Monday, January 16, 2017

UTATA NDANI YA QURAN. "AYA ZA QURAN ZAPINGANA"

No automatic alt text available.


HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM:
Sura Al-Baqara 2:109
Wengi wa watu wa kitabu, kutokana na wivu wao, wanatamani kuwarudisheni kwenye kutoamini baada ya kuwa mmeamini, pamoja na kwamba ukweli umeshadhihirishwa wazi mbele yao. Kwa hiyo wasameheni na kuwavumilia hadi Allah atakapowafunulia mapenzi yake. Yeye ana nguvu juu ya kila kitu.
Quran pia inawaagiza Waislamu katika Sura Al Imran 3:20 kwamba:
... if they give no heed, then your only duty is to warn them.
Yaani:
... kama wasipowasikiliza, basi ninyi kazi yenu pekee ni kuwaonya tu.
Kwa hiyo, kutokana na aya hizi mbili, yaani Al-Baqara 2:109 na Al Imran 3:20, tunaona mambo yafuatayo:
1. Ni wajibu wa Waislamu kuhubiri dini yao lakini si wajibu wao kuwalazimisha watu kuamini dini yao.
2. Allah kwa wakati wake atawafunulia wale wasioamini ukweli wa mambo.
3. Ni wajibu wa Waislamu kutoa maonyo tu kwa wale wanaowahubiria.
LAKINI, HEBU TAZAMA AYA ZIFUATAZO UONE KIZUNGUMKUTI KWENYE HII DINI YA KUTENGENEZA:
Al-Nisa 4:101
Wale wasioamini ni maadui zenu wakubwa.
Vilevile inasema katika sura Al-Tawba 9:3
Tangazeni mapigo makuu (ya ole) kwa wasioamini.
Pia quran inasema katika sura Al-Anfal 8:39
Fanyeni vita juu yao hadi kusiwepo na mateso tena na hadi pale dini ya Allah itakapokuwa imetawala.
MASWALI WANAYO YAKIMBIA WAISLAM:
1. Je, aliyempa Muhammad maneno ya Quran 2:109, Quran 3:20 na yale ya Quran 4:101, 9:3, 8:39 ni huyo huyo au ni wawili tofauti?
2. Iweje aseme kuwa usiwalazimishe watu kuamini bali waonyeni na kuwavumilia tu, kisha anageuka sehemu nyingine na kusema walazimisheni, tena kwa vita?
3. Je, hii si ishara ya tabia ya usahaulifu ambayo si tabia ya Mungu bali ni ya mwanadamu?
4. Kama ni huyo huyo, je, aya hizi zinafanana au zinapingana?
5. Kama zinafanana, ni kwa vipi?
6. Kama zinapingana, huu si ushahidi tayari kuwa quran haitoki kwa Mungu wa kweli kama ambavyo quran yenyewe imeweka kigezo cha kujua hilo? Maana Mungu wa kweli hawezi hata kidogo kusahau jambo alilolisema kabla halafu aje aseme kitu tofauti. Ni viumbe tu ndio wanaweza kusahau na kukosea.
Hakika Quran si kitabu cha Mungu. Waislam nawakaribisha kwa Mungu wa Biblia ambaye alimtuma Mwanawe kuja Duniani kwa ajili ya dhambi zetu.
Karibuni kwa Yesu.
Mungu awabariki sana,
Max Shimba Minsitries Org.

1 comment:

Unknown said...

Max Simba wakati WA utapeli umeisha watu wanauamini uislam Kwa elimu ya KWELI ww Baki na propaganda za kulazimisha kupindisha ukweli ushauri wa Bure qur an inataka uwe na elimu ya uelewa wa ubongo kwanza pili mpenda mungu tatu mpenda haki nne mchukia uwongo ndyo utaongozwa na qur an vingi dvyo endelea kutapeli waliojitungia dini ya kuchumia kipato kama wewe ila ukifa motoni na kizuri Zaid hata ww unajua ukifa ni jahannam kwahyo Haina shida na pole Kwa kushikwa na pepo la kuipenda Dunia Kwa kudhurumu waumini wako

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW