Saturday, August 22, 2015

YESU NI UPENDO (SEHEMU YA PILI)

Huruma ni sehemu nyingine ya upendo wa Yesu.

Huruma ni nini? Katika Biblia, huruma na rehema zinahusiana sana. Maneno kadhaa ya Kiebrania na Kigiriki yanadokeza sifa ya huruma yenye upendo. Kwa mfano, mara nyingi kitenzi cha Kiebrania ra·chamʹ hutafsiriwa “onyesha rehema” au “sikitikia.” Neno hilo la Kiebrania, ambalo Yesu anatumia kujihusu, linahusiana na neno linalomaanisha “tumbo la uzazi” linaloweza kufasiriwa kuwa “huruma ya mama.”

Biblia inatumia hisia ambazo mama huwa nazo kwa mtoto wake mchanga kutufundisha kuhusu huruma ya Yesu. Andiko la Isaya 49:15 linasema: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie [ra·chamʹ] mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” Ni vigumu kuwazia kwamba mama anaweza kusahau kumnyonyesha na kumtunza mtoto wake mchanga. Kwa kweli, mtoto mchanga ni dhaifu; anahitaji kupendwa na kutunzwa na mama yake usiku na mchana. Ingawa hivyo, inasikitisha kupata habari kuhusu akina mama wanaowatupa watoto wao, hasa katika ‘nyakati hizi za hatari.’ (2 Timotheo 3:1, 3) “Lakini mimi sitakusahau wewe,” atangaza Mungu. Huruma nyororo ya Yesu ni yenye nguvu zaidi ya hisia yenye nguvu tunayoweza kuwazia, yaani, huruma ambayo kwa kawaida mama humwonyesha mtoto wake mchanga.

Waisraeli walipatwa na nini katika nchi ya Misri ya kale, naye Mungu aliitikiaje kilio chao?
Mungu huonyeshaje sifa ya huruma akiwa kama mzazi mwenye upendo? Sifa hiyo ya huruma inaonekana wazi kutokana na jinsi alivyolitendea taifa la Israeli la kale. Kufikia mwisho wa karne ya 16 K.W.K., mamilioni ya Waisraeli waliteswa sana walipokuwa watumwa huko Misri. (Kutoka 1:11, 14) Waisraeli walimlilia Mungu awasaidie walipokuwa wakiteseka. Je, Mungu mwenye huruma nyororo aliitikiaje?

Mungu aliwahurumia. Akasema: “Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao . . . maana nayajua maumivu yao.” (Kutoka 3:7) Mungu hangeweza kuwatazama watu wake wakiteseka au kusikia vilio vyao na asiwahurumie. Yehova ni Mungu mwenye hisia-mwenzi. Nayo hisia-mwenzi, yaani, sifa ya kuguswa moyo na uchungu wa wengine, inahusiana sana na huruma. Lakini Mungu hakuwahurumia tu watu wake; alichochewa kuwasaidia. Andiko la Isaya 63:9 linasema: “Kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe.” Mungu wa Israel aliwaokoa Waisraeli kutoka Misri kwa “mkono hodari.” (Kumbukumbu la Torati 4:34) Baadaye, aliwalisha kimuujiza na kuwapa nchi yenye rutuba.

(a) Maneno ya mtunga-zaburi yanatuhakikishiaje kwamba Mungu anamjali sana kila mmoja wetu? 
(b) Mungu hutusaidia katika njia gani mbalimbali?
Mungu hawahurumii watumishi wake tu wakiwa kikundi. Mungu wetu mwenye upendo anamjali sana kila mmoja wetu. Anajua kabisa mateso yoyote yanayoweza kutupata. Mtunga-zaburi alisema: “Macho ya BWANA huwaelekea wenye haki, na masikio yake hukielekea kilio chao. BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa.” (Zaburi 34:15, 18) Mungu anamsaidiaje kila mmoja wetu? Si lazima aondoe jambo linalofanya tuteseke. Lakini yeye amewapa maandalizi tele wale wanaomwomba msaada. Neno lake lina mashauri yanayofaa ambayo yanaweza kutusaidia sana. Katika kutaniko, Mungu ameweka waangalizi wanaostahili kiroho, ambao hujitahidi kuwa na huruma kama yeye wanapowasaidia waabudu wenzao. (Yakobo 5:14, 15) Akiwa “Msikiaji wa sala,” Mungu huwapa “Roho Mtakatifu wale wanaomwomba.” (Zaburi 65:2, NW; Luka 11:13) Maandalizi hayo yote ni uthibitisho wa “huruma nyororo ya Mungu wetu.”—Luka 1:78.

Utaitikiaje upendo wa Yesu?
Je, si jambo lenye kusisimua kutafakari juu ya upendo wa Baba yetu wa mbinguni? Katika makala iliyotangulia, tulikumbushwa kwamba Baba Mungu ameonyesha nguvu, haki, na hekima yake kwa njia ya upendo ili kutunufaisha. Na katika makala hii tumeona kwamba kwa njia ya pekee, Mungu ameonyesha upendo wake moja kwa moja kwa kila mmoja wetu na kwa wanadamu kwa ujumla. Sasa kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza, ‘Nitaitikiaje upendo wa Yesu?’ Na uitikie kwa kumpenda kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote. (Marko 12:29, 30) Maisha yako ya kila siku na yaonyeshe kwamba una tamaa ya kutoka moyoni ya kumkaribia Mungu hata zaidi. Na Yesu, Mungu ambaye ni upendo, na akukaribie hata zaidi—milele!—Yakobo 4:8.
Mungu awabariki sana.

Yesu anakupenda.

Max Shimba

Max Shimba Ministries @ 2015.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW