Saturday, June 18, 2016

YESU NDIYE ATAKAYE HUKUMU WATU WOTE, WAFU NA WALIO HAI

Ndugu msomaji,
Kama ulikuwa haujui nani atahukumu walimwengu wote pamoja na imani na dini zote, basi fahamu kuwa Hakimu Mkuu ni Yesu Kristo.
Tuanze kwa kuthibitisha haya kwa kutumia aya za Biblia:
ZABURI 58:11 inasema kuwa: ‘Hakika yuko Mungu anayetawala katika dunia“. (UFUNUO 18;8 ) “Kwasababu hiyo, mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti na huzuni na njaanaye atateketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu“. Tena ndiye atakaye ihukumu Dunia yote “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana (YESU) hukumu yote“.
Neno la Mungu linatufundisha kuwa, atakaye toa hukumu ni Mwana ikimaanisha ni Yesu. Hivyo basi ni vyema umfuate Mwana ambaye atatoa hukumu na kuachana na miungu kama Allah wa Waislam.
Kumbe Muhammad na Waislam wote watahukumiwa na Yesu.
MATHAYO 25:31-32 inasema: “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu (YESU) katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake. Na mataifa yote yatakusanyika mbele zake, naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi”.
Yesu atayatoa Magugu "Waislam" na kuyatupa kwenye ziwa la moto. Ni vyema uanze kufuata mafundisho ya Yesu na kuachana na Allah aka Muhammad. Biblia inatuhakikishia kuwa Yesu ndie Hakimu Mkuu na sio Allah.
MATENDO 10:42 inasema: “Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudiaya kuwa huyu ndiye (Yesu) aliyeamriwa na Mungu awe mhukumu wa wahai na wafu” ( WARUMI 2:16 ) “Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu“.
Unaona sasa? Yesu ndie Hakimu Mkuu na sio Allah wa Waislamu. Muhammad na Waislamu wote watapiga goti mbele ya Yesu na kukiri kuwa Hakika Yesu ni Mungu.
2 TIMOTHEO 4:1 inasema “Nakuagiza mmbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakaye wahukumu waliohai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake’.
Kristo ndie atakaye hukumu waliohai na wafu kama Muhammad wa Waislam.
Ndugu nakushauri uchukue hatua na kumkubali Yesu hii leo. Yesu bado anakupenda na anataka kukuokoa kutoka dhambi.
Wasiliana nasi kama haufahamu nini cha kufanya ili uokoke.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW