Friday, December 7, 2018

YEHOVA NI NANI?

Image may contain: night
Katika Biblia Takatifu, Mungu anasema: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.” (Isaya 42:8) Ingawa ana majina mengi ya cheo kama vile “Mungu Mweza-Yote,” “Bwana Mwenye Enzi Kuu,” na “Muumba,” anawaheshimu waabudu wake kwa kuwaalika wamwite kwa jina lake la kibinafsi.—Mwanzo 17:1; Matendo 4:24; 1 Petro 4:19.
Biblia inamtaja Yehova kuwa Mungu wa Kweli, Muumba wa kila kitu. (Ufunuo 4:11) Manabii kama Abrahamu na Musa walimtumikia. (Mwanzo 24:27; Kutoka 15:1, 2; Yohana 20:17) Yeye si Mungu wa watu fulani pekee, bali wa “dunia yote.”—Zaburi 47:2.
YHWH / YAHWEH / YEHOVA: "BWANA" (Kumbukumbu la Torati 6: 4; Danieli 9:14) — kwa kusema, jina pekee la Mungu. Ilitafsiriwa katika maandiko ya Kiingereza "BWANA" (miji yote) ili kuitenganisha kutoka Adonai, "Bwana." Ufunuo wa jina hulitolewa kwanza kwa Musa "MIMI NIKO AMBAYE NIKO" (Kutoka 3:14). Jina hili linafafanua haraka, uwepo. Yahweh yupo, anaweza kupatikana, karibu na wale wanaomwita kwa ajili ya ukombozi (Zaburi 107: 13), msamaha (Zaburi 25:11) na mwongozo (Zaburi 31: 3).
Kama inavyoonyeshwa katika Biblia, Yehova ni jina la pekee la Mungu. (Kutoka 3:15; Zaburi 83:18) Linatokana na kitenzi cha Kiebrania kinachomaanisha “kuwa,” na wasomi wengi wanaona kwamba jina hilo linamaanisha “Husababisha Iwe.” Maana hii inapatana kabisa na cheo chake akiwa Muumba na Mtimizaji wa makusudi. (Isaya 55:10, 11) Biblia inatusaidia pia kuelewa utu wa Yehova, hasa sifa yake kuu ya upendo.—Kutoka 34:5-7; Luka 6:35; 1 Yohana 4:8.
Jina Yehova limetafsiriwa kutoka kwa jina la Mungu katika lugha ya Kiebrania lenye herufi nne za Tetragramatoni יהוה (YHWH).
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW