Friday, August 26, 2016

YESU ANAWAPENDA SANA WATOTO WADOGO


Nyakati nyingine pia, Yesu anaonyesha namna anavyopenda sana watoto wadogo. Miezi michache baadaye watu fulani wanaleta watoto wamwone Yesu. Mitume wanajaribu kuwazuia. Lakini Yesu anawaambia mitume wake hivi: ‘Acheni watoto waje kwangu, msiwazuie, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wa watu kama hao.’ Ndipo Yesu anachukua watoto mikononi mwake, anawabariki. Ni vizuri kujua kwamba Yesu anawapenda watoto wadogo.
Mathayo 18:1-4; 19:13-15; Marko 9:33-37; 10:13-16.

No comments:

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW