Sunday, June 19, 2016

SHEHE OMARI ASEMA QURUANI IMEJAA UCHAWI NA USHIRIKINA

SIRI YA WATOTO WA DAWA YAWEKWA HADHARANI NA SHEIKH OMARI
**********************************************************************************************
Sheikh Omari akifundisha hapo jana kanisa la Ufufuo na Uzima Kawe jijini Dar es salaam.
Shehe Omari akielezea jinsi alivyokuwa akitengeza watoto dawa na Dalili zake.
Kwasababu ya mila nyingi za kiafrika, watu wengi sana wamejikuta wakikimbilia kwa waganga pale wanapogundua kukosa mtoto. Wakati ninasomea falaki nilijifunza namna 11 jinsi ya kumpatia mwanamke mtoto hata kama hana uwezo wa kuzaa. Wakati nikiwa mkuu wa chuo cha kichawi pale temeke, tulikuwa tukifundisha watu kwa habari ya mimba za kijini.
Kwa wakati mteja alipokuwa ananijia kwaajili ya kuaguliwa, jinni ambalo lilikuwa ndani yangu lilikuwa linapanda ndani yangu na kwenda na kumwendea mteja alafu husoma taarifa ya mteja. Baada ya muda hutoka kwa mteja na kurudi kuja kuniambia mimi tatizo la mgonjwa huyo. Baada ya hapo nilikuwa namtajia mteja tatizo lake na kumfanya aniamini kuwa nitatatua tatizo lake hapo kila nitachomwambia lazima atafanya.
Baada yakuupata (win) moyo wa mteja, nilikuwa namwagiza vitu mbalimbali vya kufanya na kuniletea kwaajili ya uaguzi. Baada ya siku kadhaa lazima mteja huyo (ambao wengi wao walikuwa wanawake) atarudi kwaajili ya uaguzi. Katika namna hii ya kwanza ya kutengeneza mtoto wa dawa; tulikuwa tunaingiza jini ndani mwanamke na jinni yule alikuwa na uwezo wa kwenda kuiba mtoto katika nyumba ya mtu wa karibu na kumwingiza katika tumbo la mwanamke yule. Matokeo ya aina hii ya mtoto wa dawa ni uwezekano wa wazazi wakitanzania kujikuta wamezaa mzungu au mtoto mwenye sura ya jirani yake.
Madhara ya aina hii, husababisha ile mimba ambayo imeibiwa kwa mtu wajirani kupotea. Na ndio maana unaweza kumwona mtu alikuwa mjauzito lakini baada ya muda mimba ile ikapotea. Na ikitokea yule jini ameshindwa kumpatia mtoto kutoka katika maeneo yale, huamua kujitengenezea nyama kutoka katika mwili wa mwanamke. Matokeo ya aina hii mwanamke anasumbuliwa sana na mimba; unaweza kuta ni muda mfupi tu wa ujauzito lakini mwanamke huyo anakuwa ameshasumbuliwa sana na magonjwa mbalimbali.

Hivyo mtoto kama huyo akizaliwa anakuwa mwili ni binadamu lakini katika roho ni jini asilimia mia moja.
Dalili za kumtambua mtoto wa dawa wa aina hii:-
1. Macho yake hayachezi mfano akigeuka huwa anageuka na shingo yote
2. shingo yake huwa inageuka polepole haigeuki kwa haraka.
3. Macho yake huwa yanameza picha/ ukiangalia kwenye kiini cha jicho lake hakionyeshi picha.
4. Safari zake za muhimu (anazozisisitizia) huelekea upande ambao haangaliani na jua.
5. Ana sifa nyingi zilizojificha/ anaweza kuwa na elimu ya juu lakini haionekani.
6. Huwa anafanya jambo zuri lakini hazingatii wakati:- mfano inawezekana wamekuja wageni nyumbani alafu yeye ndio akaanza kufagia muda ule.
7. Yeye ni mtendaji mzuri sana lakini hapendi kukubaliana. Ya
ani kama ni mtoto unaweza ukamwachia kazi afanye yeye akakataa kwa muda ule lakini jioni ukija utamkuta amefanya vyote.
8. Kwenye mikusanyiko mingi hupenda kuwa wa mwisho kutoka.
9. Ukimwangalia kwenye kipaji cha uso; kama una nguvu za Mungu utamwona kama nyama yake inatetemeka/ inatikisika
10. Huwa hafi. Kwasababu huyu ni jini hivyo hutumika katika mwili kwa muda fulani lakini baada ya muda hupotea tu bila kuonekana.
Hizo ni dalili za mtoto wa dawa anayetengenezwa kwa namna hii:
Swali: kuna madhara gani kwa wanafamilia?
Wanafamilia wanaoishi naye watapata madhara, kwasababu jini/mtoto huyu anaweza kuwa maskani ya majini na mapepo wachafu katika familia. Nakumbuka alikuwepo mama mmoja tanga tuli tulimtengenezea mtoto wa namna hii. Baada ya muda mama yule aliokoka lakini yule mtoto hakuwahi kulipuka mapepo na mara nyingi inaghalimu msaada wa Roho mtakatifu kumsaidia mtu wa namna hii.
Swali; Jini hili laweza kukua na kuwa kiongozi au kuoa?
Kiukweli linaweza kabisa kuwa kiongozi, mbunge, waziri au hata rais. Pia linaweza kuoa pia na kuzaa watoto pia; mfano mwanaume wa kijini akioa mke wa kawaida watoto wake watakuwa na ujini sana. Lakini kama mwanamke ni jini na mwanaume ni binadamu watazaa watoto wanaowasumbua sumbua sana.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW