Monday, August 10, 2015

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA SABA)

Je, Yesu ni Mwana wa Mungu?
Je, Isa bin Mariam ni Mwana wa Mungu?

Biblia inasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu. Katika hii mada, tuanze kwa kuangali, Je, Biblia inasema nini kuhusu Yesu? Kumbuka kuwa, Biblia ndio ilikuja kwanza kabla ya Quran. Ushahid unonyesha kuwa Biblia ilikuwepo miaka 632 kabla ya Quran kuandikwa na marafiki zake Muhammad.


YESU NI MWANA WA MUNGU

Tunaona hapa Biblia inatuambia YESU KRISTO ni Mwana wa Mungu (YOHANA 20:30-31) hapa Yesu mwenyewe anasema yeye ni Mwana wa Mungu ( MATHAYO 26:59-64; 16:13-17 ) , Neno Mwana linamzungumzia Yesu Mwana siyo kuwa Mungu anazaa la hasha

Yesu anaitwa mwana wa Mungu kwa sababu alizaliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Hata sisi tumezaliwa kwa mara ya pili kwa Roho tunapo mwamini Yesu Kristo hivyo tunahesabika kuwa ni wana wa Mungu.(WAFILIPI 2:14-15,YOHANA 1:12). Kwahiyo Yesu anapoitwa Mwana wa Mungu maana yake ni chapa ya  Mungu (HUIOS) WAEBRANIA 1:1-3. Ndiyo maana hapa Yesu anawaambia wanafunzi wake, mumeniona mimi ; mumemuona Mungu, maana yake ndiyo hiyo (HUIOS) yaani chapa ya Mungu (YOHANA 14:7-9)

Tunaona hapa Yesu alisema Yeye ni Mwana wa Mungu  (YOHANA 9:35-37)
Shetani naye anajua kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (MARKO 3:11,LUKA 4:41).
Malaika nao wanasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (LUKA 1:30-35)
Mungu mwenyewe anasema kuwa Yesu ni Mwanangu mpendwa (MATHAYO 3:17,MATHAYO 17:5   )


ISA WA QURAN SIO MWANA WA MUNGU

Kama kuna jambo ambalo Allah Mungu anayeabudiwa na waislamu analikataa sana kupitia Qurani basi jambo hilo si lingine bali ni uwana wa Mungu. Allah anasema hivi.
Quani 6:101 Suratul Al-An-am [Wanyama]
Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.
Qurani 9:30 Suratul At-Tawba [Kutubu]
Na mayahudi wanasema “uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu;”na “Wakristo wanasema Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasina na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyenzi Mungu uwaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa!

Allah anasema katika aya hizo hapo juu kuwa, yeye hana Mwana na kuwa Wakristo na Wayahudi wanamsingizia Allah kuwa na Mwana. Allah anasema kuwa, yeye hana Mwana kwasababu hana MKE. Ikiimanisha kuwa, Allah hana uwezo wa kuwa na Mwana bila ya kufanya tendo la ndo na Mwnamke. Huu ni ushahid tosha kuwa, Allah sio mjuzi wa yote, maana hawezi kuwa na mwana bila ya mke. 

Hebu tuangalie aya zingine za Biblia zinasema nini kuhusu Yesu.
1. Mathayo 17:5 ….Huyu ni mwanangu mpendwa wangu…
2. Malaika wa Mungu alisema hivi.
Luka 1:30-31,35
Malaika akamwambia usiogope Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu.

Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa.

Leo tumejifuinza kwa mara nyingine tena kuwa Isa wa Quran sio Yesu wa Biblia kwa kuwa Isa wa Quran yeye sio Mwana wa Mungu.
Katika huduma yake,

Max Shimba

Max Shimba Ministries

Copyright © Max Shimba Ministries 2015

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW