia ukiangalia ndani ya SURALJINN ( QURAN 72:1-2, 8-9, 12 ) Mapepo hawa wanajieleza waziwazi kabisa kuwa mwanzo waliishi Mbinguni, walipogeuka kwa kuasi, walitegwa na Mungu. Linganisha na maandiko haya katika Biblia ( UFUNUO WA YOHANA 12:7-9; YUDA 1:6-8; UFUNUO 20:10; UFUNUO 21:8 ). Kwa mujibu wa dini ya Kiislamu, hawa majini ( Mapepo ) waliotegwa na Mungu Mbinguni wakiwa Malaika huko na kutupwa Duniani baada ya kuasi huko, sasa, wakati wa mtume Muhamad katika safari yake ya kurudi Taif mwaka 620 AD (baada ya Yesu) wapo walioamini na kuona kuwa Quran ni ya ajabu ya kuwatangazia neema ya kuabudu. Katika vol 8-9, husema , wanapojaribu kwenda Mbinguni ( walikotoka zamani ), hukuta ile Mbingu imezungushiwa vimondo vya moto. Hivyo, hudai kuwa mbingu yao iko Akhera, yaani Kuzimu, maana Mbingu ya juu ina moto na hawana uwezo wa kwenda huko. SOMA (QURAN 72:9), Mbingu ina utisho wa moto ila Akhera ( kuzimu ) hakuna shida kwao.
MAJINI MACHAFU YANAMWABUDU ALLAH
Hivyo basi, kulingana na jinsi Allah asemavyo ndani ya Quran kuwa nimeumba binadamu na majini ili muniabudu ( QURAN 57:58 ; 51:56) na kuwa , mbinguni mwao Majini wanaabudu (Majini waliosilimu mwaka 620 AD) ,SOMA QURAN 72:14, ambao ni wema wanaosafiri na kurithi uzima wa milele upatikanao Akhera ( Kuzimu ). Lengo kubwa la Shetani na Majini ni kufanya urafiki na wanadamu wengi ili kwa wingi huo apate watu wengi wa kwenda nao JEHANAMU ( QURAN 6:128 ). Jambo la muhimu kujua hapa ni kwamba moto wa milele hakuwekewa Mwanadamu bali ni Shetani na malaika zake wote ( Majini au mapepo ). Hawa, hawana nafasi tena ya kuungama au kutubu.
Yesu Kristo anayetambuliwa na Waislam kama Mtume tu, hakuwa na urafiki wowote na Shetani wala Mapepo ( Majini ). Aliyaamuru Majini kutoka ndani ya watu waliokuwa wakiteswa nayo ( MATHAYO 8:29: MARKO 5 N,K )
Wakati Yesu anaondoka hapa duniani, alichukuliwa na wingu na kupaa kuelekea juu. Mbinguni ni juu kama Quran inavyothibitisha. Yesu aliweza kupaa na kuingia Mbinguni lakini Majini ( Mapepo ) walioslimu wakijaribu tu, wanakutana na moto mkali. Tumeona kuwa Majini ambao ni Waislamu kwa kusilimu, wanaishi AKHERA yaani Kuzimu. Je, Waislamu wengine unadhani wataishia wapi milele? Katika imani ya Kiislam huamini kuwa, Muislam akifa anakuwa na Majini wawili wa Kumlinda humo Kaburini.
KILA MUISLAM ANA JINI KATIKA MWILI WAKE
Majini wamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote, hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea. Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam. Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo. Ni ukweli usiopingika kuwa bila Majini hakuna Uislamu kama vile pasipo Roho Mtakatifu hakuna Ukristo. Majini ndiyo yaliyomchukua mtume Muhamad kwa muda wa siku 40 akiwa Mabondeni walikompeleka na kuanza kumuagiza kuhusiana na kuanzisha imani hiyo ya Kiislamu.
USHAURI WANGU KWA WA WAKRISTO:
Ushauri wangu wa bure kwa Mkristo ni huu, USIMUACHE KAMWE KRISTO NA KUINGIA KATIKA IMANI ZA MASHETANI (1TIMOTHEO 4:1-2 ).
Majini au Mashetani ni kitui kimoja na wala hakuna tofauti yao. Wote hao Mashetani/Majini yalimpinga Mungu na kutupwa duniani. Biblia inasema kuwa Hakuna Msamaha kwa Majini maana wao walisha hukumiwa na wanacho subiri ni kutupwa Jehannam.
Shetani bado ni “mfalme wa nguvu za anga” (Waefeso 2:2). Hii inamaanisha kwamba Shetani na Malaika wengine walioasi wanaweza kushawishi mia zetu na mawazo yetu kupitia miziki, runinga, mijadala, nk. Tumeambiwa kujihadhari katika mawazo na nia zetu (2Wakorintho 10:3-5). 2Wakorintho 4:4 inatuambia kuwa mungu wa dunia hii amepofusha mawazo ya watu ili wasiamini.
Shetani ndiye yuko nyuma ya dini zote za uongo na dini za dunia. Shetani atafanya na kila kitu katika uwezo wake ili ampinge Mungu na wale wote wanaomfuata. Ingawa hatima ya Shetani imewekwa muhuri kuwa tanuru la moto milele (Ufunuo Wa Yohana 20:10).
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW