Monday, August 3, 2015

JE, NI NANI MUUMBAJI, ALLAH AU YEHOVA?

Kila mtu mwenye kufuata Dini huamini kuwa Mungu ndiye muumbaji ambaye ameumba wanandamu, wanyama na vyote tunavyoviona na vile tusivyoviona. Hivi yafaa tuangalie kile kinachosemwa na Yehova kuhusu uumbaji na vile Allah anavyosema. Je, kauli zao zinapatana au zinatofautiana?
Je, mtu ameumbwa kwa mfano wa nani?
Allah anasema hivi;-
Qurani112:1-4 Suratul Al-Ikhlas (utakaso)
Sema: Yeye ni Mwenyenzi Mungu mmoja (tu) Mwenyenzi Mungu (tu) ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe vyake vyote kwa kumuabudu na kumuomba na kumtegemea) Hakuzaa wala hakuzaliwa Wala hana anayefanana naye hata mmoja.
Kadiri ya aya hii Allah asema kuwa mungu hakuzaa wala hakuzaliwa wala hana mfano wa mtu au watu Yehova anasema hivi kuhusu mtu au watu……
Mwanzo1:26-27
Mungu akasema “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale samaki wa baharini, ndege wa angani na wanyama , na nchi yote, pia na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba.
Hapa tunaona Mungu wetu Yehova ameumba mtu kwa mfano wake, lakini Allah anasema hana anayefanana naye hata mmoja……Swali kwako mfuatiliaji: Je, Allah ndiye Yehova? Tafadhali usome aya hizi ili kujua zaidi (Mwanzo 5:1-2, 9:6, 1Korintho 11:7, Kolosai 1:15, 3:10, Matendo 17:28-29, Yakobo 3:9). Pengine waweza kusema Je, Mungu amefanana na mimi kivipi?Jua kwamba Mungu ni Roho (Yohana 4:24) Naye alitupa pumzi(yaani roho ya uhai (Mwanzo 2:7))isitoshe Mungu ndiye Baba wa roho zetu (Waebrania 12:9) Mungu anasema Roho zetu ni mali yake(Ezekieli 18:4,Hesabu 16:22)
Kuapa kwa Mungu kuhusu viumbe
Qurani 91:1-7 Suratul Ash-Shams (Jua)
Naapa kwa jua na kwa mwangaza wake. Na kwa mwezi unapoliandama. Na kwa mchana unapolidhihirisha. Na kwa usiku unapolifunika.Na kwa mbingu na kwa Aliyezijenga. Na kwa ardhi na Aliyeitandaza. Na kwa nafsi (roho) na Aliyeitengeneza.
Qurani 92:1-3 Suratul Al-Layl (Usiku)

Naapa kwa usiku ufunikapo (kila kitu). Na kwa mchana uangazapo. Na kwa aliyeumba kiume na kike.
Hapa tunaona Allah Mungu anayeabudiwa na Waislamu anaapa kwa mbingu na kwa aliyezinjenga, kwa ardhi na aliyeitandaza. Je, huyo mtandazi wa ardhi na mjengaji wa mbingu ni nani? Qurani inaendelea kuhadithia hivi……..
Qurani 45:22 Suratur AL- Jathiyah (kiyama/ kupiga magoti)
Na mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi kwa haki…
Qurani 44:7-8 Suratul Ad-Dukhan (moshi)
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake,ikiwa mnayo yakini (basi yakinisheni haya) Hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye anahuisha na kufisha. Mola wetu na ni mola wa wazee wenu (wote) wa mwanzo (na mola wa kila kitu)
Hapa tunaona kuwa Allah kupitia Qurani anasema kuwa mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi na tena anasema hakuna aabudiwaye ila yeye. mjengaji wa mbingu na mtandazaji wa ardhi anajieleza hivi ……
Isaya 44:24
BWANA,mkombozi wako yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi, “Mimi ni BWANA, nifanyaye vitu vyote, nizitandaye mbingu peke yangu, niienezaye nchi. Ni nani aliye pamoja nami?”
Mungu wetu Yehova anasema mimi ninafanya vitu vyote.
(Soma Isaya 45:6-7, 11-12, Yeremia 27:5) Bila shaka Yehova ndiye muumbaji wa vitu vyote
JE Mungu Yehova aliapia vitu alivyoviumba kama Allah?
Isaya 45:22-23
Niangalieni mimi mkaokolewe, Enyi ncha zote za dunia. Maana mimi ni Mungu hapana mwingine. Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba, mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.
Waebrania 6:13-16
Kwa maana Mungu alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake. akisema “Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza, Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi. maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo kwa kuyathibitisha.
Hapa tunaona Mungu wetu Yehova haapi kwa mtu wala vitu alivyoviumba kama Allah anavyoapa, bali Yehova anasema “Naapa kwa nafsi yangu”.Waweza pia kusoma jinsi Yehova alivyoapa kwa nafsi yake katika aya hizi;-(Isaya 14:24 na Mwanzo 22:16)
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW