Thursday, December 20, 2018

SHETANI NI NANI?


SHETANI NI NANI?
JE, SHETANI ALIUMBWA NA MWENYEZI MUNGU KAMA WANAVYO DAI WAISLAM?
Biblia humwita “mungu wa ulimwengu huu.” Lakini alitoka wapi? Je Mungu alimuumba kama alivyo? Je, yeye ni roho aliyeanguka? Haya hapa ni majibu kutoka katika Neno la Mungu!
Biblia inamfafanua Shetani kuwa kiumbe halisi ambaye yuko katika makao ya roho. (Ayubu 1:6) Inatueleza kuhusu sifa zake za ukatili kutia ndani matendo yake ya uovu. (Ayubu 1:13-19; 2:7, 8; 2 Timotheo 2:26)
Asili ya Shetani ni wapi au nini?
Tangu mwanzo Shetani hakuwa anaitwa Shetani, yaani hapakuapo na kiumbe kilichoumbwa na kuitwa Shetani. Alikuwa ni “mwana wa asubuhi” (Isa.14:12) yeye pamoja na jeshi lingine la mbinguni,waliumbwa wote wakiwa wakamilifu katika njia zao zote ( Ezekieli. 28:14-19). Kulikuwa na amani na umoja Mbinguni. Kisha mambo yakaharibika. Biblia haiko wazi sana juu ya swala hili ni nini hasa kulitokea na kwa namna gani, ila uovu au kutokumtii Mungu kulioneka kwa Lucifa. Mwishowe alifukuzwa kutoka Mbingini, pamoja na jeshi lake lote lililoasi, wakafukuziwa mbali kabisa kutoka mbinguni na kutupwa, na wanazunguka zunguka katika nchi (duniani).
(Wakolosai 1:15) Mungu aliumba malaika. (Ayubu 38:4-7) Wote walikuwa wakamilifu na waadilifu. Hata hivyo, mmoja kati ya malaika hao aliitwa Lusifa ndie akaja kuwa Shetani.
Malaika huyo hakuitwa Shetani alipoumbwa. Jina hilo ni la kumfafanua, na linamaanisha “Mpinzani; Adui; Mshtaki.” Alikuja kuitwa Shetani kwa sababu alichagua kumpinga Mungu. Ni sawa na kusema, Mungu hakuumba majambazi, bali Majambazi ni sifa ambayo mtu anaipata anapo fanya unyang'anyi kwa kutumia nguvu. Mungu wetu hakuumba uovu.
Kiumbe huyo wa roho akaanza kukuza hisia za kiburi na za kushindana na Mungu. Alitaka wengine wamwabudu yeye. Yesu alipokuwa hapa duniani, Shetani alimtaka Yesu ‘amfanyie tendo la ibada.’—Mathayo 4:9.
Shetani alitupwa na malaika wake?
Ufunuo 12: 7-21 Imeandikwa “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; 8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. 9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. 10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya MwanaKondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. 12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.
Ufunuo 12 husema juu ya Shetani na pepo wake wabaya “walitupwa katika nchi” (fu. 13). Kwa hakika sura hii imepachikwa katikati ya kitabu cha Ufunuo, na ni muhtasari mfupi wa historia ya Kanisa la Agano Jipya.
Fungu la 3 linamwelezea Shetani kama “joka” aliye “kokota theluthi ya nyota za mbinguni na kuziangusha katika nchi” (fu. 4). Kumbuka kwamba “nyota” hizi zilikuwa ni theluthi ya malaika wote waliokuwa chini ya Nyota ya alfajiri kabla hajaasi.
2 Petro 2:4 hutoa kiashiria kingine juu ya huku “kutupwa chini” kwa Shetani na malaika zake “aliowakokota pamoja” naye. Angalia: “Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa [Shetani hakuwa malaika pekee aliyeasi], bali aliwatupa shimoni.” (Neno la Kigiriki hapa ni tartaros na linamaanisha aidha “gerezani” ama “kizuizini”—hii ni dunia yenyewe.) Pepo hawa wabaya pamoja na Shetani “wanalindwa hata ije hukumu,” wakiisha “kutiwa…katika vifungo vya giza.” Hii inafunua kwamba Mungu aliwatia katika gereza hili la giza pepo wengine wengi walioanguka waungane na “mkuu wa giza.”
Ufunuo 12:7-9 hueleza, kwa undani, lini Shetani na pepo wake wabaya watatupwa hata nchi kwa mara ya mwisho wasipate tena kibali cha kuingia mbinguni. Mafungu ya 12-14 yanaonyesha kwamba mwitikio wa ibilisi ni hasira kuu. Wakati huu wa kutisha unakuja kwa ulimwengu mzima hapo mbeleni kidogo!
Shetani anatushawishi vipi?:
Asili ya shetani ni roho mchafu. sio kitu kinachoweza kuonekana, lakini ni kitu ambacho tunaweza kukifahamu kwa kusoma Biblia. Biblia ilitolewa kama Neno la Mungu. Yesu Kristo alikuja kwetu kama mfano hai wa Neno la Mungu. Ni katika kusoma Biblia tu, ndipo tunaweza kutambua mazuri na mabaya, kujua juu ya utauwa, au kutambua haki na imani ya kweli, na yapi yaliyo ya shetani. Na ni nini yaliyo Mapenzi ya Mungu. Sio jambo tunaloweza kulifahamu tangu kuzaliwa au ambalo tukiwa tunazaliwa tunakuwa tunalifahamu.Wengi kati yetu tunafanya uchaguzi mbaya kwa sababu hatusomi Biblia na kulifuata Neno la Mungu, sawa sawa na Mapenzi ya Mungu.
Shetani ni roho mchafu na anatushawishi kiroho, njia moja ya kumuona shetani ni katika mawazo yetu, akilini mwetu. Tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu. Shetani sio kitu kilichoandikwa, sio kitu tunachoweza kukiona kwa macho, kukisikia, kugusa, kuonja au kunusa. Mungu ni kama hivyo kwa namna fulani na malaika wote na hata shetani pia.
Waefeso. 2:2 Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumufuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi.
Mwisho wa Shetani ni wapi?
Ufunuo 20:2 Akamshika yule joka, yule joka wa zamani, ambaye ni ibilisi na shetani, akamfunga miaka elfu.
Shetani atafungwa na hataweza kumshawishi mtu tena mwanadamu yeyote kwa muda miaka elfu moja kisha atafunguliwa tena (Ufunuo 20:7) mwisho wa hiyo miaka elfu moja. Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, shetani atafunguliwa, atoke kifungoni kwake; na kutambua ya kwamba ameshidwa; ni mnyonge hawezi kupata nguvu pasipo Mungu, na kuna vita vingine tena vitakavyotokea dhidi ya Mungu kama shetani atakavyowadanganya nakuwashawishi watu tena kama anavyofanya wakati huu wa sasa
Shetani anatupwa katika shimo (Isaya 14:15-17). Na wale wanaomwona washangaa na kustajabu ya kwamba huyu ndiye yule aliyeleta matatizo yote ya duniani na huzuni na masikitiko yote. Ghafla anabadilika na kutokuwa tena yule mnyama wa roho chafu ya kutisha na ya kuogofya ambaye hapo mwanzo alikuwa ni wa kuogofya na wa kutisha, aliyeweza kusababisha watu waamini ya kuwa ndivyo alivyo. Yeye ni mhongo aliyouadhibu uumbaji wa Mungu uliyofundishwa kumkili Mungu katika nguvu zake ambaye Yeye ni Mweza.
Ufunuo 20:10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.
Hata hivyo shetani atatambua ya kuwa Mungu alikuwa ni wa haki wakati wote. Hili neno “shetani” maana yake ni mshitaki. Shetani ataacha kuwa mshitaki, hatakuwa shetani tena. Hatawashitaki tena ndugu, kama alivyowashuhudia kwa uongo. Mashitaka yamekwisha lakini yatakuwepo daima kama kumbukumbu. Adhabu gaini kwa shetani ! Mashitaka yake hayatasahaulika. Yatakumbukwa daima kama aliyemvunjia Mungu heshima, na kwa kuudan ganya ulimwengu. Atapata mateso yake kwa sababu atatambua makosa yake. Msamaha wetu ni muhimu sana katika kurudisha utukufu na heshima yake na katika maisha mema.
Mwishowe, kila mtu atamtambua Kristo kuwa ni Mfalme na Kuhani Mkuu anayeunganisha dunia yote na kumwakilisha Mungu. Jambo hili litakapokamilika vita kati ya mema na mabaya vitakuwa vimekwisha. Ushawishi wa shetani utakuwa umekwisha. Mauti yamekwisha. Makanisa ya uongo na manabii wa uongo na unabii wa uongo utakuwa umekwisha. Yote yatakuwa yamekwisha; wote watatambua Mpango wa Mungu na watakuwa sehemu ya Familia ya Mungu. Wote watakiri ya kwamba Mungu alijua yote, na anajua yote, na daima atajua yote.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13
Image may contain: 1 person, text

1 comment:

Limba Willy said...

Ubarikiwe sana ndugu yangu.

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW