Wednesday, July 1, 2015

Zul-Qarnain na Kutua kwa Jua katika Sura 18:85-86

Je, ni kweli kuwa jua linazama katika chemichemi za maji zenye tope au giza, au Koran ina makosa, au kuna maelezo mengine? Kwanza tutaangalia maana ya wazi Sura ya 18:85-86, na kisha tutaangalia maelezo na majibu ya baadhi ya Waislam kuhusu jambo hili.
Unajimu Kidogo
Inawezekana kuwa haijulikani kwa mapana kwamba watawala wa kislam wa Abbasid, Waarabu na Waajemi waliendelea sana katika unajimu, wakizipa majina nyota nyingi, hata walinukuru na kusahihisha baadhi ya orodha za hesabu za watawala wa Misri (Ptolemy’s tables). Hata hivyo jua ni kubwa mara nyingi zaidi ya dunia nzima, na dunia husafiri ikilizunguka jua. Jua halizami katika chemichemi za maji zenye tope.
Zul-Qarnain ni Nani?
Hatuna ushahidi kama Muhammad alimwambia mtu yeyote kuwa Zul-Qarnain alikuwa nani hasa. Waislam wana mitazamo minne tofauti.
  
Alexander Mkuu
 (wa Makedoni) ni mtazamo wa Waislam wengi zaidi. Zul-Qarnain humaanisha kuwa ni "mtu mwenye pembe mbili." Kuna hadithi ya kubuniwa isemayo kuwa Alexander Mkuu alikuwa mungu na alikuwa na pembe mbili za kondoo dume zilizokuwa zinakua pembeni mwa kichwa chake. Licha ya ukweli kwamba hii haikuwa kweli (na ni tatizo kupata kofia ya vita—helimeti inayoweza kutosha), hadithi hii ilijulikana, na waislam wengi hudhani kuwa Allah katika sura ya 18 Alexander alitajwa kwa jina hili, mungu.
  
Koreshi I Muajemi 
ni mtizamo mwingine. Ufalme wake hasa ulikuwa ufalme uliohusisha makundi mawili: Wamedi na Waajemi, lakini zaidi ya hayo hakuna uthibitisho kuwa pembe mbili zinamhusu yeye.
  
Mfalme wa Yemeni
 ambaye alivaa kofia ya vita yenye pembe mbili za kondoo dume, ni mtazamo walionao baadhi ya Waislam.
  
Mtu asiyejulikana 
ni mtizamo wa nne. Hata hivyo inaonekana si vema sana kutoa maelezo juu ya watu ambao msemaji hajawahi kuyasikia.
  
Hitimisho:
 Haijalishi kuwa Zul-Qarnain alikuwa nani hasa. Kama aligundua kuwa jua hutua kwenye chemichemi za maji zenye tope, na huwa halizami kwenye chemichemi za maji zenye tope, kwa hiyo huu ni ubatili, bila kujali mtu ambaye Muhammad alimzungumzia.
Sura 18 Mawazo na Majibu

Je Uislam Umejiboresha na kuwa Mzuri Kuliko Ukristo?


Je Muhammad anatimiza na kukamilisha lengo na huduma ya Kristo? Muhammad anajibu ‘ndiyo’ kwa msistizo.

Thiolojia ya msingi ya kiislam inafundisha kwamba kwa vile Allah alimtuma Gabriel akiwa na Kurani kwa Muhammad Mjumbe wa Allah, Muhammad na Kurani vinatimiza na kukamilisha lengo na huduma ya Kristo na Agano Jipya. Muhammad anaelekea kutambua umuhimu wa Biblia (Sura 4:47; 4:136; 4:163; 5:44-48; 5:82-83; 6:92, 154), lakini, ukristo na Agano Jipya vinatakiwa kujinyenyekeza kwa uislam na Kurani, ufunuo mpya na ulio bora zaidi.

Sura 5:15-16 inaeleza mtazamo wa Muhammad kwa kutumia mfano. Kwa muktadha wa upotofu wa Muhammad wa mafundisho ya kikristo ya Yesu kuwa Mwana (v. 17), na katika muktadha wa madai yake kuwa Wayahudi wamelaaniwa (v. 13), kifungu hiki kwenye Kurani (kikiwa kinaviwakilisha vingine) kinasema kwamba Wakristo (na Wayahudi) wamekuwa wakitembea gizani hadi wakati Muhammad alipokuja:

5:15 Watu wa Kitabu [Wayahudi na Wakristo] . . . mwanga umekuja kwenu sasa kutoka kwa Mungu, na Maandiko [Kurani] ikifafanua mambo, 16 ambayo kwayo Mungu huwaongoza wale wafuatao mambo yanayompendeza kwenye njia za amani, akiwatoa kutoka gizani na kuwaleta kwenye mwanga, kwa matakwa yake, na kuwaongoza kwenye njia iliyonyooka. (Haleem) (linganiasha na 4:157).

Mkristo wa leo mwenye ufahamu wa Biblia atatambua mara moja tamathali ya mwanga. Yesu anasema kuwa alitumwa toka mbinguni kama nuru ya ulimwengu, na Wakristo wamevuka kutoka giza kwenda nuruni (John 1:4-5, 8:12, 9:5, 12:46; 1 Petro 2:9). Lakini, sasa, Muhammad anadai kuwa Wakristo wamekuwa wakiishi kwenye giza, na amekuja kufafanua mambo kwao, kana kwamba mambo yalikuwa yamevurugwa. Kurani inatoa maongozi kwenye "njia iliyonyooka", mada ambayo imerudiwa mara kadhaa kwenye Maandiko ya kiislam (k.m. Sura 1) na "inafafanua mambo." Mstari wa 16 ni moja ya mistari ambayo Muislam anaweza kuufikiria wakati anapoonyesha kuwa uislam ni dini ya amani. Lakini je ni kweli?

Mkristo aliyejitoa, na mwenye ufahamu wa Biblia hawezi akaamini kwa vyovyote vile kuwa Uislam ni bora, tunawezaje kuuunja mvutano huu uliokwama? Je tuupuuzie? Kwa kuzingatia matokea ya karibuni kama mashambulizi ya kigaidi ya Marekani (Septemba 11, 9/11), jambo hili haliwezekani tena. Je tunajifanya kuamini kuwa dini zote ni sawa? Lakini jambo hili linatulazimisha kuyakana baadhi ya mafundisho ya msingi yasiyoweza kujadiliwa ambayo dini zote zinakuwa nazo na yale ambayo hayawezi kupatanishwa. Kwa jinsi hiyo basi, je tunabishania mafundhisho haya ya kuwazika tu?

Kujadili mambo ya kuwazika kama vile Umoja wa Utatu wa Mungu, kuna sehemu yake katika mazungumzo ya Waislam na Wakristo, lakini hakuna upande unaoweza kudai kuwa unaweza kuthibitishwa kwa uelekevu rahisi wa kutambua (simple observation). Kurani kila sehemu inatamka kwa dhati Umoja wa Mungu, wakati Agano Jipya linatamka kwa udhati kuwa Yesu ni Mungu na Roho Mtakatifu ni nafsi. Kwa hiyo tumepambanisha kifungu kitakatifu kimoja dhidi ya kingine, na ili kuuvunja mvutano huu usiokwisha ni lazima tutumie njia zingine. (Kwa habari zaidi za kuaminika kwa Agano Jipya, tembelea tovuti hii, site; kwa matatizo asilia ya Kurani, nenda hapa here.)

Kwa kuwa Muhammad anampinga Kristo na ukristo kuwa ni kweli, sisi Wakristo tunapaswa kumjibu. Je Yesu angesemaje? Kama ilivyotokea kuwa, Yesu ametupa mafundisho wazi kabisa ya namna ya kumtathmini nabii anayekuja baada yake katika historia, hasa kama huyo nabii anadai kuwa mkubwa kuliko Yesu: tathmini matunda yake.

Kwenye muktadha wa Hotuba ya Mlimani, Kristo aliongea kwa makutano, ama hakuna mtu kati yao aliyekuwa mwana thiolojia ama ni wachache tu, bali walikuwa wakulima wa hali ya chini. Kwenye Mathayo 7:15-20, Kristo anatumia lugha isiyokuwa na utata kuhusu namna ya kuutambua ukweli wa manabii:

Uislam na Fani ya Tiba

Uislam na Fani ya Tiba
Mchango katika Historia
 

Toleo la Juni 2006
Kwa kiasi kikubwa, fani ya tiba ya kisasa imetokana na fani ya tiba ya kimagharibi (Ulaya), ambayo ina asili ya fani ya tiba ya Ugiriki na Urumi kale. Ingawa jambo hili ni sahihi, limerahisishwa kupita kiasi; watu wengi zaidi, Waislam kwa wasio Waislam, hawafahamu kuwa fani ya tiba ya kimagharibi isingekuwa hapa ilipo sasa bila ya mchango mkubwa na muhimu sana wa fani ya tiba ya Kiislam. Yafuatayo ni maelezo kwa muhtasari ya baadhi ya michango, yakifuatiwa na mafundisho ya Koran na Hadithi kuhusu fani ya tiba.
Mwanzo wa Fani ya Tiba katika Uislam
Ingawa Waarabu kabla ya Muhammad walikuwa na ufahamu wa fani ya tiba ya kale, Wamisri, Wabizanti (Byzantines) na Waajemi walikuwa wameendelea sana. Walifanya upasuaji, walikuwa na dawa nyingi zilizotokana na mitishamba na mimea mingine, waliunganisha mifupa, walifahamu kuondoa maji machafu na takataka, na waliwatenga wenye ukoma. Hata hivyo, palikuwa na ushirikina mwingi na dawa mbaya za tiba pia.
 
Waislam wanakubaliana kwa ujumla kuwa Waabbasidi (Abbasids) hawakuwa waangalifu sana katika imani yao kama Waislam (mtawala mmoja alizama kwenye dimbwi la mvinyo), lakini kupitia kwao kuvumiliana, sayansi na fani ya tiba vilishamiri.
 
Madaktari wa kwanza kwenye ulimwengu wa Kiislam kwa kiasi kikubwa walikuwa ni Wakristo wa Kinestoria kama hawa wafuatao. Jurji bin Bakhtishu’ kutoka Iran ya magharibi (aliyekufa mwaka 830 B.K., 215 A.H.) na wanawe walikuwa madaktari chini ya khalifa al Mansur. Yuhanna ibn Masawayh (aliyekufa mwaka 243, 857) Mnestori Hunayn ibn Ishaq (miaka kama 800- 873 B.K. (260 A.H.)) aliteuliwa na al Ma’mun kuwa kiongozi wa Dar al Hikmah (Nyumba ya Hekima), na ndiye aliyetafsiri kazi nyingi za tiba ya fani na za sayansi kuwa Kiarabu. (Tazama http://www.masnet.org/history.asp?id=1033) na http://www.nlm.nih.gov/hmd/arabic/bioI.html
Kwa habari zaidi).

Hata hivyo, kufikia mwaka 931 B.K., madaktari 869 walikuwa katika mtihani wa hati ya Khalifa al Muqtadir mwaka 931 B.K.

Waganga na Wafamasia Muhimu Zaidi wa Kiislam

Uislam na Sayansi: Mitazamo Iliyosahauliwa Imekumbukwa

Uislam na Sayansi:
Mitazamo Iliyosahauliwa Imekumbukwa 

Toleo la Juni 2006
Je, maneno kama aljebra, alkali, pombe, astrolabe, naphtha, na zircon kitu gani kinachoyapatanisha hasa? Maneno haya yote ni ya Kiingereza yaliyotoholewa kutoka katika Kiarabu na maneno ya Kiajemi yanayoturudisha nyuma kwenye miaka ya 700-1150 BK, wakati kituo cha kujifunza Sayansi bila shaka kilikuwa Mashariki ya Kati.

Watu wengi yawezekana wasijue mchango muhimu uliotolewa kwa sayansi na hesabu kutoka Mashariki ya Kati. Ifuatayo ni orodha fupi ya mafanikio ya mambo haya, na kisha hutafiti kauli za kisayansi zilizomo katika Korani. Lakini kuna maendeleo mengi makubwa ya kitabibu ambayo hayajatajwa hapa; huleta sifa kwa mjadala wake wenyewe.
 
Sayansi ya Mashariki ya Kati ya Zamani
Hata Wasumeria wa kwanza (3500-2000 KK) walikuwa na mchanganuo wa wanyama wote waliowajua. (Wadudu wakubwa kama vile nzige walijumuishwa pamoja na ndege, kama viumbe warukao.) Wamisri wa zamani na Wababeli walitumia nyota ili kuwasaidia kujua ni wakati gani wangeanza kupanda. Watu hao wa zamani walikuwa na maendeleo kadhaa katika kutengeneza meli, ufugaji wa wanyama, na upasuaji, hata upasuaji wa kichwa. Wamisri walitumia dawa ya meno tangu mwaka 2500 KK. Mitatu kati ya michango muhimu sana ya kisayansi ni kuandika, kulima pamoja na sayansi na teknolojia ya vitu yabisi kama vyuma.
 
Pengine mafanikio ya juu zaidi kielimu ya ulimwengu wa zamani yalikuwa maktaba ya mji wa Alexandria. Hapa kulitunzwa mamia ya maelfu ya juzuu za nakala asilia au nakala za fasihi nyingi za ulimwengu wa watu wa wakati ule.
Uhandisi na Uhandisi Majengo wa Zama za Kale
Wamisri walikuwa na gubeti tangu 2500 KK. Katika uhandisi majengo, kila mtu anajua mapiramidi ya kuvutia nchini Misri na mahekalu (Ziggurats) ya Sumeria na Babeli.
 
Kitu kisichojulikana sana ni kuwa Kaskazini-mashariki mwa Iran kulikuwa na bwawa kubwa, lililoibuka hasa katika mwaka 1800 KK, kushinikiza wahamiaji wengi katika nchi za India na Iran. Bwawa nchini Yemen liliufanya ufalme wa Sheba kuwa kituo maalum cha kilimo na biashara hadi hapo lilipovunjwa pia zaidi ya karne moja kabla ya Muhammad. Ujenzi wa mifereji, bustani zinazoning’inia, na miji yenye kuta nene ni mambo ya kuvutia hata leo. Na kwa hakika, kama ungeliweka Mji wa Ashuru, Ninawi kati ya Ufaransa na Ujerumani wakati wa Vita Kuu ya Kwanza, pasingekuwa na upande wowote ambao ungeweza kuuteka. Hatimaye ulitekwa, lakini ni kwa sababu tu mto wa Khosr ulipofurika na mafuriko yake yalivunja sehemu ya ukuta wa mji huo..
Mashariki ya Kati ya Kale na Hesabu
Haya majengo ya kiuhandisi yasingeweza kujengwa kama pasingekuwa na msaada wa hesabu. Wababeli wa zamani walikuwa na mfumo wa kuhesabu hadi 60. Walipendelea namba zinazoshabihiana; kwa mfano, wangegawa a/b kama *l/b. Wababeli wa zamani walikuwa wa kwanza kutumia aljebra kwa hesabu za mistari na hesabu za mchanganyiko wa namba na herufi (quadradic problems). Chati iitwayo Plimpton 322 ni chati ya namba za Pythagorean (a^2 + b^ + c^2). Wababeli walibuni vipimo vya namba za mraba kama uchoravyo mstatili na kisha kuhesabu ukubwa wa eneo. Kimahesabu, watu hawa hawakutumia kitu chochote zaidi ya vipimo vya mraba (squares). Wakati huo huo Wababeli walikuwa na thamani tofauti ya pai (pi), na iliyokuwa sahihi zaidi ilikuwa 3.125. Mwanamahesabu wa Kiarabu wa karne ya 10 Abu’l-Wafa’ alisema watu waliotoa elimu ya kimahesabu walikuwa mafundi sanaa (wanasanaa) na wasanii.
 
Hesabu za maumbo ya pembetatu za Wamisri zilikuwa bora kuliko za Wababeli, kwa sababu Wamisri walikuwa na ufahamu juu ya kona, na walikuwa na ile thamani ya pai ya 31/7 au 3.16. Hii si mbali na 3.14159. Na hii imo katika nyaraka za Rhind Paparas—paparas (mwaka wa 1650 KK) na Paparas ya Moscow iliyokuwapo wakati ule ule. Majengo mengi ya Kimisri yalikuwa na pande za 3 kwa 4, lakini hawakujua juu ya nadharia ya Pythagoras (Pythagorean theorem). Sayansi na hesabu nyakati za zamani zilikuwa za "kivitendo". Pengine hii ndiyo sababu, kwa shauku tu, hapakuwa na yeyote aliyekuwa na wazo la "sifuri" hadi ilipogunduliwa nchini India.
Aljebra Zilitoka Wapi?
Hesabu ya aljebra ya kwanza tunayoifahamu ilikuwa imehifadhiwa katika Paparas ya Rhind iliyotolewa nakala na mwandishi wa Kimisri aliyeitwa Ahmes (mwaka wa 1650 KK.). Huu ni muda mrefu sana kabla Musa hajazaliwa. Wakati huo huo Wayunani walikuwa wakipendelea zaidi hesabu za maumbo, Wachina walikuwa wakikokotoa hesabu za mchanganyiko wa namba na herufi kabla Kristo hajazaliwa, na Wahindu (kwenye miaka ya 628-1150 BK) walikokotoa na kupata majibu ya maswali tata zaidi ya hesabu. Huko Baghdadi Muhammad ibn Musa al-Khowarizmi/Khawarizmi (mwaka wa 825 BK), Abu Kamil (mwaka wa 900 BK) na al-Karkhi (mwaka wa1100 BK) waliziendeleza hesabu za aljebra zaidi. Kwa kiasi kikubwa sana ziliziambukiza hesabu za Ulaya wakati Robert wa Chester alipotafsiri kitabu cha al-Khowarizmi kwenye mwaka wa 1140 BK kiliitwa kwa Kilatini Liber Algorism, maana yake kwa ujumla ni "Kitabu cha al-Kowarizmi." Na neno algorism baadaye lilikuwa algorithm and aljebra [kwa lugha ya kimahesabu].
 
Hapa chini jedwali laorodhesha baadhi ya wanasayansi wa Mashariki ya kati na wale wa Kiarabu pamoja na wanamahesabu.
 
Avicenna (Ibn-Sina) 979/980-1037 BKLicha ya kuwa tabibu muhimu sana kati ya enzi za Warumi na enzi ya leo, alikuwa mwanasayansi pia, mwanafalsafa, na mjenga hoja aliyeandika takriban kazi sanifu zipatazo 200. Albert Magnus wa England alijifunza mengi kutoka kwake
Averroes (Abu al-Walid Muhammad bin Ahmad ibn Muhammad ibn Roshd) 1126-1198 BKAlimsujudu [mwanafalsafa] Aristotle. Alisema mengi juu ya umaskini na masumbuko kutokana na jinsi Waislam walivyowachukulia
Avempace (Ibn Gabirol) 1021-1058 BKMwanafalsafa wa Kiyahudi na Kihispania aliyemwuunga mkono Aristotle
al-Karkhi miaka ya 1100 BKMichango mbalimbali katika kwa hesabu za Aljebra
Kemia/Alkemia na Fizikia
Makhalia wa Abbasid wa Baghdadi walikuwa na shulu ya Alkemia kwenye ya karne ya 9 au ya 10. Kazi za kwanza kabisa za Alkemia ya Kiarabu nusu ni za Kiarabu na nusu ni Kisiria. Khalid mwana wa Yezid (alikufa mwaka 708 BK) mwanafunzi wa mtawa wa Kisiria Marianus, alikuwa mwandishi wa kwanza wa Kiislam juu ya Alkemia, kufuatana na kitabu Kitab-al-Fihrist. Vipaji vya Wanaalkemia viliharibiwa kwa kujaribu kubadili madini ya "risasi" na vitu vingine kuwa dhahabu, lakini katika mchakato huo waligundua mambo mengi hii ni pamoja na Kemia pia. Wafuatao ni baadhi ya wanakemia maarufu wa Kiajemi na Kiarabu.
 
Geber (Jabir ibn-Hayyan) Kwenye miaka ya 760-815Mwanaalkemia wa Kiarabu aliyechuja chachu kitaalam na kutengeneza tindikali itokanayo na maji na naitrojeni. Alianza utafiti juu ya kubadili maumbo ya vitu yabisi (metals) na alivutiwa sana na kimiminika kiitwacho Zebadi (Mercury). Alikuwa mwenye sifa na maarufu kiasi kwamba kemia ikapewa jina la utani "Usanifu wa Jabir"
Ibn al Haytham Alikufa mwaka 1039 BH [Baada ya Hija]Alisomea mambo ya shinikizo, sumaku na sayansi ya mambo ya mwanga. Alisema kuwa huwa tunaona kwa kutumia mwanga unapoyaingia macho yetu, si miale ambayo jicho hutupa nje.
Quth al-Din 1236 BKAlielezea umbo la upinde wa mvua
Rhazes (Al-Razi) kwenye miaka ya 850-925Mkemia wa kiajemi (na mwana anga) aliyetengeneza chokaa ya kuta za nyumba ya Paris na alijifunza madini ya shaba na kristole (crystalline) yaani antimony
Abdul Salam of Pakistan. 1926-1996 BKAlishiriki tuzo ya Nobel ya mwaka 1979 katika Fizikia. Alikuwa Qadiani ambaye Waislamu wengi humchukulia kama wenye mafundisho potofu wasio waislamu
Geber (Jabir ibn-Hayyan) (alikufa mwaka 808 BK 193 BH [Baada ya Hija]) alikuwa Msufi mwenye imani ya kujikana mwenyewe kwa ajili ya mambo ya kiroho. Alikuwa na maabara huko Dameski. Vitabu vyake 200, vinane kati ya hivyo vilikuwa vya kemia, kujumlisha vitabu juu ya usindikaji, kutengeneza rangi, na uzito pamoja vipimo mbalimbali. Ama kwa hakika, wengine waiita kemia jina la utani "usanifu wa Jabir." Alitengeneza mezani iliyoweza kupima hadi uzito wa 1/6 ya gramu. Wakati watu wa Ulaya wa baadaye walidhani kuwa Phlogiston iliongezwa kwenye vitu vilipounguzwa, lakini Jabir alielewa kwa usahihi kwamba nguvu ya vitu vilivyoungua ilikuwa ikitoka, na kuacha mabaki ya majivu yasiyounguzika. Aligundua karatasi isiyounguzwa na moto, kizuia kutu, na kilichozuia maji kwenye nguo. Kwa uhalisia, alikuwa na wito wa karibu toka kwa watu japo alishauri kuwa maabara ya kikemia yalipaswa kuwa mbali na miji. 

Waislam Wauliza Wakristo

Swali la 1: Kwa nini mnaliamini Agano la Kale?
Jibu: Maandiko na elimukale (archaeology) vinaonyesha kuwa hakuna mabadiliko makubwa kwenye nakala za sasa kwa sababu angalau tano:
1. Mungu aliahidi kulinda neno lake katika Isaya 55:10-11; 59:21; 1 Petro 1:24-25, Mathayo 24:35. Hatima ya yote tunapaswa kuamini kuwa ama Mungu anaaminika au haaminiki. Lakini kama Muislam anaamini kuwa Mungu hakulinda neno lake katika Agano la Kale, na kwamba hakulinda neno lake katika Agano Jipya, ni kwa nini abadilishe na kulinda neno lake kwenye Kurani?
2. Yesu na Agano Jipya limethibitisha maandiko ya Agano la Kale katika Mathayo 19:4; 22:32,37; 39; 23:35; Marko 10:3-6; Luka 2:23-24; 4:4; 11:51; 20:37; 24:27,44
3. Ushahidi wa Elimukale: Kwenye Septuagint, Torati ilitafsiriwa kwenye Kiyunani/Kigiriki karibu mwaka 400 K.K. Hati toka Bahari ya Chumvi (Dead Sea Scrolls) yaliandikwa kuanzia karibu mwaka 100 K.K hadi baada ya Kristo, na tunaweza kuyalinganisha na Biblia zetu za leo. Tafsiri za Kiaremi (Aramaic Targums) zilitolewa karibu na muda Yesu alipokuwepo duniani. Maandiko toka Bahari ya Chumvi yana vipande karibu 95,000 kutoka kwenye nyaraka 867 zilizoandikwa kwa mkono za Agano la Kale na maandiko mengine. Karibu 1/3 ya nyaraka zilizoandikwa kwa mkono za Hati toka Bahari ya Chumvi ni nyaraka za Agano la Kale kwa mujibu wa NIV Study Bible uk.1432. Elimukale inaonyesha kuwa Biblia ambayo Yesu aliijua ilikuwa imehifadhiwa. Nahal Hever ni pango karibu na Engedi, ambalo lina kipande kilichoandikwa kati ya mwaka 50 K.K. na 50 B.K. cha Manabii Wadogo katika lugha ya Kiyunani. Huko Masada, kulikuwa na nakala ya kitabu cha Yoshua iliyoandikwa mwaka 169-93 K.K. Mafunjo ya Nash (Nash Papyrus), yaliyoandikwa mwaka 150 K.K., yana amri kumi. Hati ya wadi Muraba’at ya Manabii Wadogo iliandikwa karibu mwaka 132 B.K.
4. Waandishi wa kanisa la awali, kuanzia kama mwaka 97/98 B.K, walilitumia Agano la Kale mara nyingi sana. 

Angalia kwa orodha ya angalau waandishi 15 wakristo hadi mwaka 258 B.K waliotumia Agano la Kale.

5. Waandishi wa Kiyahudi, ingawa walikuwa maadui wa ukristo, walilihifadhi Agano la Kale lile lile lililomo kwenye Biblia za kiprotestant za leo. Kipekee, waandishi wa kiyahudi Philo na Josephus walitumia Agano la Kale mara nyingi sana.
Kwa muhtasari, Mungu ni Mwenye enzi, ajuaye yote, na asiye na uzembe wa aina yoyote ile. Tunaweza kuamini kuwa ameweka muelekeo sahihi kwa wote wanaotafuta kumfuata kokote anakowaongoza.

Swali la 2: Je tunaweza kuliamini Agano Jipya?
Jibu: Ndiyo, kuna sababu tano zinazofanana na zile zilizotangulia, kuanzia na tumaini kuwa Mungu hataruhusu watoto wake wadanganywe kabisa, hadi kwenye ushahidi mkubwa wa nyaraka zilizoandikwa kwa mkono.
1. Mungu ameahidi kulinda neno lake katika Isaya 55:10-11; 59:21; 1 Petro 1:24-25, Mathayo 24:35. Tunaweza kumwamini Mungu.
2. Nyaraka za zamani zaidi zilizoandikwa kwa mkono zilizolindwa ni pamoja na:
100 B.K. uk.6 (kipande cha Luka)
117-138 B.K. John Rylands (Yohana 18:31-33,37-38)
100-150 B.K. Chester Beatty II (uk.45)
125-175 B.K. - Bodmer II (uk.66)
125-175 B.K. uk.104 (kipande cha Mathayo)
Zaidi ya nyaraka 30 zilizoandikwa kwa mkono zilizoandikwa kabla ya mwaka 300 B.K.

A’isha: Mke wa Muhammad Mwenye Miaka Tisa

Watu wengi wamesema kuwa Muhammad alifanya tendo la ndoa na mke wake mwenye umri mdogo zaidi, A’isha, binti wa Abu Bakr, alipokuwa na miaka karibu 53 na [A’isha] alikuwa na miaka tisa. Baadhi ya Waislam wanakataa maneno haya. Kama mtu atadai kuwa Muhammad na A’isha walijamiiana wakati A’isha alipokuwa na umri wa miaka tisa, na walifanya makosa, jambo hili litakuwa ni kashfa kubwa sana kwa Muhammad. Kwa upande mwingine, kama ilikuwa kweli, jambo hili litaonyesha sura tofauti kabisa ya Muhammad itakayo washtua watu wengi. Kwa hiyo basi, madai haya dhidi ya Muhammad ni ya kweli au uongo? 
 
Andiko hili litaanza kwa kutoa ushahidi wa A’isha kuwa na miaka tisa wakati ndoa yake ilipokamilishwa kwa tendo la unyumba, kisha litatoa vipingamizi 11 dhidi ya jambo hili, na mwishoni, litauliza itakuwa vipi endapo kila wazo lilikuwa sahihi.
 
Jambo hili ni la muhimu kwa desturi iliyotumika sehemu nyingi sana lakini ambayo imepuuzwa sana siku za leo: mabibi arusi watoto kwenye nchi za Kiislam waliotokana na mfano wa Muhammad.
Huko Iran, hadi kufikia Juni 2002 iliruhusiwa kisheria kwa msichana wa miaka 9 kuolewa kwa ruhusa ya wazazi. Voices Behind the Veil (Sauti Ttokea Nyuma ya Mtando) uk.136-137.
Huko Ivory Coast kitabu hiki pia kinatuambia kuhusu msichana wa miaka 12 ambaye alikuwa anaondoka nyumbani asubuhi kwa masaa mengi kabla ya kurudi nyumbani. Baada ya baba yake kumfunga, alimuunguza kwa kipande cha chuma, alimfungia kwa muda wa siku tatu bila chakula, hatimaye almwoza kwa mwanaume wa miaka 40. Hakuwahi kumpeleka shule kwa sababu alisema kuwa jambo hilo litawaondoa kwenye desturi zao, (mabinti) wataanza kuuliza maswali, na kutokupenda kuolewa mpaka wafikishe umri wa maka 19 au 20. 
Wataliban
 walizishawishi familia zao kuoza mabinti wao wakiwa na umri mdogo hata miaka nane. Voices Behind the Veil uk.110.
Gazeti la Dallas Morning News 9/28/03 uk.1,10S lilikuwa na habari ya kusikitisha kuhusu tabu ya wasichana wa Kiislam wa Nigeria ambao waliolewa wakiwa na umri mdogo sana, walipata ujauzito na walipopata uchungu wa uzazi miili yao midogo ilikuwa bado haijawa tayari. Kwa kiasi kikubwa habari hii ilikuwa mbaya, kimsingi wengi wa wasichana hao walihitaji kuzaa kwa upasuaji (C-section) lakini hawakuweza kupata huduma hiyo. Wengi wao walinusurika, lakini hawakuweza kupata watoto tena kwa sababu ya kuharibiwa kwa miji ya mimba.
 
Ili kuelewa asili ya mamlaka ya mfano wa Muhammad, ni muhimu tufahamu jambo moja kuhusu Hadithi za Kiislam. Hadithi zina nafasi ya juu sana katika madhehebu ya Suni kuliko mapokeo yalivyo na nafasi kwenye makanisa ya Katoliki na Orthodox. Waislam wa madhehebu ya Suni wanaamini kuwa mikusanyiko sita ya Hadithi ndiyo yenye mamlaka kubwa zaidi kwenye Uislam baada ya Kurani. Sehemu iliyobaki ya andiko hili inaonyesha kuwa dai hili ni la kweli kabisa, kwa mujibu wa vyanzo vingi vya awali vya Kiislam vyenye kuunga mkono. Pamoja na nukuu hizi toka kwenye Hadithi sita zinazoaminika ni nukuu toka kwa wana historia wa zamani wa Kiislam wanaoheshimika sana ibn Ishaq na al-Tabari.
 
1. Sahih al-Bukhari 810-870 BK, 256 BH
1a. "Alisimulia baba wa Hisham: Khadija alkufa miaka mitatu kabla ya Nabii kuondoka Madina. Alikaa huko miaka miwili au zaidi kisha akamuoa ‘Aisha alipokuwa msichana mwenye umri wa miaka sita, na Muhammad aliikamilisha ndoa yao kwa tendo la unyumba wakati ‘Aisha alipokuwa na umri wa miaka tisa." Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 43 na.236, uk.153.
  

1b. Habari hizo zipo pia kwenye Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 43 na.234, uk.152.
  

1c. "Alisimulia ‘Urwa: Nabii aliandika (mkataba wa ndoa) na ‘Aisha wakati msichana alipokuwa na umri wa miaka sita na aliikamilisha ndoa yake nay eye kwa tendo la unyumba wakati akiwa na miaka tisa na ‘Aisha aliendelea kuwa naye kwa miaka tisa (yaani mpaka kifo cha Nabii). Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 62 sura ya 60 na.88, uk.65.
  

1d. Alisimulia ‘Aisha: Nabii alikuwa akinisitiri kwa Rida (vazi lenye kukinga sehemu ya juu ya mwili) yake nilipokuwa nawaangalia Waethiopia waliokuwa wanacheza kwenye ua wa nyuma wa msikiti. (Niliendelea kuangalia) hadi nilipotosheka. Hivyo unaweza kuelewa ni jinsi gani binti mdogo (ambaye hajafikia umri wa kuvunja ungo) ambaye ana hamu ya kufurahia burudani alivyofanyiwa mambo ya namna hii. Bukhari juzuu ya7 kitabu cha 62 sura ya 115 na.163, uk.119.
  

1e. "Alisimulia ‘Aisha: (mke wa Nabii) sikumbuki kama wazazi wangu waliamini dini yoyote ile isipokuwa dini ya kweli (yaani Uislam), na (sikumbuki) siku yoyote iliyopita bila sisi kutembelewa na Mtume wa Allah asubuhi na jioni." Bukharijuzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 4 na.245, uk.158. Kwa hiyo, ‘Aisha ama hakuwa mkubwa ama hakuwa amezaliwa kabisa wakati wazazi wake walipo badili dini na kuwa Waislam. Jambo hili linaendana na yeye kuwa mtoto wakati ndoa yake na Muhammad ilipokamilishwa kwa tendo la unyumba.
 
2. Sahih Muslim 817-875 BK, 261 BH
Mkusanyiko huu unachukuliwa kuwa wa pili wenye kuaminika zaidi miongoni mwa Hadithi.
  

UTATA NA SHAKA MBALI MBALI KATIKA HADITH ZA MUHAMMAD

Hadithi za Bukhari
Mamia ya maelfu ya hadithi (mapokeo) yanadai kuelezea mafundisho na matendo ya Muhammad na wafuasi wake wa karibu. Waislam wa kale walizichambua hadithi hizi ili kuona ni zipi kati yake ni za kweli. Kuna makundi sita ya hadithi zinazofikiriwa na Wasuni kuwa "sahihi" au halisi na zenye mamlaka ya kidini. Hadithi hizi huchukuliwa kuwa ni muhimu karibu sawa na Kurani yenyewe. Kundi refu zaidi ni Sahih al-Bukhari lenye juzuu tisa na hadithi 7,275. Mambo yafuatayo yana mvuto mkubwa kwa wasomaji wote Waislam na wasio Waislam toka kwenye hadithi za kundi la Bukhari. Dondoo hizi zimetolewa toka kwenye kitabu kiitwacho Tafsiri za Kiarabu na Kiingereza za Maana za Sahih Al-Bukhari kilichoandikwa na Dr. Muhammad Mushin Khan wa Chuo Kikuu cha Kiislam cha Medina Al-Munawwara, Saudi Arabia.

Muhammad Haabudiwi
"Baada ya hapo Abu Bakr alisema Tashah-hud (yaani hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammad ni Mtume wake)... Abu Bakr alisema, ‘Amma ba’du, yoyote miongoni mwenu aliyemwabudu Muhammad, basi Muhammad amekufa, lakini yoyote aliyemwabudu Mungu, Mungu yu hai na hatakufa kamwe. Mungu alisema: ‘Muhammad ni Mtume tu’" Bukhari juzuu ya 2 kitabu cha 23 (Kitabu cha Misiba) sura ya 3 na. 333 uk.188-189.
Hata hivyo Waislam wanamthamini sana Muhammad. "Kwa [msaada wa] Allah, Mtume wa Allah alipotema mate, mate yaliangukia kwenye mkono wa mmoja wa (yaani washiriki wa nabii) ambaye alifuta uso na ngozi vyake; alipowaamuru, washiriki wake walitimiza" maagizo yake mara moja; aliponawa walipigania kuchukua maji yaliyobakia; na walipoongea naye, walipunguza sauti zao na hawakumwangalia usoni mara kwa mara kwa ajili ya heshima." Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 50 (Masharti, ‘Conditions’) sura ya 13 na. 891 uk.564-565.

Marufuku Vinywaji Vikali
"‘Aisha [mke wa Muhammad] Nabii alisimulia akisema, ‘Vinywaji vyote vyenye kuleta ulevi ni Haram (vimezuiliwa) kunywa." Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 4 (Kitabu cha Kujitakasa) sura ya 75 na. 243 uk.153.
"Abu Huraira alisimulia: ‘Nabii alisema, ‘Mzinzi, wakati anafanya tendo la ndoa lisiloruhusiwa si muumini; na mtu yeyote, wakati anapokunywa kinywaji chenye kulevya, si muumini; na mwizi, wakati anapoiba si muumini" Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 69 (Kitabu cha Vinywaji) sura ya 1 na. 484 uk.339.

Waislam pia wamezuiliwa kuuza mvinyo, sanamu na nyama ya nguruwe. Muislam Sahih juzuu ya 3 kitabu cha 9 (Kitabu cha Biashara) sura ya 621-622 na.3835-3840 uk.828-830. Hawaruhusiwi kununua, kuuza au kubeba mvinyo. Ibn-i-Majah juzuu ya 4 kitabu cha 30 (Kitabu cha Vinywaji) namba 3380-3381 uk.493-494; juzuu ya 4 kitabu cha 30 na.3382 uk.494. Kuuza pombe kumezuliwa kwenye Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 8 (Kitabu cha Maombi) sura ya 73 na. 449 uk.267.

Je Muhammad Aliona Mwezi Ukigawanyika Vipande Viwili?
"Ombi la wapagani kwa Nabii kuwa awaonyeshe muujiza. Nabii aliwaonyesha kugawanyika kwa mwezi. ‘Abdullah bin Massud alisimulia: Wakati wa uhai wa Nabii mwezi uligawanyika vipande viwili na Nabii alisema, ‘Shuhudia (jambo hili).’" Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 (Wema na Uadilifu wa Nabii na Washiriki Wake) sura ya 26 na. 830 uk. 533.
"Anas alisimulia kuwa watu wa Maka walimwomba Mtume wa Mwenyezi Mungu awaonyeshe muujiza, na kwa ajili hiyo aliwaonyesha kugawanyika kwa mwezi." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 (Wema na Uadilifu wa Nabii na Washiriki Wake) sura ya 26 na. 831 uk.533.
"Ibn ‘Abbas alisimulia: Mwezi uligawanyika vipande viwili wakati wa uhai wa Nabii." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 (Wema na uadilifu wa Nabii na Washiriki Wake) sura ya 26 na. 832 uk.534.

Nyota Zinapaswa Kuyapiga Mashetani?
"Uumbaji wa nyota ulikuwa na malengo matatu, yaani kuwa mapambo ya mawingu, kupiga mashetani, na ishara za kuongozea wasafiri. Kwa hiyo, mtu yoyote anapojaribu kutafuta tafsiri tofauti, amekosea na anapoteza nguvu zake..." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 3 maelezo ya mwenye kutafsiri kabla ya na. 421 uk.282.

UISLAM UNADHARAU WAAFRIKA

Si MWEUSI wala MWAFRIKA
Na Abdullah Al Araby
Rangi ya ngozi ya mtu mara imekuwa kigezo cha dini. Wakereketwa wa uislam wamekuwa wakijaribu kuwashawishi Waamerika wenye asili ya Kiafrika kuwa uislam ni dini ya mtu mweusi, kwamba uislam ni dini ya kiafrika na kwamba Muhammad alikuwa mweusi. Hatuhitaji kusema kwamba Waislam wamekuwa wakitoa madai haya kwa watu weusi tu; lakini kwa wazungu hutumia njia tofauti!
Kwa kujua kuwa haya ni mawazo potofu yaliyofikiriwa kwa umakini mkubwa sana, yaliyokusudiwa kuwavuta watu weusi kwenda kwenye uislam, nimejisikia kuuweka ukweli wazi. Hakuna kitu chochote kwenye makala hii kinachoafikiana na mtazamo huu wa ubaguzi wa rangi. Kama tukiupokea au kuukataa uislam, basi iwe ni kwa sababu za sifa halisi za uislam wenyewe na si rangi ya ngozi ya mtu au chimbuko lake.
Chanzo change kikuu cha taarifa za makala hii, licha ya Koran, ni Maandiko matakatifu ya Waislam "Hadithi", ambazo ni matendo na maneno ya Mtume Muhammad wa uislam kama yalivyonukuriwa na "Sahih al Bukhary" na "Sahih "Muislam."

AFRIKA HAIKUWA CHIMBUKO LA UISLAM
Uislamu ulizaliwa katika karne ya 7, katika rasi ya Arabia, ambayo ilikuwa sehemu ya bara la Asia. Asia ya njano na Afrika nyeusi vimetengwa na bahari ya Shamu [Red Sea]. Hapa tunazungumzia mabara mawili tofauti na rangi mbili tofuati.
Uislamu ulikwenda Afrika muda si mrefu sana uliopita, na hii si dini inayotawala Afrika. Kuna uwezekano mkubwa kuwa Waamerika wenye asili ya Kiafrika walikuwa ama Wakristo ama waumini wa dini za jadi wakati walipoletwa Amerika.
Ukristo umekuwapo Afrika tangu nusu ya kwanza ya karne ya kwanza. Mtakatifu Marko, mwandishi wa Injili ya Marko, alikuwa Myahudi wa Afrika kaskazini aliyeihubiri Injili kule Misri. Kutokea kule, ukristo ulisambaa Afrika ya kaskazini yote, na kusini mwa mipaka ya Misri. Kanisa la mashariki liliwapa weusi wengi hadhi ya utakatifu [sainthood]. Kwa mfano Mtakatifu Musa mweusi, Mtakatifu Tekla Himanote, mwethiopia na wengineo. Mmojawapo wa walimu na manabii katika kanisa la kwanza alikuwa "Simoni Niger", na Ninger inamaanisha mtu mweusi kwa Kilatini (Matendo 13:1). Upande wa mashariki mwa Afrika ulifanywa kuwa wa kikristo kutokana na huduma ya mjumbe wa bunge la Malkia Kandake wa Ethiopia aliyebatizwa na mwinjisti Filipo (Matendo 8:6-40).

Unajimu na Kurani

 Baadhi ya Waislam wanasema Kurani ina ukweli wa kisayansi kuhusu mizunguko ya jua, mwezi, (na nyakati nyingine sayari). Ninapenda kuchunguza jambo hili, na tutazunguka pande tofauti tofauti kabla ya kufikia uamuzi. Lakini jambo la msingi ni kuwa: isipokuwa Muislam awe ameziona hizi aya kama misemo ya kufananisha, aya hizi hazitakubali, hazithibitishi usahihi wa kisayansi wa Kurani. 
 
Sura 36:37-40 inasema, "Na ishara yao ni usiku: Tulijitoa pale toka mchana, na tazama wakazamishwa kwenye giza; 38 na jua linafuata mkondo wake wa kawaida kwa muda liliopangiwa; hii ni amri yake (yeye), aliyeinuliwa kwenye nguvu, yeye ajuaye vyote. 39 Na mwezi-tumeupimia majumba makubwa (kupita toka upande mmoja hadi mwingine) hadi unabadilika kuwa kama sehemu ya chini ya kikonyo cha mtende kilichozeeka (na kunyauka). 40 Jua haliruhusiwi kuukuta mwezi na usiku hauwezi kwenda haraka hata kuupita mchana: Kila kimoja huelea tu kwenye mkondo wake wenyewe (kwa mujibu wa sheria)." (Tafsiri ya Yusuf Ali, toleo la kwanza) [Maneno yaliyo kwenye mabano yamo katika mabano kwenye tafsiri.]
 
Baadhi ya Waislam wanasema kuwa "jua hufuata njia yake kwa muda ambao limepangiwa" na neno "mkondo" likiwa limewekwa mwishoni. Hata hivyo, hatuwezi kusema vitu vingi sana kuhusu "mkondo" wa jua kwa sababu tafsiri ya Yusuf Ali ina rejeo (la 17) chini ya ukurasa linalohusiana na neno hili likisema "mzunguko, njia." Pia, toleo la Yusuf Ali lililofanyiwa marekebisho linasema "mahali pa kupumzika" badala ya "kipindi."
 
Ni kwa Jinsi Gani Baadhi ya Waislam Huitafsiri Kurani kwa Uhuru?
Tovuti ya Wasufi http://www.sufi.co.za/modern_science_and_islam.htm hupita kiwango ikisema
"Vitu hivi vyote dunia, mwezi na sayari zote na wakati wote hutembea kwenye mikondo (au mihimili) yake ni matufe yaeleayo" (Ansari)
Inaongeza maneno "(vyote hivi ni sayari)" na "(au mihimili yake)" kwenye mabano, kwa sababu hayamo kabisa kwenye Kiarabu. Hebu tuliache hili kwa kuwa ni tafsiri isiyo sahihi, na tujiulize "Sura 36:37-40 inafundisha nini hasa?" Inaweza kuwa moja ya vitu hivi vitatu:
  
Mikondo ya jua na mwezi:
 Kurani inafundisha kuwa jua na mwezi vilienda bila kupumzika kwenye njia/mikondo vikiizunguka dunia kwa kipindi maalum kilichopangwa.
  
Kuogelea kuelekea sehemu linaposimama:
 Jua huogelea kwenye mawingu wakati wa mchana, na huelekea sehemu linapopumzika usiku, na kurudi mahali pake lilipokuwa asubuhi iliyotangulia. Vivyo hivyo mwezi huogelea kwenye njia yake.
  
Misemo ya kufananisha:
 Kama sehemu iliyotangulia, ila hili limekusudiwa kama maelezo ya jinsi vitu vinavyoonekana kuwa, si jinsi vilivyo hasa. 

MABINTI WATATU WA ALLAH


Mabinti wa Allah


Mara nyingi Waislam wamekuwa wepesi kuwaambia watu wengine kuwa Mungu ameruhusu Biblia kupotoshwa. Kitu wanachodokeza ni kuwa Kurani leo hii ni neno la Mungu lenye kuaminika wakati ambapo Biblia sivyo. Biblia ina maandiko yanayotofautiana mengi yenye tofauti ndogo, lakini ushahidi wa mabadiliko ya mafundisho hauna uzito. Kurani ina ushahidi mkubwa zaidi wa kupotoshwa kwa mujibu wa Ubai, aya zilizobatilishwa‘Uthman, na matatizo mengine ya Kurani. Hata hivyo, tofauti kubwa zaidi ya mafundisho ya Kurani, iliyoletwa na Waislam wenyewe, ni "mabinti wa Allah."

Muhtasari

Tovuti ya Kikristo http://answering-islam.org/Responses/Saifullah/sverses.htm inasema, "Moja ya matukio yenye kuaibisha zaidi kwenye maisha ya Muhammad lilitokea wakati Shetani alipoweka maneno yake kwenye mdomo wa Muhammad. Muhammad alisema maneno ya Shetani kama neno la Mungu. Tukio hili limethibitishwa kwa maandishi na waandishi kadhaa wa Kiislam wa kale na limeongelewa kwenye Hadithi na Kurani. Waislam wa miaka iliyofuata, kwa kujisikia aibu kuwa nabii wao aliyejitangaza mwenyewe amesema maneno ya Shetani, walikana kuwa tukio hili lilitokea. Visingizio na kukana kwingi vimekuwa vikitolewa na hawa Waislam wa miaka iliyofuata ili kulifunika kosa lenye kuhusisha dhambi la Muhammad.
Ni muhimu ikafahamika tena kuwa tukio la ‘Aya za Shetani’ si jambo ambalo limetungwa na watu wasiokuwa Waislam. Tukio hili limerekodiwa na vyazo vya kale zaidi vya Kiislam vilivyokuwepo wakati wa uhai wa Muhammad. Mtu yoyote asifikiri kuwa jambo hili ni hadithi iliyotungwa na watu wenye kuupinga Uislam. Ni kisa kinachopatikana moja kwa moja kwenye rekodi za kale za Kiislam.
Hili moja ya masomo yenye kubishaniwa zaidi kwenye Uislam. Shetani alimsababishia Muhammad kunena maneno yake (Shetani) kama maneno ya Mungu."

Je Kurani Ilisema Nini Mwanzoni?

Sura ya Nyota (Sura 53) mistari ya 19-20 inasema, "Je umemwona Lat, na ‘Uzza, Na mwingine, (mungu mke) wa tata, Manat?"

Allah alikuwa maarufu huko Arabia kabla ya kuja kwa uislam, kama mungu aliyekuwa na mabinti watatu: al-Lat, al-Uzza, na Manat. (Kumbuka kuwa al- inamaanisha ‘yule’, kwa Kiingereza "the".)

Waandishi wanne wa mwanzo wa maisha ya Muhammad waliandika kuwa awali aya hizi zilifuatwa na:

"Hawa ni mawinchi (wasuluhishi) ambao maombi yao yanapaswa kutumainiwa"

Tafsiri: Mabinti wa Allah walifikiriwa kuwa viumbe wa mbinguni wenye kuomba kwa ajili ya wengine. Mawinchi marefu ya Kinumidia ilikuwa ni sitiari yao. Maneno mbadala ya "inatakiwa kutumainiwa" (turtaja) ni "imekubaliwa kwa kuthibitishwa" (turtada). (Kutoka kwenye tafsiri ya Alfred Guillaume ya The Life of Mohammed, iliyoandikwa na Ibn Ishaq, uk.166.

An Academic Critique of Internal Contradictions in the Quran with Reference to Eschatological Descriptions of Hell’s Sustenance

  Title: An Academic Critique of Internal Contradictions in the Quran with Reference to Eschatological Descriptions of Hell’s Sustenance Au...

TRENDING NOW