Thursday, June 2, 2016

ALLAH AWALAANI WANAWAKE WANAO JIPAMBA NA KUJIPODOA, ASEMA KUJIPAKA MANUKATO NI KUWA KAMA MALAYA


1. Allah awakataza Wanawake kuvaa Wig
2. Allah awakataza Wanawake kujipaka Manukato.
3. Allah awakataza Wanawake kujipodoa.
Ndugu zanguni,
Leo ningependa tujifuze kidogo kuhusu mapenzi ya Allah kwa Wanawake alio waumba.
Hebu twende moja kwa moja kwenye Ushahidi:
Allah Anasema:
“Wala wasionyeshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika. … Na wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao…” (24: 31).
Pambo la mwanamke linajumlisha sehemu zake za kimaumbile kama uso, nywele na sehemu nyingine za kuvutia za mwili wake na nyongeza za uzuri wa bandia kama nguo, vito vya thamani, vipodozi na mfano wake. Haifai kwa mwanamke yeyote Muislamu kutoka nyumbani kwake akiwa amejipaka vipodozi au manukato.
ALLAH ASEMA WANAWAKE WANAPO TUMIA MANUKATO WANAKUWA NI SAWA NA MALAYA
Mwanamke wa kiislam anapo-tumia manukato mwilini mwake anakuwa Malaya....
Mishkat al-Masabih – vol 2, p. 255
MTUME MUHAMMAD ASEMA KUVAA WIGI AU NYWELE BANDIA NI HARAM
Mtume (s.a.w.w) amewataka Wanawake wazikirimu nywele zao kwa kuzitazama vyema, kuzipata mafuta na hata kuzitia henna na katm (mmea kutoka Yemen). Inafahamika kuwa mafuta, henna na katm zinabadilisha umbile la nywele, kwani zote hizo zina kemikali. Dawa za nywele zinaweza kutumiwa ikiwa zitabaki katika misingi ya Uislamu, miongoni mwayo ni: -
Na Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Haifai kudhuru wala kulipana madhara” (Ibn Maajah na ad-Daaraqutniy).
Ikiwa zitamlazimu kutotia maji kichwani, hivyo hutaweza kutawadha wala kuoga na Swalah zitakuwa ni zenye kukupita au kupoteza mda mwingi kuwa katika saloon ili kutiwa hizo dawa badala ya kutekeleza mambo muhimu. Pia jambo hili litakufanya kutoweza kutekeleza haki zako kama mke kwa mume ambayo ni ‘Ibadah na thawabu kubwa.
Na ifahamike kuwa mambo ya mapambo ya nywele ambayo yamekatazwa kabisa na sheria ya Kiislamu. Mfano wake ni kukata au kukatwa nyusi kwani katika hili Mtume (s.a.w.w) amemlaani mwenye kukata na mwenye kukatwa.
ALLAH AMELAA NI WANAWAKE WANAO KATA NYUSI. ALLAH ASEMA HUKO NI KUBADILISHA MAUMBILE ALIYO UMBA ALLAH
((Allah Amemlaani mwanamke anayefanya tatoo (chanjo za kujichora) Na mwenye kuomba kufanyiwa, na anayetoa nyusi na mwenye kuomba kutolewa na anayechonga meno kuweka nafasi (mwanya), kubadilisha maumbile ya Allah kwa ajili ya kupata uzuri)) Al-Bukhariy Imetoka kwa 'Abdullah Ibn Mas'uud (r.a.)
MUHAMMAD ASISITIZA KUWA KUVAA WIGI NI HARAMU NA ALLAH HUTEREMSHA LAANA YAKE KWAKO
Na pia Uislamu umekataza mtu kuvaa wigi au kuongeza vipande vya nywele ikiwa ni za kwake au za mtu mwingine au ni za bandia. Mtume (s.a.w.w.) amewalaani wanawake wenye kazi ya kuunganisha (kutia) watu wigi (au vipande vya nywele) na wanawake wenye kuungiwa hizo nywele.
((Mwanamke wa Ki-Ansari aliyemuozesha binti yake ambaye nywele zake zilianza kung'ooka. Mwanamke huyo wa Ki-Ansari alikuja kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumtajia kwamba: "Mumewe (mume wa mwanangu) ameona kwamba nimwachie avae nywele za bandia" Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Usifanye hivyo kwani Allah Huteremsha laana Yake kwa wanawake kama hao wanaoongeza nywele za bandia")) Al-Bukhariy 7:133 kutoka kwa Bibi 'Aisha (r.a.)
Kwa hiyo ieleweke kuwa mambo haya yakifanywa na wanaume uovu unakuwa mkubwa zaidi na ni madhambi makubwa.
ALLAH ANASEMA KUWA: WANAWAKE WOTE NI MASHETANI NA WACHAFU KAMA SEHEMU ZA SIRI!!!
Wanawake ni mashetani; wao ni kama uchafu wa sehemu za siri.
Sahih Muslim - 8.3240, 3242; Ghazali - gombo la 2, p. 26, gombo la 2, p. 43
Baada ya Allah na Mtume wake kumwaga sheria kali kwa Wanawake wa Kiislam, Allah na Mtume wake wamalizia kwa kusema haya hapa:
Wanawake ni wabaya zaidi ya watu walio kufa (Maiti), hawaruhusiwi hata kufuata jeneza
Sahih Muslim - 4.2039
HIVI MWANAMKE WA KIISLAM UNAFANYA NINI HUKO?
WEWE NI MBAYA KULIKO MAITI ASEMA ALLAH
Ndugu zanguni, huu ndio Uislam unao pigiwa debe kila siku, lakini umejaa chuki kubwa kubwa kwa Wanawake na Mama zetu. Swali ninalo kuuliza wewe Mwanamke wa Kiislam, ni ahadi gani Allah amekupa baada ya kifo?
Hebu endelea kusoma Ahadi kubwa kubwa kwa Wanaume wenu baada ya kifo:
Sura 78: 29. Na kila kitu tumekidhibiti kwa kukiandika. 30. Basi onjeni, wala hampati kwetu ila kuzidishiwa adhabu tu. 31. Hakika wenye kumcha Mola wao Mlezi watapata kuokoka na adhabu, na wataipata Pepo, 32. Na mabustani yenye matunda, na mizabibu mizuri, 33. Na wanawari walio watipwatipwa wa hirimu yao, 34. Na bilauri safi (Matiti)zilizo jaa pomoni, Ushahid zaidi soma (QURAN 37:40-4) : (QURAN 44:51-55) (QURAN 52: 17-20): (QURAN 55:54-59): (QURAN 55:70-77): (QURAN 56:37-40): (QURAN 78:31-34)
Allah anamwaga baraka kwa Wanaume wa Kiislam, lakini hakuna hata sehemu moja kwenye Quran ambayo Allah ametoa ahadi kwa Wanawake.
Wanawake wa Kiislam, karibuni katika Ukristo ambako hakuna ubaguzi wa Mungu katika jinsia kama ambavyo Allah anaonyesha katika Quran yake.
Mungu awabariki sana.
Katika Huduma yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW