Watu wengu wanafikiri kuwa, Mungu aliwaumba ili wawe watu wa kawaida tu, la hasha, Mungu amekuumba wewe ukiwa Tajiri. Ukisoma kuhusu Adam katika Kitabu cha Mwanzo, utaona kuwa, Mungu alimuumba Adam na Hawa baada ya kuumba dunia na kila kitu. Baada ya Adam na Hawa kuubwa, walikabidhiwa kila kitu kilichopo hapa duniani. Huo ni Utajiri mkubwa sana. Soma. Mwanzo 1: 28 Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.” 29Kisha Mungu akasema, “Tazama, nawapeni kila mmea duniani uzaao mbegu, na kila mti uzaao matunda yenye mbegu; mbegu zao au matunda yao yatakuwa chakula chenu. 30Nao wanyama wote duniani, ndege wote wa angani, viumbe vyote vitambaavyo, naam, kila kiumbe chenye uhai, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikawa hivyo.
UNAONA: Mungu alimpa kila kitu Adam na Mkewe Hawa. KUMBE ADAMA NA HAWA WALIKUWA MATAJIRI. Je, wewe unasubiri na kungoja nini? Muamuru Shetani akurudishie mali zako zote kwa Jina la Yesu.
Mithali 3:16; (Yesu kristo Mnazareti) ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na Heshima katika mkono wake wa kushoto.
MAANA YA TAJIRI:
Tajiri ni yule mtu mwenye mali nyingi na mwenye moyo wa kusaidia wenye uhitaji na anayefaidi mali zake kwa amani kuu na sio tu kumiliki na kutawala mali nyingi. Huyo ndiye Tajiri katika Bwana anayesomeka pajini mwa uso wake hata pasipo kujua utajiri anaomiliki. Lakini ile kuwa na roho mtakatifu ni utajiri unaothihirika hadi mwilini. Kama ilivyokuwa kwa Mfalme Sulemani (2 Mambo ya Nyakati 1:15) inasema; "Mfalme Sulemani alifanya fedha na dhahabu kuwa kama mawe ule wingi wake huko Yerusalemu na mierezi akafanya kuwa kama mikuyu iliyoko shefela kwa kuwa mingi". Hii yote inatokana na kuwa na Bwana Yesu wa Nazareti ya kwamba ni utajiri utajirishao wengi na sio tu muhusika yaani ni utajiri usio binafsi na ndiyo utajiri wa kweli unaomaanishwa.
Tajiri ni yule mtu mwenye mali nyingi na mwenye moyo wa kusaidia wenye uhitaji na anayefaidi mali zake kwa amani kuu na sio tu kumiliki na kutawala mali nyingi. Huyo ndiye Tajiri katika Bwana anayesomeka pajini mwa uso wake hata pasipo kujua utajiri anaomiliki. Lakini ile kuwa na roho mtakatifu ni utajiri unaothihirika hadi mwilini. Kama ilivyokuwa kwa Mfalme Sulemani (2 Mambo ya Nyakati 1:15) inasema; "Mfalme Sulemani alifanya fedha na dhahabu kuwa kama mawe ule wingi wake huko Yerusalemu na mierezi akafanya kuwa kama mikuyu iliyoko shefela kwa kuwa mingi". Hii yote inatokana na kuwa na Bwana Yesu wa Nazareti ya kwamba ni utajiri utajirishao wengi na sio tu muhusika yaani ni utajiri usio binafsi na ndiyo utajiri wa kweli unaomaanishwa.
Biblia katika Waefeso 3:8-11 pia inasema kwa habari ya Mtume Paulo; “Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa UTAJIRI WAKE KRISTO USIOPIMIKA; na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote, kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi. Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu."
“Na Mungu wangu atawajazeni KILA MNACHOHITAJI KWA KADIRI YA UTAJIRI WAKE KATIKA UTUKUFU, NDANI YA KRISTO YESU" (Wafilipi 4:9)