Sunday, December 4, 2016

KITABU CHA DANIEL (SEHEMU YA TISA)


Daniel Mlango wa 5:
Belshaza ambaye alirithi ufalme toka kwa mfalme Nebukadneza Baba yake hakujifunza juu ya Mungu wa Mbinguni licha ya kujua yote ambayo Mungu aliyafanya wakati wa utawala wa Baba yake. Siku Moja Mfalme Belshaza , aliwafanyia wakuu wake elfu karamu kubwa. Akiwa katika kilele cha ulevi na anasa, akaamuru wavilete vile vyombo vya dhahabu na fedha, ambavyo baba yake, Nebukadreza, alivitoa katika hekalu ililokuwako Yerusalemu; ili kwamba mfalme, na wakuu wake, na wake zake, na masuria wake, wapate kuvinywea.
Na kibaya Zaidi ya haya Mfalme Belshaza akiwa katika anasa zake hakumsifu Mungu wa Mbinguni wala kumtukuza, Bali wakaisifu miungu ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe. Saa iyo hiyo vikatokea vidole vya mkono wa mwanadamu, vikaandika katika chokaa ya ukuta wa nyumba ya enzi ya mfalme, mahali palipokikabili kinara maneno ambayo hakuna awezaye kuyasoma. Mfalme na wote waliokuweko katika ile sikukuu wakakiona kile kitanga cha Mkono kilichoandika.
Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana. Mfalme akaagiza waletwe wachawi, na wanajimu na wakaldayo na wenye hekima wa Babeli ili kwamba wapate kumsomea Maneno yaliyoandikwa Ukutani na kile kitanga cha mkono. Walakini wenye hekima wote wa Babeli hawakuweza kuyasoma naneno yake yote yaliyoandikwa. Walakini Malkia alimwendea Mfalme katika ile karamu kisha akamwambia kuwa asifadhaike kwani yupo Mtu aitwaye Danieli ambaye Roho ya Miungu watakatifu inakaa ndani yake na ambaye wakati wa Baba yake alimtafsiria Mfalme Nebukadneza ndoto zake zote alizoziota.
Mfalme akaagiza Kwamba Danieli aletwe ilia some naneno yale na kumjulisha mfalme tafsiri ya maneno yale kwa ahadi kwamba atapewa zawadi kubwa na kufanywa awe mtu wa tatu katika Ufalme. Danieli alivyoletwa mbele za Mfalme na kuyasoma yake maandishi aligundua maana yake. Nabii danieli akamkumbushia Mfalme kisa cha Baba yake jinsi alivvyojitukuza dhidi ya Mungu wa Mbinguni, na jinsi Mungu alivyokinyenyekeza kiburi chake.
Alimwambia Mfalme kwambaIngawa aliyafahamu hayo yote yaliyompata Baba yake, hakumtukuza Mungu wa Mbinguni bali aliagiza vyombo vya Mungu wa Mbinguni viletwe ili vitumiwe katika Ulevi na Anasa, na Zaidi ya hayo yote akaitukuza miungu ya miti na ya shaba na ya Mawe na kumsahau Mungu wa Mbinguni.
Ndipo Danieli akamsomea yale maneno yaliyoandikwa katika ule ukuta. Biblia yasema hivi;”- Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI. Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi. Ndipo Mfalme kwa Hofu alamvika danieli mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake na kumtangaza Daniel kama Mtu wa tatu katika Ufalme. Lakini Hukumu ya Mungu ilitekelezwa siku ileile. Wamedi na waajemi waliuvamia Ufalme wa Babeli usiku ule na mfalme akauawa na Wamedi wakaumiliki Ufalme.
SWALI:
Kwenye Daniel 5:1 na 30, Belshaza alikuwa ni nani? 

JINSI WACHAWI WANAVYOCHUKUA NYOTA YAKO


ASKOFU JOSEPHAT GWAJIMA


UTANGULIZI:

Huu ni mwendelezo wa somo la Nyota na Maisha mtu aliyonayo. Mathayo 2:1; Kama tulivyoona tangu mwanzo kuwa nyota ni kipawa, uweza, hatma au hali ya mtu ya baadaye. Tukaona nyota ya Yesu ilionekana kabla Yesu hajazaliwa na mamajusi wa mashariki walimwona kama Mfalme.


MAANA YA NYOTA:

Kama tulivyooa sehemu ya kwanza kuwa nyota ni kiashiria cha rohoni, kinachoonesha mtu atakuwa nani baadaye, mafanikio ya mtu au hatma ya mtu. Viashiria hivi ndivyo vinavyoitwa nyota.


NYOTA KATIKA BIBLIA:

Hesabu 24:14-17 Baraki alikuwa mfalme, na alipoona kuwa wanaisrael wanakuja ili kushambulia ufalme wake, akamtafuta Balaam amtabirie. Hayo ni maneno ya Balaamu aliyoona, Hivyo Balaamu alipoangalia taifa la Israel akaona nyota, kimsingi nyota ya mtu inaonyesha jinsi mtu atakavyokuwa baadaye. Hivyo balaamu aliweza kumuona Yesu tangu mwanzo na ndio maana mamajusi wa mashariki nao pia walimwona Yesu kama nyota.


Nyota yaweza kuonyesha kusudi la maisha ya mtu, na ndio maana ingawa Suleimani alizaliwa na mke wa Huria ambaye Daudi alimuua mumewe ili ampate lakini kwasababu nyota ya kujenga hekalu ilikuwa juu yake (yaani Suleimani), Mungu alimchagua kujenga Hekalu. Daudi alikuwa na watoto wengine wengi, lakini aliyechaguliwa kujenga ni Suleimani kwasababu ndio mwenye nyota ya kujenga yaani tangu anazaliwa


Isaya 47:8-12; Hapa biblia inataja neno “wajuao Falaki”, hii ni elimu inayohusu mambo ya nyota ambayo wachawi husoma. Katika Mathayo 2:1- Biblia inataja mamajusi, wao ni wasomaji wa nyota ambao waliiona nyota ya Yesu kabla ya Yesu hajazaliwa. Nyota ya Yesu iliwafanya mamajusi kumfuata kutoka mbali, na wakati huohuo Herode alifadhaika. Kumbe nyota ya mtu ikionekana watu wanaweza kuifuata na kukuletea unalohitaji. Watu wengi wapo katika vifungo mbalimbali kwasababu nyota zao zimefunikwa.

Saturday, December 3, 2016

Imam wa Msikiti wa Mayaha, Kisisi apokea Uponyaji kwa Jina la Yesu!



Mchungaji Michael Peter Imani wa WAPO Mission International Tawi la Mbagala Maji Matitu akiwa amemshikia kipaza sauti Mzee Musa Hombe (Idd Hussein Seba) (73) Imam wa Msikiti wa Mayaha, Kijiji cha Kisisi, Kata ya Ekhanoda Wilaya ya Singida Vijijini.

Aliyekuwa Imam wa Msikiti wa Mayaha, akishuhudia jinsi Yesu alivyomponya baada ya kuugua kwa miaka 15 “Sasa ninatafuta wa kuninunulia Biblia, Yesu anaponya mimi nimepona, ninyi waislamu wenzangu mnapoteza muda”

Pichani ni mtoto wa aliyekuwa Imam baada ya kupokea uponyaji na kumpokea Bwana Yesu

Christopher ambaye pia ni mtoto wa Juma Kombe, akifurahia kuuona Utukufu wa Mungu baada ya kuokoka, alikuwa amepagawa mapepo na biashara zake zikawa haziendi baada ya kuokoka kwa wiki tatu akaanza kuona mabadiliko ya biashara yake kushamiri kwa kasi.  “Nilipofanyiwa maombi ya wiki 3, nikakaa sawa, nikaingia darasani kusoma, nilipojazwa Roho Mtakatifu, usiku nimelala walikuja wachawi, wakaniita jina la zamani, Abdallah, lakini sauti ya upole ikaniambia, usiitike”.

Kijana Christopher ndiye aliyesababisha baba yake Kumpokea Bwana Yesu.

Friday, December 2, 2016

YESU NDIYE ATAKAYE HUKUMU WATU WOTE, WAFU NA WALIO HAI


KUMBE MUHAMMAD ATAHUKUMIWA NA YESU!
Ndugu msomaji,
Kama ulikuwa haujui nani atahukumu walimwengu wote pamoja na imani na dini zote, basi fahamu kuwa Hakimu Mkuu ni Yesu Kristo.
Tuanze kwa kuthibitisha haya kwa kutumia aya za Biblia:
ZABURI 58:11 inasema kuwa: ‘Hakika yuko Mungu anayetawala katika dunia“. (UFUNUO 18;8 ) “Kwasababu hiyo, mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti na huzuni na njaanaye atateketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu“. Tena ndiye atakaye ihukumu Dunia yote “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana (YESU) hukumu yote“.
Neno la Mungu linatufundisha kuwa, atakaye toa hukumu ni Mwana ikimaanisha ni Yesu. Hivyo basi ni vyema umfuate Mwana ambaye atatoa hukumu na kuachana na miungu kama Allah wa Waislam.
Kumbe Muhammad na Waislam wote watahukumiwa na Yesu.
MATHAYO 25:31-32 inasema: “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu (YESU) katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake. Na mataifa yote yatakusanyika mbele zake, naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi”.
Yesu atayatoa Magugu "Waislam" na kuyatupa kwenye ziwa la moto. Ni vyema uanze kufuata mafundisho ya Yesu na kuachana na Allah aka Muhammad. Biblia inatuhakikishia kuwa Yesu ndie Hakimu Mkuu na sio Allah.
MATENDO 10:42 inasema: “Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudiaya kuwa huyu ndiye (Yesu) aliyeamriwa na Mungu awe mhukumu wa wahai na wafu” ( WARUMI 2:16 ) “Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu“.
Unaona sasa? Yesu ndie Hakimu Mkuu na sio Allah wa Waislamu. Muhammad na Waislamu wote watapiga goti mbele ya Yesu na kukiri kuwa Hakika Yesu ni Mungu.
2 TIMOTHEO 4:1 inasema “Nakuagiza mmbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakaye wahukumu waliohai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake’.
Kristo ndie atakaye hukumu waliohai na wafu kama Muhammad wa Waislam.
Ndugu nakushauri uchukue hatua na kumkubali Yesu hii leo. Yesu bado anakupenda na anataka kukuokoa kutoka dhambi.
Wasiliana nasi kama haufahamu nini cha kufanya ili uokoke.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Nilipokuwa Nje ya Mwili Wangu Nilimwona Mungu, na Wafu Walio Hai!




Huu ni ushuhuda wa mtumishi wa Mungu, Dr. Roger Mills, ambaye anaishi North Carolina kule Marekani. Hii ni sehemu tu ya ushuhuda huo ambao ameuandika kwenye kitabu. Lakini nimeona niulete viyo hivyo katika ufupi wake, maana naamini kuwa kuna mambo ya muhimu mengi ya kujifunza katika sehemu hii kwa ajili ya uzima wetu wa milele katika Kristo Yesu.
Tafadhali karibu uendelee kupokea kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo kile ambacho alimfunulia mtumishi wake kwa ajili yangu na yako.
……………………………..
Jinsi Kitabu Hiki Kilivyo:
Mungu aliniambia niwaonye wacha Mungu na wasio wacha Mungu juu ya hatari ya giza la nje la kuzimu.
kwa wale wote watakaosoma kitabu hiki, ni shauku yangu kuelezea mambo ya kweli yaliyo kwenye kitabu hili kinachoitwa “Nilipokuwa Nje Ya Mwili Wangu, Nilimwona Mungu Na Wafu Walio Hai.”
[Maelezo ya blogger: wafu walio hai hapa anamaanisha watu waliokufa duniani lakini wako mbinguni, yaani watakatifu; au wako kuzimu]
Oktoba 5, 1998, Mungu Mwenyezi alinitokea katika umbo la mwanadamu na kuniambia, “Nimekuja kuzungumza na wewe kuhusiana na Giza la Nje la Kuzimu (Outer Darkness of Hell), na ninataka wewe nawe ukaongee na wengine juu ya Giza la Nje la Kuzimu.” Aliniambia kuwa angejidhihirisha kwangu. Mungu Mwenyezi aliniambia kuwa angeniruhusu kumwona kama ilivyokuwa kwa Petro, Yakobo na Yohana walivyomwona saa chache kabla ya kusulubiwa, na siku kadhaa baada ya kufufuka kwake. Nilipomwona, sikuanguka chini kama ambavyo baadhi ya wahubiri wanasema ningetakiwa kufanya. Na hata mitume walipomwona saa chache kabla ya kusulubiwa , au siku kadhaa baada ya kufufuka nao hawakufanya hivyo. Yesu aliwatokea mitume: (Mathayo 28:16-20; Marko 16:14-18; Luka 24:31; Yohana 20:19-23; Matendo 1:6-8).
Nilimwambia Mungu Mwenyezi, “Watu hawataniamini nitakapowaambia kuwa nimekuona.” Bwana akaniambia, “Watakuwapo watu, baadhi yao wakiwa wahubiri, ambao watapinga ujumbe huu. Baadhi wataamini na wengine hawataamini, lakini kwa wale ambao hawataamini, waambie kuwa nimesema kwamba imeandikwa kwenye Neno langu Takatifu ‘Nitajidhihirisha kwa wale wanaonipenda.’”
“Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake” (Yoh 14:21).

YESU NI MUNGU


Kama kawaida Waislam wanazidi kushikiria na kupinga kuwa Yesu ni Mungu! na Kinacho nishangaza wakipewa maandiko kuhusu u Mungu wa Yesu, wanachofanya ni kubadilisha maada!
Utasikiaaa "Oooh!!! Paulo sio Mtume wa Mungu. Mara ooooh Yesu hakufa!! Ooooh Wakristo mnakula Mashonde"na wanakuletea hoja nyingi ili kupoteza mada husika na Wakristo wanapowajibu kwa kutumia maandiko na kutaka kuendelea na maada husika wanabaki kuchanganyikiwa na kukimbia maada!
HUKO NI KUJIDANGANYA WENYEWE NDUGU ZANGU WAISLAM!!!! SISI Wakristo kazi yetu kuelimisha!! Maana Bwana Yesu alituagiza KUHUBIRI INJILI
"*************"
Marko 16:15-16(Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. ).
LAKINI HOJA YAO KUU NI IPI???
Leo mwislam mmoja alikuja inbox kwangu na hii hoja tena kwa ujasili wote akasema haya leta Biblia yako unijibu hoja hii
AYUBU 36 aya 26
Tazama, Mungu ni Mkuu Nasi hatumjui. Hesabu yake haitafutiki
Haya sasa umeona hapo Juu! Hesabu ya Miaka ya Mungu hakuna aijuaye..tangu kuwepo kwake Yesu miaka yake inaesabika!! Itakuwaje Yesu awe Mungu?
Ebu soma hii
Luka 3:23
Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusuph, wa Eli!
Haya kwa mujibu wa maandiko niliyokupa hapo juu niambie JE YESU ANASIFA YA MUNGU?
Mwislam akacheka kwa kebehi
hahaahaahaaaha ni jibu bhana! Usinikimbie.
Ukiangalia hoja kama ya huyo hapo ndugu!amejitahidi kuisema kwa ujasiri wote lakini amesahau kwamba nasisi tunaijua Biblia vizuri sana na inamajibu yote.
Kwa kuangalia hoja ya huyo ndugu hapo juu, na mjibu kama ifuatavyo:
Kamata Biblia yako twende sawa hapa!
Imeandikwa:
Wafilipi 2:5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Ukiangalia maandiko hapo juu, unaona Yesu alikuwa namna ya Mungu lakini kwa upendo wake mkuu aliamua kuja ulimwengu kutuokoa (Yohana3 aya 16)
Alijifanya kuwa hana utukufu akatwaa namna ya mtumwa akawa anamfano wa Mwanadamu.
Imeandikwa kwamba: Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshima; umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (Zaburi 8:4-6).
Mtunga Zaburi anasema mtu ni kitu gani paka umuangalie.
Hapo kuwa Yesu alitupenda paka akatoka kwenye kiti chake cha enzi ili aje kutuokoa toka dhambini.
Imeandikwa: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (Yohana 3:16).
JE WEWE USIYEMWAMINI YESU una uzima wa milele? (tafakari) Ukisoma Yohana 8:56 Yesu anawaambia Wayahudi. Ibrahim, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu: naye akaiona akafurahi 57 Basi Wayahudi wakamwambia, wewe hujapata bado miaka Hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia amin, Amin, nawaambia YEYE IBRAHIM ASIJAKUAKO,MIMI NIKO.
Yesu ni Mungu alikuwepo kabla ya kuumbwa kwa dunia. YEYE NI ALFA NA OMEGA.
Imeandikwa
Hapo mwanzo kulikuwako Neno naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu (Yohana1:1)
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu: nasi tukauona utukufu wake.utukufu kama wa mwana atokaye kwa Baba: Amejaa neema na kweli. (Yohana1:14)
Nadhani hadi hapo Waislam wanaanza kuelewa somo!!
Ilibidi Yesu Mungu Mkuu kufanyika mwili ili kufidia dhambi zetu mimi na wewe! (Warumi5:8)
Imeandikwa
Yeye asiyejua dhambi alimfanya dhambi kwa ajili yetu ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika yeye.
Kuna baadhi ya Waislam wanasema "kwahiyo nyinyi Wakristo mna Mungu watatu"
Jibu ni kwamba! Mungu wetu ni mmoja tu!
Mungu Baba
Mungu Mwana
Mungu Roho Mtakatifu
=Mungu mmoja!!
Ila amegawanyika katika Utatu. (Kumb 6;4)
Maana ya Nafsi Tatu angalia mwenyewe
Mwanzo1:1, 1:26, 3:22
Isaya 6:8
Mathayo 3:16-17
Soma Yohana 10:30
Imeandikwa
1Timotheo2:5
Kwasababu Mungu ni mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja mwanadamu kristo Yesu 6 ambaye alijitoa mwenyewe kwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.
Ukiangalia kwenye andiko hilo unaona kazi ya kila nafsi!
Mungu Baba katika uumbaji
Mungu Mwana katika ukombozi
Mungu Roho Mtakatifu katika ualimu!
Majukumu
Baba-Mwana-Roho Mtakatifu!!
Wakorintho 8:6
Lakini kwetu sisi Mungu ni Mmoja tu aliye Baba ambaye vitu vyote vimetoka kwake: Yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo ambaye kwake vitu vyote vimekuwako na sisi kwa yeye huyo!
Ukiangalia andiko hilo utagundua Yesu ana sifa zote za ki Mungu!
-Yeye ni muumbaji
-Mkombozi
1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu.
MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, akaonekana na Malaika, akahubiriwa katika mataifa,
Akaaminiwa katika ulimwengu, akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii:
Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yeremia 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
HITIMISHO
Yohana 8:31 Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini. NINYI MKIKAA KATIKA NENO LANGU Mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli 32 tena mtaifahamu kweli nayo hiyo ITAWAWEKA HURU.
Ndugu zangu Waislam njooni kwa Yesu mpate kujua kweli na hiyo kweli itawaweka huru!
-itawaweka huru na dhambi
-itawaweka huru na vifungo vya Shetani
Ndugu yangu kwanini un'gan'gani kubaki kwenye vifungo vya Shetani wakati Yesu anakuita kwa sauti ya upole!!
Mimi ndimi njia ya kweli na uzima HAKUNA AJAYE KWA BABA ILA KUPITIA MIMI (Yohana 14:6)
Sasa basi unategemea kwenda mbingu ipi kama unamkataa Yesu?
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua
IJUE KWELI NAYO ITAKUWEKA HURU!!
YESU NI MUNGU.

WATU ZAIDI YA MILIONI MOJA NCHINI INDIA WAMEMPOKEA YESU NA KUWA WAKRISTO.


Mkutano mkubwa wa Injili ya Bwana wetu Yesu Kristo uliofanyika India umethibitisha kuwa YESU NI YULE YULE JANA LEO NA HATA MILELE.
Bill Wills ambaye ni mmoja ya watu ambao wapo kwenye kampeni ya kuitangza Injili ya Yesu Kristo amesema kuwa, Yesu anaokoa kwa njia ya ajabu sana. Alisema, baadhi ya vijiji VIZIMA VIMEMPOKEA YESU KWA MPIGO.
HII NI HABARI NJEMA KWA MATAIFA YOTE. YESU NI YULE YULE JANA LEO NA HATA MILELE.
Isoma habari kamili hapa:

ALLAH HANA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA


KWANINI JINA LA ALLAH HALINA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA?
KWANINI HAKUNA NGUVU YA UPONYAJI KATIKA UISLAM?
MBONA KATIKA UKRISTO WATU WANAPONA KWA JINA LA YESU?
ALLAH ASHINDWA KUMPONYA MUHAMMAD
MAOMBI YA JIBRIL YAGONGA MWAMBA
LAKINI JINA LA YESU LINAPONYA MAGONJWA YOTE
JE, UMESHA WAI ONA KUNA MKUTANO WA UPONYAJI KATIKA UISLAM?
Ndugu msomaji,
Uponyaji ni nini?
Ni tendo la kiimani la kupokea uzima katika roho au mwili kwa njia ya kuombewa,kuwekewa mikono au kulisikia neno sahihi la Kristo Yesu. Tendo hili la kiimani humletea mwamini uzima wa kiroho na afya ya kimwili pale ilipopunguka,kumbuka~wengi walipoponywa udhaifu wa miili yao,waliponywa pia na roho zao.
Hivyobasi, kwanini Allah alipo mtuma Jibril kwenda kumuombea uponyaji Mtume wake Muhammad kwa ugonjwa uliosababishwa na kula sumu, maombi yao hayakufanya kazi?
Hivyo basi, uponyaji haufanywi na mtu awaye yoyote yule isipokuwa Mungu. Hata madaktari bingwa wao hawaponyi bali hutoa tiba tu, mwenye kuponya ni Mungu. Watumishi wa Mungu pekee ndio hufanyika kama daraja au chombo cha kuleta uponyaji ulioachiliwa na Bwana kwa muhusika mwenye kuhitaji.
HEBU SASA TUMSOME ALLAH NA JIBRIL KATIKA JARIBIO LAO LA KUMPONYA MUHAMMAD:
Ibn Sa'd Ukurasa wa 265
Aisha, Mke wa Mtume Muhammad alikuwa akisema, "Wakati Nabii wa Allah alipo kuwa anaumwa, Jibril alikuwa anamwombea Muhammad kwa Allah kwa kusema haya "Katika Jina la Allah ambalo litakuponya kutoka kila magonjwa na maumivu na kutoka kila wenye ubaya nawe na kila wanakuombea ubaya, utapona..
Je, jina la Allah liliweza kumponya Muhammad? Hebu tusome Sahih hadith kama ilivyo letwa na Al Bukhari:
MAJIBU YA MUHAMMAD BAADA YA KUOMBEWA UPONYAJI NA ALLAH/JIBRIL:
Bukhari's Hadith 5.713:
Imesemwa na 'Aisha:
Mtume Muhammad wakati alipo kuwa anaumwa na kuchukuliwa na kifo alikuwa akisema, O Aisha, bado nasikia maumivu makali sana kutokana na chakula nilicho kula kilicho kuwa na Sumu kule Khaibar, na wakati huu nasikia kama nyongo yangu inakatwa kutokana na ile Sumu niliyo kula.
Hivi Mungu anaweza kuomba na ashindwe? Mbona Allah na Jibril maombi yao ya uponyaji kwa Muhammad hayakufanya kazi?
SASA TUMSOME YESU WA KWENYE BIBLIA, JE ALIWEZA KUPONYA WATU?

MUHAMMAD ANAAPA KWA YESU MUNGU WAKE


Soma Sahih hadith kutoka Al Bukhar:
Muhammad aseme haya katika (Bukhari hadithi na 425, juzuu 3) hadithi ya Abu Huraira amesema mtume wa Allah s.a.w):
Amesema Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko ipo mkononi mwake karibu atateremka kati yenu Mwana wa Mariam atahukumu kwa uadilifu.
Kama Muhammad anaapa kwa Yesu na kukiri kuwa Yesu ndio atakaye hukumu, kwanini nimfuate Allah ambaye sio Yehova?
Kwanini Muhammad hakua-apa kwa Allah?
SASA KAMA KUAPA LAZIMA KUWE KWA MWENYEZI MUNGU, KWANINI MUHAMMAD ALIAPA KWA YESU?
KUMBE YESU NI MWENYEZI MUNGU.
katika Hadithi iliyopokelewe na Abdallah bin `Umar R.A.A. na iliyotolewa na L-Bukhari, “
"إِنَّ اللَّهَ يَنْهَاكُمْ أَنْ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ ، فَمَنْ كَانَ حَالِفًا فَلْيَحْلِفْ بِاللَّهِ أو فَلْيَصْمُتْ"
Maana yake, “Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kuapa kwa baba zenu, atakaeapa aape kwa Mwenyezi Mungu au anyamaze
SASA MSOME NABII MUHAMAMD ANAPAAPA KWA YESU:
(Bukhari hadithi na 425, juzuu 3) hadithi ya Abu Huraira amesema mtume wa Allah s.a.w):
Amesema naapa kwa ambaye nafsi yangu iko ipo mkononi mwake karibu atateremka kati yenu Mwana wa Mariam atahukumu kwa uadilifu.
KUMBE MUHAMMAD ANAJUA KUWA YESU NI MWENYEZI MUNGU.
Shalom,
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo.

UNAKIFAHAMU KITI CHA HUKUMU CHA KRISTO?


Ndugu msomaji, kwanza kabisa ningependa tujifunze maana ya maneno haya machache.
Nini maana ya Hukumu?
Hukumu ni uamuzi wa mwisho kabisa unaotolewa na mahakama juu ya suala linalobishaniwa baina ya mlalamikaji na mlalamikiwa. Uamuzi huo ndio unaotoa kauli ya mwisho na kutamka ni nani
mwenye haki katika suala linalobishaniwa na ni nini wajibu wa yule aliyekosa ushindi.
Hakimu atakayekikalia kiti hiki ni Yesu Kristo . Yeyote leo anayemkana Yesu Kristo kuwa siyo mwana wa Mungu , atafahamu hapa kwamba hukumu yote iko chini yake ( Yohana 5:22 ; Matendo 10:38-41; 17:31; Warumi 2:16; 2Timotheo 4:1 ). Ni heri kufahamu mapema hivi leo kwamba Yesu ndiye hakimu na kuomba msamaha kwake, yeye yuko tayari kulehemu na kusamehe kabisa ( Isaya 55:6-7 ). Yesu atakapokikalia kiti cha enzi kikubwa cheupe atakuwa mwenye hasira, huruma itakuwa mbali naye kabisa ( Ezekieli 7:4; 8:18; Warumi 2:4-5 ).
Warumi 14:10-12 yasema, “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.” Wakorintho wa Pili 5:10 yatuambia, “Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya.” Kwa muktadha huu, ni wazi kuwa maandiko yote yanahusu Wakristo, sio wasio Wakristo. Kiti cha hukumu cha Kristo, kwa hivyo kinahuzisha Wakristo kutoa hesabu ya maisha yao kwa Kristo. Kiti cha hukumu cha Kristo hakitambui wokovu; hiyo ilithibitishwa na kusulubiwa kwa Yesu kwa niaba yetu (1Yohana 2:2) na imani yetu kwake (Yohana 3:16). Dhambi zetu zote zimesamehewa na hatutahukumiwa kwa sababu yao (Warumi 8:1). Hatustahili kuangalia katika kiti cha hukumu cha Kristo kuwa ni Mungu anazihukumu dhambi zetu, bali kuwa ni Mungu anatuzawadi kwa maisha yetu. Naam, vile Bibilia inasema, tutatoa hesabu sisi wenyewe. Sehemu ya hii ni kwa kweli ni kuzijibu baadhi ya dhambi zetu ambazo tulizitenda. Ingawa, hiyo haitakuwa jambo la kimsingi kuangazia kiti cha hukumu cha Kristo.
Katika kiti cha hukumu cha kristo, Wakristo watalipwa kulingana na vile walimtumikia Kristo kwa uaminifu (1 Wakorintho 9:4-27; 2 Timotheo 2:5). Baadhi ya vitu vingine tunaweza hukumiwa ni vile tulivyo tii jukumu kuu la kuihubiri injili (Mathayo 28:18-20), vile tulikuwa washindi kwa dhambi (Warumi 6:1-6), na vile tulizuia ndimi zetu (Yakobo 3:1-9). Bibilia inazungumzia Wakristo kupokea taji kwa mambo tofauti kulingana na vile walimtumikia Kristo kwa uaminifu (1 Wakorintho 9:4-27; 2 Timotheo 2:5). Taji tofauti zimeelezewa katika 2 Timotheo 2:5, 2 Timotheo 4:8, Yakobo 1:12, 1 Petero 5:4 na Ufunuo 2:10. Yakobo 1:12 ni muhtasari mzuri wa vile tunastahili kufikiria juu ya kiti cha hukumu cha Kristo: “Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.”
Watu watajitetea kwa kilio hapo na kusema “mimi nilifanya miujiza kwa jina lako”, “mimi nilitoa pepo kwa jina lako”, mimi nilishuhudia na kufuatilia n.k, na Yesu atasema sikuwajua ninyi; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu (Mathayo 7:22-23).
Kila mtu atatolewa hapo na kukamatwa kwa nguvu kisha atatupwa kwenye ZIWA LA MOTO. Ziwa la moto ni tofauti na kuzimu au Jehanum. Ziwa la moto kwa sasa halina mtu ndani yake. Wa kwanza kutupwa humo watakuwa Mnyama au mpinga Kristo na nabiii wa uongo (Ufunuo 19:20). Kisha atafuata Shetani (Ufunuo 20:10). Mateso ya ziwa la moto ni mazito zaidi kuliko Jehanum. Mauti au kifo ni Jehenum ya sasa, vyote pia vitatupwa katika ziwa la moto pamoja na wenye dhambi wote (Ufunuo 20:14-15, 21:8). Hapo itakuwa “kwaheri ya kutokuonana tena” kwa wenye dhambi na watakatifu.
Je, unataka kwenda kwenye ZIWA LA MOTO AU KWENDA MBINGUNI? Uchaguzi ni wako, ingawa mimi nakushauri umpokee Yesu Kristo, HAKIMU MKUU, ili upate uzima wa milele.
Shalom
Max Shimba Ministries

An Academic Critique of Internal Contradictions in the Quran with Reference to Eschatological Descriptions of Hell’s Sustenance

  Title: An Academic Critique of Internal Contradictions in the Quran with Reference to Eschatological Descriptions of Hell’s Sustenance Au...

TRENDING NOW