Wednesday, August 10, 2016

KAMA YESU NI MUNGU, ALIKUWA ANAMWOMBA NANI?


Hili ni moja ya Swali linalo ulizwa sana na Waislam na dini zinazo pinga uungu wa Yesu.
Kama Yesu alikuwa Mungu , ni jinsi gani aliomba kwa Mungu?
Je! Yesu alikuwa akijiomba mwenyewe?"
YESU ALIKUWEPO TOKEA MILELE YOTE
Ili umwuelewe Yesu kama Mungu duniani akiomba kwa Baba yake mbinguni , tunahitaji kutambua kwamba Baba wa milele na Mwana wa milele walikuwa na uhusiano wa milele kabla ya Yesu kuuchukua mwili wa mwanadamu. Tafadhali soma Yohana 5:19-27, hasa mstari wa 23 ambapo Yesu anafundisha kwamba Baba alimtuma Mwana (pia tazama Yohana 15:10). Yesu hakuwa Mwana wa Mungu wakati Yeye alizaliwa katika Bethlehemu. Yeye daima amekuwa Mwana wa Mungu kutoka milele iliyopita, bado ni Mwana wa Mungu, na daima atakuwa.
ISAYA ANAKUJIBU
Isaya 9:6 inatuambia kwamba Mwana alipeanwa na mtoto alizaliwa. Yesu alikuwa daima sehemu ya utatu, pamoja na Roho Mtakatifu. Utatu ulikuwa kila mara, kama, Mungu Baba , Mungu Mwana, na Mungu Roho, si miungu mitatu, lakini Mungu ni mmoja anajidhihirisha kama watu watatu. Yesu alifundisha kwamba Yeye na Baba yake ni kitu kimoja (Yohana 10:30), kumaanisha kwamba Yeye na Baba yake ni wa kiini kimoja na asili moja. Baba, Mwana na Roho ni watu watatu walio na ushirikiano sawa wakiwepo kama Mungu. Hawa watatu walikuwa, na wataendelea kuwa na uhusiano wa milele.
YESU NI MWANA WA MILELE
Wakati Yesu, Mwana wa milele wa Mungu, aliuchukua ule mwili wa mwanadamu usio na dhambi Yeye pia alichukua namna ya mtumwa, kupeana utukufu wake wa mbinguni (Wafilipi 2:5-11). Kama Mungu -mwanadamu, alikua na kujifunza utiifu (Waebrania 5:8) kwa Baba yake hasa wakati wa kujaribiwa na Shetani, mshitakiwa uongo na wanadamu, kukataliwa na watu wake, na hatimaye alisulubiwa. Kuomba kwa Baba yake mbinguni kulikuwa kwa kumwomba nguvu (Yohana 11:41-42) na hekima (Marko 1:35, 6:46). Kuomba kwake kulionyesha utegemezi wake kwa Baba yake katika ubinadamu wake ili atekeleze mpango wa ukombozi wa Baba yake, kama ilivyoshuhudiwa katika Sala ukuhani mkuu ya Kristo katika Yohana 17. Kuomba kwake kulionyesha kwamba Yeye hatimaye alijisalimisha kwa mapenzi ya Baba yake, ambayo ilikuwa kwenda msalabani kulipa adhabu (kifo) kwa kuvunja kwetu sheria Mungu (Mathayo 26:31-46). Bila shaka, Alifufuka katika mwili kutoka kaburini, akishinda msamaha na uzima wa milele kwa wale ambao watatubu dhambi zao na kumwamini kama Mwokozi.
HAKUNA TATIZO KWA UNGU KUWA NA MWANA

Hakuna tatizo kwa Mungu Mwana kuomba au kuzungumza na Mungu Baba. Kama ilivyotajwa, walikuwa na uhusiano wa milele kabla ya Kristo awe mwadamu. Uhusiano huu ni taswira katika Injili ili tuweze kuona ni jinsi gani Mwana wa Mungu katika ubinadamu wake ulitekeleza mapenzi ya Baba yake, na katika kufanya hivyo, kulinunua ukombozi kwa ajili ya watoto wake (Yohana 6:38). Kwa kuendelea kujiwasilisha kwa Baba yake mbinguni Kristo daima aliwezeshwa na kutiwa nguvu na akabaki kuwa na lengo katika maisha yake ya maombi. Mfano wa Kristo wa maombi ni wetu kuufuata.
YESU KRISTO HAKUWA CHINI YA MUNGU
Yesu Kristo hakuwa chini ya Mungu duniani wakati anaomba kwa Baba yake mbinguni. Alikuwa anaonyesha jinsi hata katika ubinadamu wa dhambi ni muhimu na maisha ya maombi ili kufanya mapenzi ya Baba yake. Kuomba kwa Yesu kwa Babaye kulionyesha mfano wa uhusiano ulioko katika Utatu wake na mfano kwetu sisi, kwamba ni lazima tumtegemee Mungu kwa nguvu na hekima tunahitaji kwa njia ya maombi. Tangu Kristo, kama Mungu -mwanadamu, alihitaji kuwa na maisha mahiri ya maombi, hivyo ndivyo inavyowapasa wafuasi wa Kristo hii leo.
YESU NI MUNGU

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW