Monday, March 18, 2019

BIBLIA NI KITABU KILICHO TOKA KWA MUNGU


Biblia ni zawadi ya Mungu, na tunapaswa kumushukuru sana kwa zawadi hiyo. 

Biblia ni kitabu kilicho tofauti na vitabu vingine. Inatujulisha mambo ambayo hatungejua. Kwa mfano, inatuelezea namna dunia na mbingu zenye kujaa nyota viliumbwa, na namna mwanaume na mwanamuke wa kwanza waliumbwa. Kanuni za Biblia ni za kweli na zinaweza kumusaidia mutu ajue namna ya kushindana na magumu na mahangaiko ya maisha. Inatufasiria namna Mungu atatimiza kusudi lake na kufanya maisha yawe mazuri sana duniani. Kweli, Biblia ni zawadi yenye kufurahisha kabisa!

Biblia inapatikana katika luga zaidi ya 2 500, yote nzima ao kwa sehemu; kwa hiyo watu wengi duniani wanaweza kuipata (zaidi ya 90%). 

Biblia zaidi ya milioni moja zinagawanywa kila juma! Mamilioni na mamilioni ya Biblia zimekwisha kuchapishwa, iwe yote nzima ao kwa sehemu. Kwa kweli, hakuna kitabu kingine kinacholingana na Biblia.

Biblia ‘imeongozwa na Roho ya Mungu.’ (2 Timotheo 3:16) Maana yake nini? Biblia yenyewe inajibu hivi: “Wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na Roho Mtakatifu.” (2 Petro 1:21) 

Kwa hiyo, Biblia yote nzima ni “neno la Mungu.”​—1 Wathesalonike 2:13.

Shalom,

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW