Thursday, September 13, 2018

ETI NYOTA ZINAREJEA NA KUJIFICHA AU NI UKOSEFU WA ELIMU KWA ALLAH NA MOHAMMAD WAKE?

ETI NYOTA ZINAREJEA NA KUJIFICHA AU NI UKOSEFU WA ELIMU KWA ALLAH NA MOHAMMAD WAKE?
Image may contain: night and text
Tuanze na aya:

Quran 81:15. Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma, ***16. Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

Nyota ni nini?

Nyota ni kama jua letu, lakini ziko mbali sana. Nyota ziko mbali kiasi gani. Mwanga unasafiri kwa kasi (speed) ya 299,793 km/sekunde au 1,079 milioni km/saa. Mara nyingi umbali wa nyota hupimwa kwa muda utakaotumiwa na mwanga kusafiri mpaka kutufikia sisi. Kwa mfano, mwanga kutoka jua letu unasafiri kwa takriban dakika 8 hivi kutufikia sisi kutoka hapa duniani).

Nyota iliyo karibu sana na sisi ni ile iitwayo alpha-Centauri (kwenye constellation ya Centaurus) ambayo iko umbali wa 4.4 light-years kutoka hapa (mwanga kutoka alpha-centauri huchukua miaka 4.4 kutufikia) ndio maana nyota zinaonekana ndogo sana ukifananisha na nyota yetu (jua) hapa duniani. Jua letu ni moja ya nyota ndogo sana. Kuna mizinga ya nyota kama. Betelgeuse (kwenye Constellation ya Orion) ambayo ina ukubwa wa majua yetu 1,000 na iko umbali wa 643 light-years kutoka hapa.Chanzo cha mwanga wa nyota.

Nyota zote (pamoja na jua letu) zinatoa mwanga, joto, na nishati nyingine kutokana na nguvu za nyuklia aina ya fusion inachukua atom mbili za hewa ya hydrogen na kuziunganisha ili kutengeneza atom moja ya hewa ya Helium. Uzito wa zile atom mbili za hydrogen ni mkubwa kuliko uzito wa atom ya helium iliyotengenezwa.

Nyota kwa mang'amuzi na lugha ya kawaida ni nuru ndogo zinazoonekana angani wakati wa usiku. Lakini Allah anadai eti Nyota zinarejea, sijui kutoka wapi na vile vile anadai eti Nyota zinajificha. Huu kama si Msiba ni nini ndugu zangu?

1. Nyota zinarejea nyuma kutokea wapi?
2. Nyota "ZINAZO KWENDA" zinaelekea wapi?
3. Nyota zinajificha wapi?

Ninapo sema kila siku kuwa Allah ni bandia huwa sibahatishi.

Shalom

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW