Wednesday, August 10, 2016

UTATA NDANI YA KORAN JE, INJIL ILIKUWEPO WAKATI WA MUSA


Ndugu zanguni,
Leo nitazungumzia makosa na utata ndani ya Koran. Katika somo letu la leo, mtaona utata na makosa kutoka kwa Allah, alipo kuwa anamjibu Musa maombi yake. Allah anamjibu Musa na kumweleza kuwa eti Nabii asiye fahamu kusoma na kuandika yupo ndani ya Injili, huku ikifaamika kuwa Injili ilikuwa bado haikushushwa. Sasa Musa alijuaje Injil na huku ilikuwa bado haijateremshwa na Allah, kama ambavyo Quran inasema? Injili iliteremshwa miaka 1653 baada ya kuzaliwa Musa. Musa alizaliwa 1593 B.C na kufariki akiwa na miaka 120. Hivyo basi Musa alikufa 1473 B.C Soma Kumbukumbu ya Torati 34:5-7.
Aya nyingi katika Qur'ani zipo wazi kwamba Injil ilitolewa kwa Yesu ambaye alizaliwa miaka mia kadhaa [1473] baada ya Musa.
Lakini cha kushangza, eti Musa aliye ishi miaka 1473 kabla ya YESU kuzaliwa na yeye anajibiwa na Allah kuhusu Injili ya Yesu kama vile yeye Musa alizaliwa baada ya Yesu. Soma majibu ya Allah kwa Musa hapa chini.
Quran 7: 155. Na Musa akawateuwa watu sabiini katika kaumu yake kwa miadi yetu. Na ulipo fika mtetemeko mkubwa alisema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ungeli taka ungeli wahiliki wao na mimi zamani! Unatuhiliki kwa waliyo yafanya wajinga katika sisi? Haya si chochote ila ni mtihani wako, umpoteze umtakaye na umhidi umtakaye. Wewe ndiye Rafiki Mlinzi wetu. Basi tughufirie na uturehemu. Na Wewe ndiye mbora wa kughufiria. ***
156. Na utuandikie mema katika dunia hii na katika Akhera. Sisi tumerejea kwako. (Mwenyezi Mungu) akasema: Adhabu yangu nitamsibu nayo nimtakaye. Na rehema yangu imeenea kila kitu. Lakini nitawaandikia khasa wanao mchamngu, na wanao toa Zaka, na wale ambao wanaziamini Ishara zetu, ***
157. Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii, asiye soma wala kuandika, wanaye mkuta kaandikwa kwao katika Taurati na Injili, anaye waamrisha mema na anawakanya maovu, na anawahalalishia vizuri, na ana waharimishia viovu, na anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyo kuwa juu yao. Basi wale walio muamini yeye, na wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyo teremshwa pamoja naye - hao ndio wenye kufanikiwa. ***
Koran imejaa mashaka kila sehemu. Leo tunaona Allah anamjimu Musa kuhusu Injili ambayo ilishushwa miaka 1653 baada ya kifo cha Musa. Hivi huyu Allah alipitiwa na kuanza kuzumguzia Isa Bin Maryama kwa Musa au ni kufichuka kwa siri kwamba Quran si kitabu cha Mungu? Au labda Isa Bin Maryam alikuwa teyari anaishi sehemu fulani "pre existence"
Kama kweli Allah ni Mungu, kwanini afanye makosa makubwa namna hii?
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
For Max Shimba Ministries Org
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW