
Daniel Mlango wa 5:
Belshaza ambaye alirithi ufalme toka kwa mfalme Nebukadneza Baba yake hakujifunza juu ya Mungu wa Mbinguni licha ya kujua yote ambayo Mungu aliyafanya wakati wa utawala wa Baba yake. Siku Moja Mfalme Belshaza , aliwafanyia wakuu wake elfu karamu kubwa. Akiwa katika kilele cha ulevi na anasa, akaamuru wavilete vile vyombo vya dhahabu na fedha, ambavyo baba yake, Nebukadreza, alivitoa katika hekalu ililokuwako Yerusalemu; ili kwamba mfalme, na wakuu wake, na wake zake, na masuria wake, wapate kuvinywea.
Na kibaya Zaidi ya haya Mfalme Belshaza akiwa katika anasa zake hakumsifu Mungu wa Mbinguni wala kumtukuza, Bali wakaisifu miungu ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe. Saa iyo hiyo vikatokea vidole vya mkono wa mwanadamu, vikaandika katika chokaa ya ukuta wa nyumba ya enzi ya mfalme, mahali palipokikabili kinara maneno ambayo hakuna awezaye kuyasoma. Mfalme na wote waliokuweko katika ile sikukuu wakakiona kile kitanga cha Mkono kilichoandika.
Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana. Mfalme akaagiza waletwe wachawi, na wanajimu na wakaldayo na wenye hekima wa Babeli ili kwamba wapate kumsomea Maneno yaliyoandikwa Ukutani na kile kitanga cha mkono. Walakini wenye hekima wote wa Babeli hawakuweza kuyasoma naneno yake yote yaliyoandikwa. Walakini Malkia alimwendea Mfalme katika ile karamu kisha akamwambia kuwa asifadhaike kwani yupo Mtu aitwaye Danieli ambaye Roho ya Miungu watakatifu inakaa ndani yake na ambaye wakati wa Baba yake alimtafsiria Mfalme Nebukadneza ndoto zake zote alizoziota.
Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana. Mfalme akaagiza waletwe wachawi, na wanajimu na wakaldayo na wenye hekima wa Babeli ili kwamba wapate kumsomea Maneno yaliyoandikwa Ukutani na kile kitanga cha mkono. Walakini wenye hekima wote wa Babeli hawakuweza kuyasoma naneno yake yote yaliyoandikwa. Walakini Malkia alimwendea Mfalme katika ile karamu kisha akamwambia kuwa asifadhaike kwani yupo Mtu aitwaye Danieli ambaye Roho ya Miungu watakatifu inakaa ndani yake na ambaye wakati wa Baba yake alimtafsiria Mfalme Nebukadneza ndoto zake zote alizoziota.
Mfalme akaagiza Kwamba Danieli aletwe ilia some naneno yale na kumjulisha mfalme tafsiri ya maneno yale kwa ahadi kwamba atapewa zawadi kubwa na kufanywa awe mtu wa tatu katika Ufalme. Danieli alivyoletwa mbele za Mfalme na kuyasoma yake maandishi aligundua maana yake. Nabii danieli akamkumbushia Mfalme kisa cha Baba yake jinsi alivvyojitukuza dhidi ya Mungu wa Mbinguni, na jinsi Mungu alivyokinyenyekeza kiburi chake.
Alimwambia Mfalme kwambaIngawa aliyafahamu hayo yote yaliyompata Baba yake, hakumtukuza Mungu wa Mbinguni bali aliagiza vyombo vya Mungu wa Mbinguni viletwe ili vitumiwe katika Ulevi na Anasa, na Zaidi ya hayo yote akaitukuza miungu ya miti na ya shaba na ya Mawe na kumsahau Mungu wa Mbinguni.
Ndipo Danieli akamsomea yale maneno yaliyoandikwa katika ule ukuta. Biblia yasema hivi;”- Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI. Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi. Ndipo Mfalme kwa Hofu alamvika danieli mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake na kumtangaza Daniel kama Mtu wa tatu katika Ufalme. Lakini Hukumu ya Mungu ilitekelezwa siku ileile. Wamedi na waajemi waliuvamia Ufalme wa Babeli usiku ule na mfalme akauawa na Wamedi wakaumiliki Ufalme.
Ndipo Danieli akamsomea yale maneno yaliyoandikwa katika ule ukuta. Biblia yasema hivi;”- Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI. Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi. Ndipo Mfalme kwa Hofu alamvika danieli mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake na kumtangaza Daniel kama Mtu wa tatu katika Ufalme. Lakini Hukumu ya Mungu ilitekelezwa siku ileile. Wamedi na waajemi waliuvamia Ufalme wa Babeli usiku ule na mfalme akauawa na Wamedi wakaumiliki Ufalme.
SWALI:
Kwenye Daniel 5:1 na 30, Belshaza alikuwa ni nani?
Kwenye Daniel 5:1 na 30, Belshaza alikuwa ni nani?