Saturday, June 4, 2016

USTAADH NA HAKIMU WA MAHAKAMA YA KADHI AOKOKA NA KUSEMA KUWA UISLAM NI NJIA YA KWENDA JEHANNAM – Sehemu ya 1

Ahmed alikuwa ni injinia. Baadaye alishawishiwa na Ulama mmoja na kupandikiziwa chuki dhidi ya Wakristo na Wayahudi kiasi kwamba aliamua kuacha kazi yake na kwenda kusomea masomo ya dini ya Kiislamu (licha ya mama yake kupinga sana).
Masomo hayo yalimwezesha kuwa hakimu wa mahakama ya sharia. Kutokana na ukandamizaji mkubwa aliouona kwenye mahakama hizo na kukosekana kwa haki na pia kukosekana kwa msimamo juu ya tafsiri sahihi ya sheria za kiislamu, moyo wake ulikosa kabisa amani.
Kwa neema za Yesu Kristo, Ahmed alifunguliwa macho yake na sasa anajiuliza ilikuwaje akaamini Uislamu?
Ufuatao ni ushuhuda wake kwa maneno yake mwenyewe ambao ameupa kichwa cha habari: “Njia ya Allah Kuelekea Jehanamu au Njia ya Yesu Kuelekea Mbinguni.”
*********************
Njia ya Allah Kuelekea Jehanamu au Njia ya
Yesu Kuelekea Mbinguni
Hadithi ya Kweli
Kila kitu kilikuwa kinaniendea vizuri wakati mimi (mhandisi wa ujenzi) nilipokuwa naingia ofisini kwangu kila siku kufanya kazi. Baba yangu alikuwa karani, na japo mshahara wake hakutosheleza, mama yangu, ambaye alikuwa akitembeza vitu mtaani, aliweza kupata kipato kilichojazia kwenye upungufu. Kimsingi, alikuwa ni mama ndiye aliyetulipia watoto wote elimu yetu na matunzo. Nilipopata kazi, nilimpunguzia mama mzigo mkubwa wa matumizi, lakini baba yangu nilimpa kiasi kidogo tu kila mwezi.
Dunia yangu iligeuka ghafla pale nilipokutana na Ulama (mtu mtakatifu wa Kiislamu). Alinieleza jinsi Waislamu wanavyonyanyaswa na dini zingine na jinsi dunia ilivyosimama kinyume na Uislamu, huku Marekani ikiwa ndio kinara wa mambo hayo. Aliniambia kuwa Marekani, kwa makusudi, inalazimisha kuwapo kwa haki za binadamu kila mahali, maana ziko kinyume na sehemu kubwa ya imani ya Kiislamu, hivyo hilo linaufanya Uislamu uonekane umepitwa na wakati. Wayahudi nao wanawalaghai Wamarekani kwa ajili ya maslahi yao ili kuidhibiti Mashariki ya Kati. Allah alishaliona hili, na kusema kwenye Sura 5.51 ya Quran, kuwa tusiwe na urafiki na Wayahudi na Wakristo. Lakini nchi za Kiislamu zinaikubalia tu Marekani.
Kukosekana kwa Maustaadh (walimu wa dini) kwenye eneo langu, kunakowanyima Waislamu welewa wa kutosha juu ya uzuri na maajabu ya Uislamu, lilikuwa ni jambo jngine tuliloliongelea kwa kirefu sana. Baada ya mazungumzo ya ushawishi ya miezi kadhaa, niliulizia kwenye mji mkuu na nikapata taarifa zote kuhusiana na kujiunga na chuo cha kiislamu. Baada ya kujiuliza sana, ikiwa pamoja na chuki iliyopandikizwa ndani yangu, niliamua kuacha kazi yangu ya uhandisi, lakini mama yangu alipinga kabisa. Lakini mwishowe niliweza kumshawishi kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya Allah, hivyo nikaenda kujiunga na Chuo cha Kiislamu.

Baada ya kuhitimu kama Ustaadhi, mara moja nilipangiwa kwenye eneo langu. Hakukuwa na shule maalum ya Kiislamu, hivyo mwanzoni, niliendesha masomo nyumbani kwangu. Japokuwa nilikuwa nina welewa wa kutosha juu ya elimu ya Uislamu, lakini kulikuwa na nyakati ambazo nilikuwa nakwama kujibu maswali ya wanafunzi. Matokeo yake nilianza kuongezea uongo hapa na pale kwa nia ya kumtetea Allah. Ukweli ni kwamba, wakati wa masomo yangu ya Uislamu chuoni, kulikuwa na mambo mengi ya kukisia tu yasiyokuwa na ushahidi. Pale mikanganyiko ilipoibuka ndani ya Quran, ilimalizwa tu kwa kusema ‘Allah anajua zaidi,’ au kwa kuchanganyachanganya na baadhi ya Hadith, hivyo kufikia namna fulani ya jibu linalokubalika.
Waislamu wengi wanajua kusoma Kiarabu kwenye Quran lakini , kwa ujumla, hawaelewi kile wanachosoma. Kwa hiyo, kwa ujumla Muislamu huwa hajui kile ambacho Quran inasema, hivyo anahitaji Ustaadhi wa kumwelezea kile kilichomo. Hivyo, huku kuchanganya maelezo na uongo lilikuwa ni jambo la kawaida kwa ajili ya Allah. Kusema uongo ikawa ni tabia yangu kiasi kwamba, hata mimi mwenyewe, nikaanza kuuamini huohuo uongo wangu. Chuki dhidi ya kitu chochote kisicho Uislamu ilikuwa ni sehemu ya mafunzo niliyopata.
Safari yangu kwenda Makka kwa ajili ya hija ilikuwa ya kuchosha lakini yenye matukio mengi. Sikupata fursa adimu ya kuangalia ndani ya Kaabah takatifu na miungu (idols) mitakatifu iliyomo humo ndani, ambayo mtume Muhammad alisaidia kuiweka humo, kama ilivyoelezwa na Hadithi za Bukhari. Lakini, nilikuwa najiuliza kwa nini shughuli ya kumpiga mawe shetani kimfano (kwa kupiga mawe nguzo iliyo kwenye shimo) ilikuwa ni ya muhimu sana kwenye sehemu hiyo. Nilihisi kuwa ilitosha tu kuangalia utakatifu na si kuwa na shughuli inayomhusu shetani kwenye sehemu ile, hususani Makka! Kutokana na joto kali, kila mmoja alikuwa anatoka sana jasho na ananuka. Lakini mkusanyiko wa watu zaidi ya milioni moja ulikuwa wa kushangaza na wenye vurugu. Baada ya kurudi kutoka Makka, nilianza kuvaa kofia nyeupe ili kuonyesha kwamba nimeshatimiza mojawapo ya nguzo 5 za Uislamu (yaani kwenda kuhiji Makka).
Miezi miwili baadaye, baba yangu alinitembelea ili kutaka nimuunge mkono juu ya wazo lake la kutaka kuoa mke mwingine. Ili kuhalalisha suala lake, aliniambia kuwa tayari alishampa mimba huyo msichana wa miaka 19. Nilighadhibika mno! Lakini sasa Hadithi katika Bukhari zinaniambia kuwa Allah aliumba wanawake kama ‘vitu vya kuchezea’ kwa ajili ya wanaume. Hata hivyo, nilipomtafakari mama yangu alivyohangaika kutulisha na kutusomesha, nilimhurumia sana. Bila yeye, baba yetu asingeweza kutulisha, kutusomesha, na kutuvika sisi watoto wake. Kutokana na usaidizi wa mama yangu, baba aliweza hata kufurahia maisha, na baada ya kumtumia kwa miaka hiyo yote, alikuwa sasa anataka mke mwingine dogodogo, akiwa na umri ulio chini ya nusu ya umri wake, na mdogo kuliko watoto wake wote watano!
Lakin Allah ni wa rehema na amewapa wanaume upendeleo kuliko wanawake, maana mwanamume anaweza kuwa na wake hadi wanne kwa mara moja. Pamoja na kuwa nilitafuta kila sababu ya kutomwunga mkono baba yangu, nilizungumza na mama yangu juu ya jambo hilo. Alilia sana; na hata kazini hakwenda siku hiyo. Tulijadili kwa kirefu suala la mke wa pili. Aliposema kuwa hatakubaliana na kuwapo mke wa pili, nilimwambia kuwa hakuwa na namna, maana baba angeweza kumtaliki bila ridhaa yake na bado akamwoa mwanamke huyu. Na hiyo ina maana kuwa, mama angetakiwa kuondoka na kuwaacha wanawe, kwa kuwa katika Uislamu watoto ni wa baba na si wa mama. Jambo hili lilimwumiza hata zaidi.
Wakati baba yangu alipomleta mkewe mpya nyumbani, mama yangu alitumia muda wake mwingi nje ya nyumbani, lakini huku akileta fedha kidogo tu. Hali hii ilimfanya baba yangu awe na mzigo mkubwa zaidi, maana hakuwa na fedha za kutosha kwa ajili yake mwenyewe; na kila wakati mama alipokuwa nyumbani, hali inakuwa ni kama uwanja wa vita. Sisi watoto tulilikuwa tukibakia tu na mama yangu, na kumwacha huyu mwanafamilia mpya peke yake hadi pale baba anaporudi nyumbani kutoka kazini.
Wakati huu, nilipandishwa cheo, na kulikuwa na wakati ambapo nilikaa kama hakimu wa mahakama za sharia (Mahakama ya Kiislamu). Uzoefu niliopata kutokana na mkasa wa mama yangu mwenyewe, ulikuwa kila wakati umo moyoni mwangu, na sikuweza kukubaliana kabisa na amri za Allah na kupuuza upendo, huduma na umuhimu ambao mama yangu alitupatia sisi sote. Hali hii ilikuwa na athari kwenye utoaji wangu wa hukumu kwa baadhi ya kesi katika mahakama za sharia. Nimeshuhudia kiburi na majivuno ya wanaume dhidi ya wake zao wa kiislamu, na wengi wa wanawake hawa, kama ilivyokuwa kwa mama yangu, walichangia sana kwa ajili ya watoto wao na nyumba zao, na waliletwa kwangu huku mara nyingi wakiwa wamepigwa sana, yote haya yakiwa yameruhusiwa kwenye Uislamu na Allah.
Kwa mara ya kwanza, nilidhani kuwa haya yalikuwa mambo tu ya kipekee na nikawaza kuwa Allah hawezi kukosea katika amri zake. Lakini kadiri nilivyoendelea kuona wanawake zaidi na zaidi (mara nyingi wakiwa na umri wa miaka 35 na zaidi; na mmoja alifika mahakamani akiwa amefungwa POP kwenye mkono wake mzima wa kushoto na mguu wa kushoto, huku akiwa kwenye kiti cha magurudumu), mimi nilianza kuwa na mashaka, na nilianza kusoma sana vitabu vya Kiislamu kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi bora na wenye utu kuhusiana na jinsi wanawake wa Kiislamu wanavyotendewa na waume zao, na tabia ya wanaume wa Kiislamu kutoa talaka kirahirahisi, n.k, lakini bila mafanikio yoyote. (Ndoa katika Uislamu si sakramenti mbele za Mungu, lakini ni mkataba tu wa kawaida – mara nyingi ukifanyika kwa mdomo tu - kati ya muoaji na baba wa mwanamke au mzee wa karibu; na mkataba huu unaweza kuvunjwa wakati wowote anapoamua mume, bila ridhaa ya mke wake. Hali hii mara ilinifanya nikasirike sana, maana katika ujana wake, mwanamke anakuwa ametumiwa kama mke wa upendo, kisha anakuja kutelekezwa tu baadaye, kama karatasi ya chooni). Lakini, sikuweza kupata suluhisho lolote lenye utu dhidi ya unyanyasaji huu na suala lililozagaa la talaka katika Uislamu. Hili lilinizidishia tu hali ngumu.
Siku moja niliitwa kwenye ofisi ya mufti. Niliambiwa niunde kamati ya kujaribu kusanifisha (to standardize) hukumu za mfumo wa mahakama wa Kiislamu unaotumika katika mahakama za Sharia. Unajua, kwa sababu Qur'ani, Hadith, na Sunah hazisemi kwa hakika nini cha kufanya (kwa mfano, Allah anasema katika Sura 4.34, kwamba 'mke mkaidi ni lazima apigwe na mume wake na kutengwa hadi ajirekebishe. Lakini haisemi kwamba apigwe mara ngapi, sehemu gani ya mwili wake, apigwe lini, kama ni mjamzito au la, kwa lazima au la, kwa mikono au mjeledi, kwa sababu zipi, nk. Suala hilo limeachwa mikononi mwa mume kuamua. Mara nyingi walikuja kwetu wanawake na kutuonyesha alama za vipigo kwenye miili yao, lakini hakukuwa na kitu katika Uislamu cha kukomesha hali hii, isipokuwa pale ambapo mwanamke alivunjwa mifupa, ambapo nako tulimshauri tu mume, kama ilibidi).
Kama mashahidi 4 walitoa ushahidi wa wizi wa mwanamume na mkono wake wa kulia ukakatwa kama adhabu, na wakati mwingine baadaye, ikiwa mmoja wa mashahidi alikiri kutoa ushahidi wa uongo chini ya shinikizo (maana kushuhudia uongo ni jambo la kawaida katika mahakama za sharia), matokeo yake nini basi? Kulikuwa vurugu nyingi kutokana na kwamba mahakimu tofauti wanatafsiri Uislamu kwa namna mbalimbali. (Uislamu hauko wazi kupokea mawazo ya sasa, kama kutumia DNA, au mifumo ya uhasibu, au uhalifu wa kwenye mtandao, n.k. lakini umeng’ang’ania mifumo yenye umri wa miaka 1,100 toka kwa mababu, na kutaka itumike kwenye maisha ya leo).
Watuhumiwa katika mahakama zetu walianza kuchagua kuwapo wakati kukiwa na baadhi ya majaji na kutokuwapo kukiwa na majaji wengine. Hivyo, unaweza kuwa na msururu mrefu kwa ajili ya majaji wachache lakini hakuna kesi kwa majaji wengine. Wanasheria hawakuhitajika katika Uislamu, lakini huwa tunapata mashahidi wa uongo wengi wanaokuja na kuwatuhumu kwa mambo mbalimbali watu ambao wana uhasama nao. Nilipoanza kazi yangu kwa kusanifisha hukumu, nilianza kupata matatizo mbalimbali, hoja mbalimbali, n.k. kutoka kila upande na nikaishia tu kuchukiwa na wengi. Hakukuwa na mahakimu wawili ambao walikuwa wanatafsiri kwa namna ileile Qur'ani na adhabu zinazotakiwa kutolewa. Hawakuweza hata kukubaliana juu ya mtazamo mpana wa tafsiri na adhabu (kwa mfano, muda wa chini au wa juu wa kifungo cha mtu gerezani, nk). Malalamiko makuu kutoka kwa majaji hao yalikuwa ni kusema, ‘hili halimo ndani ya Quran.’
Mwishowe, mpango ule mzima uliondolewa, na Haki za Kiislamu ziliruhusiwa kutolewa kulingana na tafsiri na welewa wa kila hakimu kuhusu Uislamu; na machafuko yanaendelea hadi leo hii. Mimi nilivunjwa sana moyo kusema kweli. Kusema kweli, kwa kila kushindwa kwa Waislamu, kuna angalau ‘conspiracy’ moja ya Wakristo/Wayahudi inayowalaumu Waislamu.
Waislamu hawatakaa wakubali kwamba mfumo wao wa utoaji haki wenye umri wa miaka 1,100 umepitwa na wakati. Ni rahisi kwao kulaumu nchi za Magharibi na kusema, 'Hawauelewi Uislamu', kuliko kujaribu kuhalalisha Uislamu, kwa sababu Waislamu wanajua kwenye akili zao kuwa, mfumo huo utaonekana kuwa wa kikatili (barbaric) na uliopitwa na wakati, na pia kwa sababu Qur'ani yenyewe inapingana na aya zake zinaweza kutafsirika kwa namna nyingi (open ended), na pia kutojua maana halisi ya aya katika Qur'ani. Kwa hiyo, ni rahisi kulaumu nchi za Magharibi kuwa 'hazina welewa' na kuwaacha wakishangaa, wakati ukweli ni kuwa nchi za Magharibi ziko sahihi kabisa kuhusiana na mawazo yao juu ya Uislamu.
Kwa vile Qur'ani ina kupingana kwingi pamoja na mambo ambayo yamepitwa na wakati, Mwislamu kamwe hawezi kujadiliana na asiye Mwislamu, kwa sababu yule asiye Mwislamu anaweza kutumia Quran dhidi yake. Kwa hiyo, inakuwa ni bora tu kusema, 'Wewe haujui uzuri wa Uislamu’ ili kukwepa aibu. Huu ndio mtazamo wa Mwislamu wa kawaida. Kwa ujumla, Mwislamu hawezi kustahimili mzaha. Huu ndio ukweli wenyewe. Ukiendelea kubishana naye inakuwa ni afadhali kwake). (Nenda kwa tovuti www.answering-islam.org na uone mwenyewe orodha ndefu ya utata ulio ndani ya Quran).
Siku moja, mimi nilimkuta mama yangu akimeza vidonge na nikaja kugundua kuwa vilikuwa vya kuondoa maumivu. Nilimpeleka hospitali kufanyiwa vipimo na akakutwa ana kansa. Ni lazima alikuwa nayo kwa muda mrefu, maana ilishaenea kote mwilini. Aliteseka kila siku. Miaka miwili baadaye, alifariki. Sisi ndugu tuliumia sana. Ulimwengu wangu ulibomoka kabisa kutokana na tukio hili. Nilijaribu kujisahaulisha kwa kufanya kazi, lakini nikawa nachanganyikiwa zaidi na zaidi kutokana na kukosa majibu sahihi.
Kwa mfano, ubakaji ulihitaji mashahidi 4 ili kumtia hatiani mbakaji, kitu ambacho kimsingi hakiwezekani. Kwa hiyo, mara zote nililazimika kuwaachia huru wabakaji. Na wakati mwingine, mbakaji huyohuyo aliletwa tena mahakamani baada ya kumbaka msichana mwingine, na bila mashahidi 4, sikuwa na cha kufanya zaidi ya kumwacha huru tena. Maisha ya wasichana wasio na hatia yanaharibiwa kwa jina la Uislamu. Japokuwa nilijua fika kwamba huyu ni mbakaji, lakini bado Uislamu haukuruhusu mimi kuona haki ikitendeka. Mbaya zaidi, ikiwa mahakama ya Kiislamu haikulichukulia hilo kuwa ni tukio la ubakaji, basi msichana aliyebakwa anahukumiwa kupigwa mawe hadi kufa kwa ajili ya kupata mimba nje ya ndoa.
Yule bibi wa Kikristo jirani yangu, aliyeishi nyumba chache tu kutoka kwangu, aligundulika kuwa ana kansa. Familia yake ya Kikristo iliomba kwa Isa Al-Masih (Yesu Kristo) kila usiku ili aweze kupona haraka kule hospitalini. Niliwaza kuwa walikuwa wanapoteza tu muda, kwa sababu bila ya huruma za Allah, ni lazima tu bibi angekufa. Lakini wiki tatu baadaye, nilishtuka nilipomwona mwanamke huyo akishughulikia maua yake mbele ya nyumba ya mtoto wake.
Nilipiga moyo konde na kwenda kuongea naye. Aliniambia kuwa, kwa neema ya Yesu Kristo aliye Bwana, maombi yake yalijibiwa, na sasa yeye alikuwa amepona kikamilifu. Mwanawe alitoka nje na kunikaribisha ndani kwa ajili ya kunywa chai. Baada ya kuzungumza kwa kirefu, nilirudi nyumbani kwangu nikiwa nimechanganyikiwa huku nikijiuliza, kwa nini Allah hakumwangalia mama yangu, ambaye alikuwa Mwislamu nzuri, mwenye umri mdogo, na asiye na dhambi, lakinibadala yake huyu bibi mzee, ambaye ana imani kubwa kwa huyu Isa Al- Masih (Yesu Kristo) aliponywa kabisa? Niliwaza, huenda hii ikawa ni kazi ya shetani.
Siku ya pili, mawazo juu ya huyu bibi hayakunitoka kabisa. Niliamua kuwa ni lazima nipate jibu juu ya suala hili. Baada ya kutoka kazini, nilienda tena kwenye nyumba hii ya Wakristo kwa lengo la kuonyesha kuwa hii nadharia ya huyu Yesu Kristo si ya kweli na pia kwenda kuwaomba wanipatie Injili yao (Agano Jipya).
Mwanzoni, walikuwa wanasitasita, maana nchi yangu ni nchi ya Kiislamu, na kuhubiri Ukristo kwa Mwislamu kutasababisha kupata kila aina ya adhabu. Baadaye, mtoto wa kiume katika familia hii ya Kikristo aliniashiria kwa macho Biblia yake iliyokuwa juu. Niliichukua (Hii ilimaanisha kuwa hakunipa yeye, bali niliichukua kwa ridhaa yangu kutoka kwenye nyumba hiyo. Hivyo, asingetuhumiwa kwa kunipa vitu vyenye kufuru).
Usiku ule nilisoma Injili ya Mathayo na kupitia sehemu zingine mbalimbali za Biblia. Nilishangaa kwa jinsi Biblia ilivyokuwa imeandikwa kwa mpangilio mzuri, na ilikuwa rahisi kufuatilia mambo yaliyoandikwa humo. Lakini ninahitajika welewa zaidi juu ya mambo yaliyomo humo na umuhimu wake. Kwa hiyo, nilianza kwenda mara kwa mara kwenye nyumba hii ya Wakristo, lakini nyakati za usiku, ili majirani wasije wakanishuku. Kutokana na kujua nafasi yangu katika jamii, wenyeji wangu walikuwa na wasiwasi wa kitendo changu kuwaingiza kwenye matatizo. Siku zikawa wiki, na nilikuwa nikiwahi nyumbani kila siku ili kwenda kusoma zaidi Biblia. Nilipenda sehemu ambapo Yesu Kristo anasema, yeyote asiye na dhambi awe wa kwanza kumpiga jiwe mwanamke aliyekamatwa kwenye uzinzi. Kuna upendo mwingi sana kwa ajili ya kila mmoja katika Injili (Agano Jipya). Mahangaiko yote na msongo uliokuwa ndani yangu ulianza kupungua, kadiri nilivyoendelea kujisikia amani na utulivu kwa huyu Yesu Kristo. Lakini chuki yangu dhidi ya dini zote nyingine ilikuwa bado imo ndani yangu.
Mimi daima nimekuwa nikijiuliza, kwa nini ni wanawake wa kiislamu tu ndio huona vivuli ya mizuka na kupagawa ama kwa pamoja au mmoja mmoja katika madarasa, viwanda, nk iwe ni usiku au mchana? Hili si tu ni jambo la kawaida katika nchi yangu, lakini katika nchi nyingine pia. Mwislamu hatakiwi kupiga au kuweka picha ya kitu chochote hai (ikiwa ni pamoja na wanadamu), na jambo hili kwangu nililiona halina maana, kwani ningependa kuweka picha za familia yangu kwa ajili ya uzao wangu. Dome of the Rock katika Yerusalemu ilijengwa takriban miaka 60 (685-691 BK) baada ya Mtume Muhammad kufa (Juni 8, 632 BK kule Makka). Hakukuwa na kitu cha maana kuhusiana na Uislamu katika Palestina wakati wa kifo chake. Basi kwa nini mwili wa Mtume Muhammad kwenda Yerusalemu kupaa hadi Mbinguni, wakati ingefaa zaidi apae kutokea Kaabah kule Makka, ambako ndiko mahali patakatifu zaidi katika Uislamu? Mashaka haya makubwa daima yalinisumbua, na hakukuwa na majibu, hata kutoka kwa wenzangu wakubwa na na wenye hekima zaidi.
Ushuhuda huu umetafsiriwa kutoka kwenye Kiingereza. Kama ungependa kuusoma kwa Kiingereza, tafadhali bofya HAPA.http://islamreview.com/category/testimonials/

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW