Monday, January 16, 2017

ALLAH HAJUI SAYANSI YA DARASA LA TANO

Image may contain: 3 people, text
Ili kumpima Allah kama kweli aliumba kila kitu, leo tutamia Sayansi na tuone kama atapasi "Litmus Test". Maana ni rahisi sana kujua kama Uislam ni dini ya Mwenyezi Mungu au ulitengenezwa tu na Muhammad.
SOMA:
Surat Al Kahf 18:86 inasema kuwa jua huzama kwenye chemchemi ya maji yenye tope.
Unadhani hii ni sahihi. Jua lina joto la zaidi ya nyuzijoto 6000 kwenye uso wake. Lakini maji yakifika nyuzijoto 100 yanageuka mvuke. Je, maji yanayotajwa kwenye surat Al Kahf ni maji gani? Unadhani ni Mungu aliyeumba jua na maji ndiye anayesema haya?http://www.quranitukufu.net/018.html
SASA MUHAMMAD NA YEYE ANASEMA KUWA JUA LINAZAMA KWENYE CHEMCHEM YA MATOPE
Dhu al-Qarnaiyn [Zul Qarnain] "alishuhudia kuzama kwa jua kwenye sehemu yake ya kupumzikia kwenye bwawa lenye ute mweusi na wenye harufu mbaya sana." al-Tabari juzuu ya 5 uk.173-174 (Tazama Sura 18:82-97).
Katika Al Tabari hapo juu tumesoma kuwa jua hupumzika kwenye bwawa lenye ute mweusi. Unadhani hii ni sahihi. Jua lina joto la zaidi ya nyuzijoto 6000 kwenye uso wake. Lakini maji yakifika nyuzijoto 100 yanageuka mvuke. Je, maji yanayotajwa na Muhamamd kwenye hadith hii ni maji gani? Unadhani ni Mtume wa Mwenyezi Mungu aliyeumba jua na maji ndiye anayesema haya?
MUHAMMAD ANASEMA KUWA ETI JUA LINAPOROMOKA TOKA KITI CHA ENZI MPAKA KWENYE BAHARI.
" [Muhammad] Aliendelea. Wakati jua linachomoza, linainuka juu ya kibandawazi (kinachokokotwa na farasi) toka kwenye moja ya chemchemi hizo likiwa pamoja na malaika 360 …. Wakati Mungu anataka kuvijaribu jua na mwezi, ili kuwaonyesha watumishi wake ishara na kwa njia hiyo kuwataka waache kutokumtii Yeye na kuanza kutii, jua huporomoka ghafla toka kwenye kibandawazi na kuanguka kwenye kina cha bahari, ambacho ni cha mduara.
Wakati Mungu anataka kuongeza umuhimu wa ishara kuwatisha zaidi watumishi wake, jua lote hunguka, na hapawi na sehemu yake yoyote inayobaki kwenye kibandawazi. Huko ndiko kupatwa kukamilifu kwa jua, wakati ambapo mchana hujiwa na giza na nyota hutokeza." al-Tabari juzuu ya1 uk.236.
Tunaendela na kumuumbua Allah na Muhammad: Kwenye hadith hapo juu, Muhammad anasema kuwa Jua linakokotwa na Farasi.
(i) Jua lina kipenyo cha (radius of the sun is) 432,450 miles (696,000 kilometers) na ukubwa wa 1.4 x 1027 cubic meters. Ikimaanisha kuwa ni sawa na dunia milioni moja na nukta tatu (About 1.3 million Earths could fit inside the sun.). Uzito wa jua ni sawa 1.989 x 10 kipeo cha 30. [Nisawa na uzito wa dunia mara 333,000]
(ii)Lakini Allah anadai eti hilo Jua lenye huo uzito na huo ukubwa linabebwa na farasi. Zaidi ya hapo, joto la jua peke yake litawaunguza hao Farasi na kuwa masizi.
(iii) Allah anaendelea kudai kuwa Jua hilo lina anguka kwenye kina cha Bahari. Hivi jua lenye ukubwa mara milioni moja nukta tatu zaidi ya dunia, linawezaje kuingia kwenye kina cha bahari ambayo ni sehemu tu ya dunia?
Ndugu msomaji, je, wewe bado unaendelea kumfuata huyu Allah amabye hajui hata sayansi ya kawaida tu?
Muislam anasema eti, Allah kaumba kila kitu, huku akishindwa vibaya sana sayansi ya kawaida tu, tena ya darasa la Tano.
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAMU NA MUHAMMAD WAO.
ALLAH HAJUI SAYANSI NA HIVYO BASI HAWEZI KUWA MWENYEZI MUNGU ALIYE UMBA KILA KITU.
NDIO MAANA HUWA NASEMA, UISLAM NI DINI YA KUTENGENEZA TU NA HAUKUWEPO KABALA YA KUZALIWA MAREHEMU MUHAMMAD.
Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo.
Max Shimba Ministries Org.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW