Wednesday, July 19, 2017

ALLAH NA MUHAMMAD WANADAI KUWA NYOTA NI MAKOMBORA YA KUPAMBANA NA SHETANI

Image may contain: text

Madhumuni ya Nyota na Vimondo kutokana na Uislam:
"Mbingu za chini kabisa zina taa [nyota], na ‘Tumeziumba (taa) hizi kama makombora ya kuwafukuzia waovu, na tumetayarisha Adhabu ya Moto Uwakao kwa ajili yao.’" Sura 67:5.
"Kuumbwa kwa nyota hizi kuna madhumuni matatu, yaani, kulipamba anga, makombora ya kuyapiga mashetani, na alama za kuwaongoza wasafiri. Kwa hiyo kama mtu yoyote anajaribu kupata tafsiri nyingine amekosea na anapoteza nguvu zake tu..." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 3 kabla na.421, uk.282.
Wakati mwingine vimondo hurushwa kwa mashetani ambao wanajaribu kusikiliza siri za mbinguni. Sahih Muslim juzuu ya 1 kitabu cha 4 na.902 na rejeo la 674 chini ya uk.243.
Vimondo vinapaswa kuwapiga malaika [wabaya] kabla hawajaeneza mambo waliyoyasikia. Wakati mwingine malaika wabaya huwaambia watabiri kabla ya kuwapiga. Ibn-i-Majah juzuu ya 1 kitabu cha 1 na.194, uk.110.
Vimondo huyashambulia majini (genies) Sahih Muslim juzuu ya 4 kitabu cha 24 na.5538, uk.1210.
Nyota hulinda dhidi ya shetani. al-Tabari juzuu ya 1, uk.223.
LAKINI YEHOVA ANASEMA NINI KUHUSU SHETANI NA MAJINI?
MAMLAKA YA KUTOA PEPO UMEPEWA NA YESU
Marko 16:17-18 inasema, "ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina Langu watatoa pepo...."
Kila Mkristo anao uwezo wa kuwatoa pepo! Sio swala la kwamba "una nguvu" kiasi gani au jinsi gani upo "kiroho" ; cha muhimu ni kuwa Yesu Amekupa mamlaka Yake; unatembea katika jina Lake.
Shetani hana haki ya kuendesha mambo katika maisha yako, au nyumbani mwako au katika maisha ya wale uwapendao. Tumia mamlaka yako katika Kristo dhidi yake.
MNAONA TOFAUTI YA ALLAH NA YEHOVA?
1. Allah anakimbiza mapepo kwa kutumia Vimondo na Nyota.
2. Wakristo tunakemea mapepo kwa jina la Yesu.
SASA KATI YA ALLAH NA YEHOVA NI YUPI UTAMFUATA?
Kumbe jina la Allah ni dhaifu na halina uwezo wa kutoa, au kimbiza au fukuza Mapepo au Mashetani au Shetani.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW