Tuesday, March 22, 2016

MTUME MUHAMMAD ALIKUWA ANADAI SADAKA - FEDHA KABLA YA KUONGEA NAE


Ndugu msomaji,
Leo nitajibu hoja ambayo Waislam wamekuwa wakiitumia kwa muda mrefu kuwashutumu Wakristo kuwa tunadai Sadaka kutoka waumini, huku wakificha aya kutoka Quran zinazo onyesha kuwa Muhammad alikuwa anapokea Sadaka.
Watu waliokuwa wakiishi katika zama za Mtume walikuwa wanaenda kwa Mtume katika nyakati tofauti, na walikuwa wanamuuliza masuala tofauti yenye faida na yasiyo na faida, na suala hili lilisababisha kumkosesha Mtume wakati wa mapumziko, ndipo ilipokuja Qur-ani na kuwaamrisha watu kuwa kila anayetaka kuuuliza suala basi kwanza anatakiwa kutoa sadaqa, kabla ya kuuliza suala lake. Na Aya hiyo iko katika (Surat Mujadila aya ya 12) inasema hivi:-
يَا اَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَاجَيْتُمُ الرَّسُولَ فَقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيْ نَجْوَاكُمْ صَدَقَةً ذٰلِكَ خَيْرٌ لَّكُمْ وَاَطْهَرُ فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فَإِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ[1]
Maana ya Aya hiyo ni kama hivi ifuatavyo:-
“Enyi mlioamini! Mnapomsemesha Mtume Muhammad toeni Sadaqa kabla ya kumsemeza; hayo ni bora kwenu na ni ya kukusafisheni sana. Ikiwa hamkupata (cha kutoa), basi Mwenyeezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu”.
Kwa amri hiyo basi, wao wenyewe wakawa ni wenye kurudi nyuma, na ni mtu mmoja tu ndiye aliyekwenda kwa Mtume (s.a.w.w), na kumuuliza masuala baada ya kushuka Aya hii, naye alitoa dirham kumi, kisha akauliza masuala muhimu ya kidini mbele ya Mtume (s.a.w.w). Naye alikuwa ni Dinar ambaye ni Mtumishi wa Imam Ali bin Abi Talib (a.s).
Lakini watu walipo gundua kuwa Muhammad alikuwa mtume bandia na anatumia sadaka kulisha famila yake kubwa, Allah akashusha aya kama ifuatavyo, nayo ni (Aya ya 13 ya Surat Mujadilah) isemayo:-
اَاَشْفَقْتُمْ اَن تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيْ نَجْوَاكُمْ صَدَقَاتٍ فَإِذْ لَمْ تَفْعَلُوا وَتَابَ اللهُ عَلَيْكُمْ فَاَقِيمُوا الصَّلاَةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَاَطِيعُوا اللهَ وَرَسُولَهُ وَاللهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ[2]
Maana ya Aya hiyo ni kama hivi ifuatavyo:-
“ Oh! Mnaona tabu kutanguliza hiyo Sadaqa kabla ya kumsemeza kwenu? Ikiwa hamjafanya haya basi. (Yamekwisha hayo). Na Mwenyeezi Mungu amekusameheni. Basi simamisheni sala na toeni Zaka na Mtiini Mwenyeezi Mungu na Mtume wake. Na Mwenyeezi Mungu anayo habari ya mnayoyatenda yote”.
Kama tulivyo soma hapo kwenye Surat Mujadilah aya ya 13, Muhammad kagonga mwamba, baada ya Waarabu kumshtukia kuwa Muhammad alikuwa anakula fedha zao kwa kuwapa unabii wa uongo.
Hebu soma kwanza:
17. SURA AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
90. Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii.
91. Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu, na utupitishie mito kati yake ikimiminika.
92. Au utuangushie mbingu vipande vipande kama ulivyo dai; au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika uso kwa uso.
93. Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upae mbinguni. Wala hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie kitabu tukisome. Sema: Subhana Rabbi, Ametakasika Mola wangu Mlezi! Kwani mimi ni nani isipo kuwa ni mwanaadamu na Mtume?
(Qur-Sura 17:90-93)
Baada ya kuombwa afanye angalau muujiza mmoja tu, Muhammad alishindwa vibaya sana na kuto fanya hata muujiza mmoja.
Swali:
1. Kwanini Muhammad alishindwa kufanya miujiza kama alivyo ombwa afanye?
2. Muhammad ni Nabii peke yake alieshindwa kufanya Miujiza tokea dunia iumbwe, Je, anaa kufuatwa na kuaminiwa?
3. Kwanini Allah nay eye hakumsaidia Nabii wake kufanya muujiza?
HAKIKA MUHAMMAD ALIKUWA NABII WA UONGO
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 22, 2016

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW