Saturday, July 23, 2016

ALLAH ANASEMA MUHAMMAD ALIKUWA ANATENDA DHAMBI KILA SIKU


Ndugu msomaji,
Wakati Biblia inasema Yesu alikuwa hana dhambi, hivi ndivyo Kuran na Bukhari Hadith zinavyosema kuhusu Muhammad.
1. Hebu tuanze kusoma Sahih hadith kuhusu Muhammad wa kwenye Quran.
Muhammad pamoja na watu wake waliteka nyara misafara ya wafanya biashara na wasafiri mbalimbali. Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 37 sura ya 8 na.495 uk.280 inasema "wakati Allah alipomfanya mtume kuwa tajiri kutokanana na ushindi" 1/5 ya mateka ya vita iliwekwa katika hazina na Sahih Muslim juzuu ya 2 kitabu cha 5 sura ya 401 na.2348 uk.519 inasema familia ya Muhammad ilikuwa na hisa ndani yake. Utekaji nyara wa mali za watu wa kwanza kufanywa na Waislam ulijulikana kama Nakha la Raid. Wakati wa mwezi wa kusimamisha vita kwa muda, wafuasi wake waliushambulia msafara kwa kuuvamia na kuua mtu mmoja, na kuwafanya watu waliosalia kuwa watumwa, na kuchukua nyara. Muhammad mwenyewe aliongoza uvamizi wa pili pale Badr. Muhammad aliongeza utajiri wake kwa kuyashambulia makazi ya Wayahudi ya Khaibr. Yeye na wafuasi waliokuwa waaminifu kwake walijitwalia nyara na wake (Je Muhammad alihitaji mke mwingine?) wa Wayahudi wanaume 700-1000 wa kabila la Banu Quraiza waliowakata vichwa baada ya kujisalimisha.
2. Allah anamsihi Muhammad aombe Msamaha wa Madhambi anayo tenda kila siku.
Katika sura 40:55 na 48:1-2, Allah anamwambia Muhammad kuomba msamaha kwa ajili ya dhambi zake (au udhaifu wake). Sasa, watu hawahitaji msamaha kwa ajili ya madhaifu ya miili bali maadili. Sahih Muslim juzuu ya 1 kitabu cha 4 sura ya 268 na.1695 uk.373 inasema Muhammad aliomba, "Nilijikosea mwenyewe na kufanya toba ya dhambi zangu. Nisamehe dhambi zangu . . ." Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 2 sura ya 13 na.19 uk.23; juzuu ya 1.12.57 na.781 uk.434; juzuu ya 6.60.3 na.3 uk.4; juzuu ya 8.75.3 na.319 uk.213; na juzuu ya 8.75.62 kabla ya na.407 uk.271 kabla ya kueleza dhambi za Muhammad. Mambo bayana yaliyoelezwa kwenye Bukhari juzuu ya 1.4.70 na.234 uk.148; Bukhari juzuu ya 8.82.1 na.794-795 uk.520 ni kukata watu mikono na miguu, kuchoma macho yao, na kuwanyima maji hadi kufa baada ya kukatwa miguu na mikono.
Angalia Bukhari juzuu ya 8.82.3 na.796 sura ya 4 uk.797; Bukhari juzuu ya 6 sura ya 150 kabla ya na.198 uk.158-159 pia Fiqh us-Sunnah juzuu ya 1 uk.133.

Bila shaka utakubali kwamba hizi ni dhambi nzito sana. Kwa vile Muhammad alifanya hivi, alihitaji sana msamaha. Swali la kidadisi ni hili: "Ni nani hasa anayelipa gharama ya dhambi zako?" Yesu alisema alilipa fidia ya dhambi zetu. Uislam haufundishi kuwa kuna mtu yeyote aliyelipa gharama. Je, dhambi zako zinalipwaje, au Allah anazifumbia macho baadhi ya dhambi na kuadhibu nyingine??
Watu wengine wanaweza kufikiri kuwa uovu hauna madhara yoyote ili mradi mtu anajiita Muislam. Katika karne hii Waislam wanawaua wakiristo na kufanya mauaji ya kinyama kwenye vijiji vyao katika nchi za Sudan, Nigeria na Indonesia. Wakati watu walioitwa wakristo waliwaua Waislam, watu walisema kuwa wanafanya kinyume cha tabia ya Kristo. Wakati Waislam wanawaua Wakristo, wanaomwabudu Mungu wa kweli, sijawahi kusikia mtu yeyote akisema wanafanya kinyume cha tabia ya Muhammad.
Nisamehe kwa kusema bila kuficha kiasi hiki, lakini mauaji ya watu wanaomwabudu Mungu yanayofanywa na Waislam lazima yaachwe. Waislam wanapohalalisha mauaji haya kwa sababu hata nabii wao alifanya hivyo, watu hushangazwa na nabii wao, na Allah wao ambaye anatengua neno lake, na chimbuko la Uislam.
Mtume wa Allah "Muhammad" alikuwa mtenda dhambi na alikufa na dhambi kubwa kubwa.
Karibuni kwa Yesu aliye hai na Mwokozi wa Maisha yako leo.
Tafakari
Chukua hatua
Okoka
Max Shimba Ministries Org.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW