Saturday, July 23, 2016

QURAN INASEMA KUWA, NABII LAZIMA AFANYE MIUJIZA; MUHAMMAD AKIRI KUWA YEYE NI MTUME BANDIA NA HAKUFANYA MIUJIZA


Qur’an nayo inathibitisha kuwa manabii na mitume ni lazima wafanye miujiza.
Qurani 40:78 Suratul Al-Muumini [Waumini] inasomeka “Na kwa yakini tumewatuma mitume kabla yako wengime katika wao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia na haikuwa kwa mtume yoyote kuleta muujiza wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu”
Muhammad hakuwai fanya muujiza wowote ule ili kuthibitisha madai ya unabii na utume wake.
Qur’an 29:50 Suratul Al-Ankabuut (Buibui). “Na walisema “Mbona hakuteremshiwa miujiza kutoka kwa Mola wake? Sema miujiza iko kwa Mwenyezi Mungu tu (akitaka atakuteremshieni na kama hataki basi),nami hakika ni mwonyaji mbainishaji (dhahiri tu).” (Taz. Qur,an 6:35-37 13:7,)
Muhammad anakiri kuwa yeye hakuwai fanya miujiza. Hivyo Kutokana na Quran yao wenyewe Muhammad ni mtume bandia.
Zaidi ya hapo Muhammad hakuwai fanya unabii wowote ule. Sasa Nabii bila ya unabii inawezekanaje?
Sifa mojawapo ya Nabii ni kutoa unabii. Muhammad hakuwai toa unabii wowote ule.
KUROGWA KWAKE MUHAMMAD
Zaidi ya hayo tunaona Muhammad alirogwa. Kurogwa ni hali ya mtu kuathirika na nguvu za giza yaani uchawi. Je nabii au mtume wa Mwenyezi Mungu wa Kweli anaweza kurogwa?
Amesema Mwanaisha Mkewe Mtume kuwa "Yahudi Mmoja aitwaye Labiid bin Al'answan alimroga Mtume Muhammad, ikawa Mtume baadhi ya Nyakati huchanganyikiwa na kuanza kuita Ovyo ovyo na kupiga makelele. (Sahih Muslim J. 4 uk. 38-39)
Huu ni uthibitisho mwingine mzito unaoonesha kuwa utume wa Muhammad una utata.
MASWALI:
(a) Hivi, kuna Mtume au Nabii yeyote yule ambaye alikiri kurogwa kama Muhammad?
(b) Hivi Allah alikuwa wapi wakati Muhammad anarogwa? [Ingawa Quran inakiri kuwa aliye teremsha uchawi/urogi ni Allah]
(c) Wapi tunasoma kuwa Muhammad aliombewa na kutoa huo uchawi/urogi aliofanyiwa na Labiid bin Al'answan?
YAANI INA MAANA MUNGU ALIKOSA MTU WA KUTUMA MPAKA ATUME MTU ALIYECHEWA NA MASHETANI KAMA HUYU?
Ndugu msomaji,
Muhammad hakuwa Mtume wa Mungu na wala hana sifa za KITUME.
1. Muhammad hakuwai ongea na Allah aliye mtuma.
2. Muhammad alikuwa na Shetani tokea kuzaliwa kwake.
3. Muhammad alikiri kuchezewa na Shetani wakati wa kusimikwa utume wake Pangoni.
4. Muhammad alikiri kuwa Shetani amechezea akili na nafsi yake.
5. Muhammad alikiri kuwa alirogwa na Labiid bin Al'answan.
SASA WAISLAM, NIONYESHENI, wapi kwenye Taurat, au Zaburi au Injili kama kuna Mtume aliye na sifa za ajabu kama za Muhammad.
Karibuni kwa Yesu ambaye ndie Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW