Wednesday, February 21, 2018

ALLAH S.W.T ANAMUHESHIMU SANA MWANAMKE WA KIISRAEL KULIKO MWANAMKE WA KIISLAMU!






Allah S.W.T Mungu anayeabudiwa na Waislamu Misikitini, ameonesha heshima kubwa sana kwa mwanamke wa Kiisrael, kuliko kwa mwanamke wa Kiislamu.
Katika Uislamu mnyama anayeitwa Mbwa anahesabika kuwa ni mnyama najisi, yaani mchafu, na hata anayehusiana naye kwa ukaribu naye huhesabika kuwa ni najisi katika Uislamu.
Lakini linapokuja suala la mnyama huyo huyo mbwa ikiwa anayehusika naye ni Muisraeli, Allah humsamehe dhambi zake bila kujali kwamba amehusika na mbwa.
Hii inaonesha kwamba Allah anawaheshimu sana Waisraeli kwa Uisraeli wao tu hata kama wamehusika na matendo mabaya, huku, hali ikiwa ni tofauti pale Muislamu anapohusika na mnyama huyo kwa namna yoyote ile.
Katika kitabu cha hadithi sahihi za Uislamu kiitwacho Sahih Al-Bukhari-kitabu kinachofuata kuaminiwa katika Uislamu baada ya Qurani-Juzuu 4, Hadithi Na.673, kuhusu mwanamke wa Kiisraeli, imeandikwa:
“Narrated Abu Huraira (r.a): The Prophet (peace be upon him) said, “While a dog was going around a well and was about to die of thirst, an Israel prostitute saw it and took off her shoes and watered it. So Allah forgave her because of that good deed.”
(Tafsiri: Imesimuliwa na Abu Huraira (radhi za Allah ziwe naye): Nabii alisema, “Mbwa alipokuwa akizunguka zunguka kisimani akiwa karibu kufa kwa kiu, kahaba wa Kiisraeli alimwona na akatoa viatu vyake na kumnyweshea maji. Hivyo, Allah alimsamehe ukahaba wake kwa sababu ya tendo lake lile jema.”)
Kwa upande wa Uislamu hali ni tofauti, mwanamke huyo wa Kiislamu yeye thamani yake amefananishwa na Mbwa na punda.
Katika kitabu cha Hadithi sahihi za Kiislamu cha Al – Lu’lu’ war- Marjan kitabu cha 1 Hadithi na. 90 ukurasa wa 163), imeandikwa,
“Hadithi ya Aisha (r.a) kutoka kwa Masruq (r.a) amesema vilielezwa mbele yake (Aisha) vinavyokata sala, mbwa, punda na mwanamke, akasema mumetufananisha na punda na mbwa” Walahi Mtume (s.a w) alisali nani niko juu ya kitanda kati yake na Qibla nimelala na inanijia haja lakini naona vibaya kukaa nikamuudhi Mtume (s.a w) kwa hiyo ninapenya miguu mwake ili nitoke.”
Katika hadihi hii Aysha mke mdogo kabisa wa Muhammad s.a.w analalamika kujikuta anafananishwa thamani yake na mbwa na punda, wakati yeye ni binadamu. Aliolewa na Muhammad akiwa na miaka 6 akashiriki tendo la ndoa akiwa na miaka 10.
Mwanamke wa Kiisareli pamoja na ukahaba wake bado Allah alimheshimu kwa utu wake na Uisraeli wake. Khaba anaweza kutubu ndiyo maana alisamehewa.
Mwanamke katika Uislamu ameitwa pia kwamba yeye ni mkosi. “Hadithi ya Ibn Umar (r.a) amesema, kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema, “Hakuna ‘adwa (kuambukiza) wala Tiyara (mkosi), ama mikosi ipo katika maeneo matatu, Mwanamke, Nyumba, na Mnyama. (Al – Lu’lu’ war- Marjan kitabu cha 3 Hadithi. 1439 uk. 836)
Kutokana na habari hizo mbili kutoka imani tofauti, lakini zote zikimhusu mwanamke, binafsi ninagundua kwamba, unyonge wa wanawake katika Uislamu unasababishwa na wao kuwa Waislamu, wala si Uanawake wao.
Ingekuwa ni kwa sababu ya Uanawake wao, basi tungemuona Allah akiwa mkali na akimdhalilisha pia kahaba wa Kiisareli na kumsamehe.
Mwanamke wa Kiislamu anayeamua kuukataa unyonge na kudhalilishwa kwa aina hii hana chaguo jingine isipokuwa kutafuta mahali atakapothaminiwa.
Imeandikwa,
“26 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. 29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.” (Galatia 3:26-29).....................Imeandikwa na na Mtafiti, Mwinjilisti Kaka Daniel Mwankemwa

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW