Sunday, December 23, 2018

KWANINI WAKRISTO TUNASHEREHEKEA KRISMAS? = SEHEMU YA KWANZA =

Image may contain: text
SOMO:-UKWELI KUHUSU SIKUKUU YA KRISMASI
NA
SABABU ZA MSINGI KI-BIBLIA ZINAZOTUFANYA WAKRISTO KUSHEREKEA KRISMASI .
Ili iwe rahisi kwetu kulielewa vizuri somo hili. Tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele vinne ambavyo ni:-
1. MAANA YA NENO KRISMASI
2. HISTORIA YA KRISMASI NA TAREHE 25/ DESEMBA
3. MAMBO YA KUYAELEWA NA KUYAZINGATIA KUHUSU HISTORIA YA KRISMASI
4. SABABU ZA MSINGI KI-BIBLIA ZA KUWAFANYA WAKRISTO TUSHEREKEE KRISMASI
Mistari muhimu ya kukumbuka :-
L U K A 2:9-11:-"Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang’aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana."
Z A B U R I 118:22-24:"Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni. Neno hili limetoka kwa BWANA, Nalo ni ajabu machoni petu. Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA, Tutashangilia na kuifurahia."
Amen!.
1/ KIPENGELE CHA KWANZA
MAANA YA NENO KRISMASI
KRISMASI (pia Noeli) ni sikukuu ambayo Wakristo wengi husheherekea kuzaliwa kwake mwokozi Yesu Kristo zaidi ya miaka 2000 iliyopita duniani .
Kwa kawaida husheherekewa tarehe 25 Desemba katika Ukristo wa magharibi na tarehe 6 Januari katika ule ukristo wa mashariki.
Kuna majina mawili yaliyo ya kawaida kwa Kiswahili kwa ajili ya sikukuu hii
Neno KRISMASI linatokana na neno la Kiingereza lenye maana ya "Christ`s Mass" yaani misa au ibada ya Kristo.
Neno Noeli inatokana na neno la Kiingereza "Noel" (au "Nowell") ambalo limepokewa kutoka lugha ya Kifaransa "No�l". Hilo ni ufupisho wa neno la Kilatini "Natalis (dies)", "(siku ya) kuzaliwa".
N.B:- IBADA NA SHEREHE YA KUZALIWA KWA YESU (KRISMASI) IKO KI-BIBLIA.
Hili si suala tu ambalo limetungwa na wanadamu fulani. La hasha! Hili ni jambo ambalo lipo ki-biblia kwa kuanzishwa na Mungu mwenyewe.
Tukio la kwanza la IBADA NA SHEREHE YA KUZALIWA KWA YESU KRISTO lilifanyika tokea Yesu alipozaliwa. Na watu wa kwanza kabisa kusherekea kuzaliwa kwake walikuwa majeshi ya malaika wa Mungu. Na pia wanadamu pia walimsifu Mungu na kumtukuza kwa kuzaliwa kwake mwokozi Yesu Kristo. Kwa hiyo suala la Krismasi liko ki-biblia
[ LUKA 2:7-14,20, 25-38].
2/ KIPENGELE CHA PILI
HISTORIA YA KRISMASI NA TAREHE 25/DESEMBA
Tarehe halisi kabisa ya kuzaliwa kwake Yesu haijulikani kwa sababu utamaduni wa Wayahudi wa wakati ule haukuwa na sherehe au kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa.
Lakini baadaye Ukristo ulienea katika Dola la Roma kati ya mataifa yaliyokuwa na kawaida ya kuzingatia siku ya kuzaliwa. Hivyo ilijitokeza hamu ya kusheherekea pia sikukuu ya kuzaliwa kwake mwokozi Kristo. Ndiyo asili ya sikukuu ya Krismasi.
Tangu mwanzo wa karne ya 3 BK kuna kumbukumbu ya waandishi mbalimbali waliojadili tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo.
Habari za kwanza kabisa za makadirio ya tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu zinapatikana kutoka Misri mnamo mwaka 200.
Mwandishi Mkristo Klemens wa Alexandria alilalamikia udadisi wa wataalamu kadhaa wa Misri waliodai kwamba wamekadiria tarehe hiyo katika mwezi Mei, wengine katika Aprili. Alisema pia kuwa kikundi cha Kikristo cha wafuasi wa Basilides huko Misri walisheherekea Epifania pamoja na kuzaliwa kwake Yesu tarehe 6 Januari.
Labda kadirio la tarehe ya 25 Desemba pia lina asili katika Misri. Kuanzia mwaka 200 (kwa mara ya kwanza katika maandishi ya Sixtus Julius Africanus) tunasikia kwamba wataalamu wa Misri walifikiri tarehe 25 Machi ilikuwa tarehe ya kufa kwake Kristo na pia siku ya utungaji mimba wake. Kwa kuongeza miezi tisa ya mimba inajitokeza 25 Desemba kama tarehe ya kuzaliwa.
Inaonekana tarehe 25 Desemba ilijitokeza wakati huo. Kuna taarifa ya mwaka 204 kutoka Ipolito wa Roma kwamba tarehe 25 Desemba ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo.
KRISMASI NA SIKUKUU YA SOL INVICTUS
Wataalamu mbalimbali walidai kwamba Kanisa lilipachika sikukuu ya Kristo kwenye tarehe hiyo kwa nia ya kufanya ichukue nafasi ya sikukuu ya jua kama mungu "Sol invictus" (yaani "Jua lisiloshindika").
Lakini pengine mambo yalikwenda kinyume, yaani kwamba Makaisari walianzisha sikukuu hiyo, halafu wakaipanga tarehe ya Krismasi ili kushindana na Ukristo uliokuwa bado chini ya dhuluma ya serikali yao lakini ulikuwa unazidi kuenea.
Aliyeingiza sikukuu ya "Kuzaliwa Jua" (Mitra) huko Roma ni Eliogabalus (kaisari kuanzia 218 hadi 222). Baadaye kaisari Aurelianus akaithibitisha rasmi mwaka 273, hatimaye ikahamishiwa tarehe 25 Desemba.
Wakati wa kaisari Licinius (308-324) sikukuu hiyo ilikuwa ikiadhimishwa bado tarehe 19 Desemba.
Mwandishi wa kikatoliki MARIO RIGHETTI kwa utii kabisa anakubali kwamba, " ili kuwezesha kukubalika imani kikristo kwa wapagani , Kanisa la Roma (chini ya mfalme Constantinel aliyeongoka na kubatizwa kuwa mkristo), WAKAIGEUZA KUTOKA sikukuu ya kipagani ya kumpa heshima " Invincible sun" Mithra na mshindi wagiza , wakaona ni busara Desemba 25 kuwa ni sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo".
( Rejea :- Historia ya mwongozo wa kiliturujia, 1955, vol. 2.P.67).
Kutoka Roma, uliokuwa mji mkuu wa Dola la Roma, sherehe ya 25 Desemba ilienea kote katika Ukristo.
Wakristo wengi husheherekea tarehe 25 Desemba (Wakatoliki na sehemu ya Waprotestanti na Waorthodoksi). Kati ya Waorthodoksi kuna tarehe nyingine, hasa 6 Januari kutokana na tofauti katika kalenda."
Mwisho wa kunukuu
3/ KIPENGELE CHA TATU
MAMBO YA KUYAELEWA NA KUYAZINGATIA KUHUSU HISTORIA YA KRISMASI.
(1) Kama tarehe 25 Desemba hapo mwanzoni ilikuwa ni sikuu ya kipagani . Halafu Wakaibadilisha kutoka katika imani ya kipagani badala yake ili ichukue nafasi ya kusherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Jambo hilo ni sahihi kabisa mbele za Mungu.
Na katika jambo hilo. Ni ROHO MTAKATIFU aliyelitumia kanisa la Roma chini ya mfalme Constantinel kuibadilisha sikukuu ya kipagani iliyokuwepo , badala yake iwe Chrismasi.
Tendo hilo ni sawa na mtu kumtoa gizani na kumleta kwenye Nuru halisi. Kumtoa katika njia yake upotevu ili kumleta sasa katika njia sahihi ya kweli iliyoonyokaa.
Hakuna tatizo la tarehe 25 Desemba ilyobadilishwa kutoka kwenye sikukuu ya upangani, ili ije kuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Krismas). Jambo ni sahihi kabisa. Kwa mfano Biblia inasema juu ya hilo katika
MATENDO 26:16-18:-"BWANA akaniambia, mimi ni Yesu.... Lakini inuka , usimame kwa miguu yako, maana nimekutokeaa kwa sababu hii , nikuwekee wewe uwe mtumishi na shahidi wa mambo haya uliyoyaona, na wa mambo ambayo katika hayo nitajidhihirisha kwako; nikikuokoa na watu wako, na watu wa mataifa, AMBAO NAKUTUMA KWAO; UWAFUMBUE MACHO YAO, NA KUWAGEUZA WAIACHE GIZA NA KUILEKEA NURU, waziache na nguvu za shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu Mimi".
(2) SIKU ZOOTE NI ZA MUNGU NA HAKUNA SIKU YA SHETANI.
Mtu anayeipinga sherehe ya sikukuu ya krismasi kwa kudai kwamba eti 25 Desemba ilkuwa ni siku ya sikuu ya kipagani. Na hivyo hana haja ya kusherekea Krismasi.
Mtu wa namna hiyo. Tatizo lake hajui wala kuelewa anachokisema badala yake anajidanganya mwenyewe na kujipotosha. Uelewa wake ni mdogo!
Ni muhimu kufahamu vizuri . Siku zote ni za Mungu na hakuna siku ya shetani. Inategemea tu na mtu mwenyewe binafsi anaitumia vipi siku hiyo kwa kufanya mambo ya kumpendeza Mungu au mambo ya shetani !! Lakini hakuna siku maalumu ya shetani . Bali Siku zote ni mali ya Mungu mwenyewe. Na anataka tuzitumie siku zote kumsifu, kumwabudu, kumtukuza na kumpendeza yeye .
Kwa mfano Biblia inasema juu ya hilo katika
MWANZO 1:14:-" MUNGU AKASEMA, na iwe mianga katika Anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka."
ZABURI 105:4:-" Mtakeni BWANA na nguvu zake, utafuteni uso wake SIKU ZOTE".
YOHANA 8:29:-" Naye aliyenipeleka yu pamoja nami: hakuniacha pekee yangu; kwa sababu NAFANYA SIKU ZOOTE yale yampendezayo ".
MATENDO 2:46-47:-" NA SIKU ZOOTE kwa moyo mmoja walidumu ndani ya Hekalu......... wakimsifu Mungu,, na kuwapendeza watu woote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa".
Unaweza kuona! Tusimpe siku shetani. SIKU ZOOTE NI ZA MUNGU, maana yeye ndiye aliyezifanya kuwako. . Kilichobaki ni kwa mtu mwenyewe tu binafsi anaitumia vipi hiyo siku kufanya mapenzi ya nani ya Mungu au ya shetani ?!
Na kwa maana hiyo. Kama tarehe 25 Desemba ilikuwa ni siku ya sikukuu ya wapagani. Hilo lilikuwa ni kivyaoo wenyewe kwa upotofu wa mioyo yao wenyewe walivyoamua kuitumia hiyo kufanya mambo yao ya kipangani. Lakini hilo Bado haimanisha kwamba 25 Desemba basi siku hiyo ni ya wapagani. La hasha !! Itakuwa ni ya kipagani kwetu wakristo iwapo kama tutashiriki mambo yao kipagani kama walivyokuwa wakifanya wao. Lakini siku hii tukiitumia tofauti na jinsi walivyoitumia wao. Hii siyo siku tena ya kipagani, bali ni takatifu kwa Bwana.
TAREHE 25 DESEMBA kwetu sisi wakristo tuliookoka tunaitumia siku hiyo maalumu kwaajiri ya kumuadhimisha BWANA kwa kukumbuka tukio kubwa mno la kuzaliwa kwake Yesu Kristo mwokozi wa ulimwengu. Biblia inasema hivi katika
WARUMI 14:4, 6-7:-" Wewe u nani umuhukumuye mtumishi wa mwingine ? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha. YEYE AADHIMISHAYE SIKU , HUIDHIMISHA KWA BWANA; naye alaye hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu ; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu . Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwenu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake."
Katika siku hii ya tarehe 25 Disemba, tunaitumia kumwadhimisha Bwana, ni siku maalumu na ya kipekee ambayo wakristo tunaitumia kutafakari mambo mengi ya ukuu wa Mungu wetu na upendo wake kwa wanadamu. Tunamshangilia , tunamsifu na kumtukuza, tunamwimbia na kumshukuru Mungu Baba yetu na MWOKOZI wetu Yesu Kristo aliyekuja kutuponya, kutuokoa na kutukomboa wanadamu kutoka kwenye gereza la Ibilisi.
" Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa, ya kwamba YESU KRISTO ALIKUJA ULIMWENGUNI AWAOKOE WENYE DHAMBI; ambao wa kwanza wao ni Mimi".
[YOHANA 3:16-17; LUKA 2:28-34; 1TIMOTHEO 1:15-16].
IKiwa watu wengine wanaweza kukumbuka kusherekea kuzaliwa kwao na wakamshukuru Mungu. Basi ni jambo zuri na bora zaidi kupita yoote kukumbuka kusherekea kuzaliwa kwake mwokozi wetu Yesu Kristo.
(3) HATUSHEREKEI TAREHE BALI KUMBUKUMBU YA TUKIO LA KUZALIWA MWOKOZI WETU ULIMWENGUNI.
Biblia inasema
YOHANA 21:25:-" kuna na mambo MAMBO MENGINE MENGI aliyoyafanya Yesu; ambayo kama yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa. Lakini hizi zimeandikwa; ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mwe na uzima wa milele kwa jina lake".
Nini maana yake? Ingawa haijulikani tarehe na mwezi maalumu aliyozaliwa Yesu Kristo au kuandikwa kwenye Biblia. Ndiyo hatuoni! Kwa sababu mbele za Mungu tarehe ya kuzaliwa Yesu sio jambo la msingi, bali lilo la msingi ni TUKIO LA KUZALIWA KWA YESU, ndiomaana Mungu akaliandika. Matukio mengi aliyoyafanya Yesu hayakuandikwa na Mungu, lakini tukio lake hili la kuzaliwa limeandikwa. Hii ni kwa sababu Mungu anataka kutufundisha, tukio hili ni la msingi sana kwetu kulitafakari.
Kujua tarehe ni ipi hilo sio jambo la msingi kwetu kama ambavyo halikuwa la msingi kwa Mungu . Narudia tena Hoja ya msingi kwetu hapa sio tarehe ngapi mwezi gani , bali HOJA YA MSINGI NI KWAMBA YESU KRISTO AMEZALIWA. Full stop. Kwa sababu lilo la msingi kwetu sio tarehe bali ni kumbukumbu ya tukio lilotendeka la kuzaliwa kwa Yesu Kristo ulimwenguni .
Narudia tena kusisitiza unielewe vyema. La msingi kwetu hapa wakristo hatureshekei tarehe, bali tunasherekea kumbukumbu ya tukio la kuzaliwa kwake Yesu Kristo.
Mbali hata na tarehe 25 Desemba, siku zote na wakati woote tungepaswa kusherekea kukumbuka kuzaliwa kwake mwokozi wetu Yesu Kristo ulimwenguni . Biblia inasema katika
MATHAYO 28:20:-"Na kufundisha kuyashika yoote niliyowaamuru ninyi; NA TAZAMA , MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, hata ukamilifu wa dahari ".
Kwa maana hiyo hiyo hata tunaposherekea 25 Desemba kuzaliwa kwake , bado Yesu yupo pamoja nasi.
4/ KIPENGELE CHA NNE
SABABU ZA MSINGI KIBIBLIA ZA KUWAFANYA WAKRISTO TUSHEREKEE KRISMASI.
Ni kwa sababu zifuatazo:-
(1) Ni taarifa ya agizo la Mungu kwetu kupitia kwa mkono wa malaika.
Biblia inasema katika LUKA 2:10-14:-" Malaika akamwambia, msiogope; kwa kuwa Mimi nawaletea HABARI NJEMA YA FURAHA KUKUU ITAKAYOKUWAKO KWA WATU WOOTE; Maana Leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwaajili yenu, mwokozi Ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia".
Unaweza kuona , hata wingi wa jeshi la mbinguni la malaika waliungamana pamoja na wanadamu kufurahia kwa kusherekea kuzaliwa kwake YESU KRISTO.
ISAYA 9:6-7:-" MAANA KWA AJILI YETU MTOTO AMEZALIWA, tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, mfalme wa Amani......."
Mtu yoyote ambaye anapinga kusherekea sikukuu za Krismasi. Mtu wa namna hiyo bila shaka anasema kwa kutumiwa na roho ya shetani bila kujitambua.
(2) Ni Agizo la Biblia kwamba (SIKU YA KRIMASI) tuishangilie na kuifurahia.
Biblia inasema katika
ZABURI 118:22-24:-" Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni. Neno hili limetoka kwa BWANA, nalo ni la ajabu machoni Petu; SIKU HII NDIYO ALIYOIFANYA BWANA, TUTASHANGILIA NA KUIFURAHIA".
Jiwe kuu la pembeni anayetajwa hapo ni Yesu Kristo (2 Waefeso 2:20). Na siku inayotajwa hapo ni siku yake ya kuzaliwa ( Christmas).
Na Biblia inasema tena katika ZABURI 70:4:-" Washangilie, wakufurahie, wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako waseme daima, Atukuzwe Mungu".
Sasa Yesu Kristo alipozaliwa, yeye ndiye aliyefanyika wokovu wa Mungu wetu [LUKA 2:27-32; 1KOR 1:30]. Na ndiomaana wakristo Leo tunaidhimisha siku hiyo ya Krismas kwa kushangilia na kuifurahia, kwa kuzaliwa kwake mwokozi wetu Yesu Kristo , aliyetupatia wokovu. HALELUYA!!
(3) Kusherekea Krismasi sio dhambi wala kosa, bali ni mapenzi ya Mungu kwetu.
Biblia inasema katika
1 WAKORINTO 10:-" Basi , mlapo , au mnywapo, au MTENDAPO NENO LOLOTE, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu".
WAKOLOSAI 3:17:-" Na KILA MFANYALO, kwa neno au kwa tendo, FANYENI YOOTE katika jina la Bwana Yesu, mkishukuru Mungu Baba kwa Yeye".
Ndiomaana Siku ya Krismasi mbali tu na kusherekea inavyostahili. Lakini bado imekuwa ni siku maalumu na ya kipekee ambayo mambo mengi mema yanayafanyika ya kuumpa Mungu sifa, heshima na utukufu na shukrani tele, kwetu sisi wakristo tuliookoka. Na Mungu anaonekana kwa namna ya kipekee siku hii pia akiwaponya, akiwaokoa, akiwagusa na kuwatembelea watu wengi.
(4) SIKUKUU YA MWANDAMO WA MWEZI NI KIVULI CHA SIKUKUU YA KUZALIWA KWA YESU KRISTO LEO (KRISMAS).
Nyakati za Agano la kale watu waliagizwa kusherekea sikukuu ya Mwandamo wa mwezi, mara tu mwezi ulipoanza kuandama . Watu walisherekea .
Biblia inasema Katika ZABURI 81:3-4:-" PIgeni panda mwandamo wa mwezi, wakati wa mbalamwezi, SIKUKUU YETU. Kwa maana nu sheria kwa Israeli, ni hukumu ya Mungu wa Yakobo ".
Ni muhimu kuelewa Sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi ilikuwa ni picha/mfano/ kivuli cha Yesu Kristo atakayekuja baadaye .
Biblia inasema katika WAKOLOSAI 2:16-17:-" Basi , mtu asiwahukumu ninyi kwa vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au MWANDAMO WA MWEZI, au sabato ; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo ; bali mwili ni wa Kristo ".
Sasa Yesu Kristo Leo yeye ndiye anayeitwa ni Nuru halisi ya ulimwengu. Biblia inatuambia katika YOHANA 8:12:-"Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima".
[ Soma pia YOHANA 1:9-10].
Sasa YESU KRISTO KAMA NURU HALISI iliyokuja katika ulimwengu. Mara tu Wakati huo Alipozaliwa Yesu Kristo katika ulimwengu huu uliojaa Giza . Ilikuwa ni sawa na kama nuru ndogo iliyochomoza na kuanza kuangaza katika ulimwengu huu uliojaa Giza. Na kwa maana hiyo kama katika Agano la kale walivyosherekea sikukuu ya Mwandamo wa mwezi. Jambo hilo lilikuwa ni kivuli tu cha Sherehe ya sikukuu ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo, tunapoisherekea leo . HALELUYA !!
(5) Tunasherekea Krismas , kwa sababu Yesu Kristo alikuja ili tuwe na uzima tena tuwe nao tele.
Biblia inasema YOHANA 10:10:-" Mwivi (shetani) haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; Mimi Yesu nalikuja ili wawe na uzima tena wawe nao tele".
Kabla ya Yesu Kristo hajaja duniani kwa kuzaliwa kwake. Hapo mwanzoni shetani alituonea , alitutesa na kutuua bila kuwa na msaada wowote ule.
Lakini kwa kuja kwake Yesu Kristo duniani. Alikuja ili atuponye, atuokoe na kutuweka huru mbali na dhambi na vifungo vya shetani . Na kwa kila allitajaye jina la BWANA anaponywa na kuolokewa.
MATENDO 10:38:-" Habari za Yesu wa Nazaret, jinsi alivyomtia Mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu; naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na KUPONYA WOOTE WALIOONEWA NA IBILISI; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye ".
LUKA 9:1-2:-" Akawaita wale Thenashara, AKAWAPA UWEZO NA MAMLAKA juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, NA KUPONYA WAGONJWA".
[ LUKA 10::17-19 ]
Kama Yesu asingezaliwa dunia Leo . Maana yake ni kwamba uzima , uponyaji wala wokovu tusingeupata.
Lakini ashukuruliwe Mungu Baba kwa kuwa kwa kuzaliwa kwake Yesu Kristo ametupa uwezo na mamlaka, tena tumeponywa na kuweka huru mbali na vifungo vyote vya Ibliisi. Neno la Mungu linasema katika
WAKOLOSAI 1:12-14:-" Mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. Naye alituokoa katika nguvu za Giza , AKATUHAMISHA NA KUTUINGIZA KATIKA UFALME WA MWANA WA PENDO LAKE; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi".
(6) Tunasherea siku ya Krismas , kwa sababu kwa kuzaliwa kwake Yesu Kristo duniani. Ametufanya sisi mataifa mengine yoote nje na Israeli, ambao hapo mwanzo tulikuwa hatuna tumaini wala MUNGU duniani. Lakini kupitia kuja kwa Yesu Kristo duniani, tumehesabika pamoja na Israel kuwa sehemu ya urithi mmoja wa watoto wa Mungu.
Maana hapo mwanzo TAIFA LA MUNGU NA WATU WAKE YEHOVA WALIKUWA NI WA ISRAELI TU . Sisi mataifa mengine tulikuwa hatuna tumaini wala Mungu duniani. Maana yake Tulikuwa ni watu wa kufa tu na kwenda Motoni moja kwa moja.
kama Yesu Kristo asingezaliwa , sisi mataifa mengine nje na Israeli, tungebaki kuwa tumetengwa mbali na uso wa Mungu milele .
Lakini kwa kuja kwake Yesu Kristo duniani alipozaliwa. Tumepatanishwa sisi na Israel kuwa kitu kimoja , SISI SOTE NI WATOTO WA MUNGU. Hakuna cha myahudi wala myunani. Biblia inasema katika WAEFESO 2:11-21; WAGALATIA 3:26-29; 1 PETRO 2:5-10.
NB.
Kwa sababu hiyo . Hizo ndizo sababu kuu za msingi ki-biblia zinazotufanya WAKRISTO TUSHEREKEE CHRISTMAS.
Kuamua kusherekea Krismasi au kuacha kusherea yote mawili sio dhambi . kwa maana hakuna Andiko linalotukaza kutoshetekea Krismasi wala hakuna sheria ya Andiko linamlolazimisha mtu kusherekea Krismasi.
Kwahiyo kama utapenda basi sherekea kwa utukufu wa Mungu. Vema. Na kama wewe moyoni mwako kwako haupendi kusherekea Krismasi. Basi acha!
La msingi tusikwazane, tusinyosheane vidole wala kuhukumiaana kwa jambo hili la Christmas. Kila mmoja atumie Uhuru wa imani yake, maadamu kwa kufanya hivyo hatendi dhambi.
Biblia inasema katika WARUMI 14:10-13, 19:-" LAKINI WEWE JE! MBONA WANUHUKUMU NDUGU YAKO? Au WEWE JE MBONA WAMDHARAU NDUGU YAKO ? kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu . kwa kuwa imeandikwa , kama niishivyo asema Bwana, kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utamkiri Mungu. Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu. BASI TUSIZIDI KUHUKUMIANA, bali afadhali toeni hukumu, MTU ASITIE KITU CHA KUMKWAZA NDUGU AU CHA KUMWAGUSHA. Basi kama ni hivyo , na tufuate mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana".
La msingi tusihukumiane wala kukwazana kwa wewe unayependa kusherekea Christmas na kwa wewe ambaye husherekei. Bado wote tunabakia ni watoto wa Mungu na tunakwenda mbinguni.
Na la msingi kuliko yote tunaposherekea sikukuu ya Christmas. Ni YESU KRISTO AZALIWE UPYA NDANI YA MIOYO YETU. Tubadilike kitabia , kiusemi, kimavazi , kimwenendo na kufanyika kuwa viumbe vipya machoni pa Mungu wetu.
2 WAKORINTO 5:17:-" Hata imekuwa , MTU AKIWA NDANI YA KRISTO AMEKUWA KIUMBE KIPYA; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya".
Na Hakuna maana yoyote ya kusherekea Christmas hii kama bado wewe hujaokoka. MPE YESU MAISHA YAKO NDUGU YANGU , AKUOKOE . Maana neno la Mungu linasema
MATHAYO 1:21:-" Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, YEYE NDIYE ATAKAYEWAOKOA WATU WAKE NA DHAMBI ZAO".
Mungu awabariki wote kwa kila asomaje ujumbe wa Neno hili.
Nakutakia HERI YA KRISMASI NA MWAKA MPYA .
Ukipenda kuwasiliana nami kwa ushauri , maombezi na mafundisho zaidi ya masomo ya neno la Mungu. Karibu :-
Mtumishi wa Mungu aliye hai.
MWL, REV:-ODRICK BRYSON
SIMU:- 0759 386 988; 0717 591 466
Email:- Odrick16@gmail.com.
Whatsapp group.
"KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA"
[ 2 WAKORINTO 2:17 ]
Shalom,
By permission Rev Odrick Bryson
Max Shimba Ministries Org,

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW