Monday, July 11, 2016

WAISLAM WENYE SIASA KALI WA BOKO HARAMU WAKAMATWA NDANI YA KANISA.



WATU sita kati ya 100 wanaoaminika kuwa ni memba wa kundi la kigaidi la Boko Haram waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Ulinzi la Nigeria wamekamatwa wakiwa wamejificha Kanisani huko Festac Jijini Lagos.
Zoezi hilo lilifanikiwa jana kutokana na ushirikiano wa raia wema wa maeneo ya karibu kutoa taarifa kwa jeshi hilo kuhusu kuwepo kwa watu waliyowatilia shaka wakiingia kwenye Kanisa hilo lililopo mjini Festac kwa lengo la kujificha ilihali muonekanao wao sio wa kusali.
Washukiwa hao waliripotiwa kutafutwa na jeshi hilo tangu wiki iliyopita baada ya kufanya shambulizi na kutokomea huko mjini Maiduguri Borno.
Watuhumiwa waliokamatwa jana wametamnbulika kwa majina ya Ali Ibrahim, Ahmed Abubakar, Kamsalem Goigoi, Adams Ibrahim, Mohammed Ibrahim na Ali Blam Babagana waliokuwa wakitoroka kutoka Borno walikotekeleza shambulio.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW