Thursday, July 27, 2017

JE’ BWANA YESU ANAPATAJE KUWA MUNGU? SEHEMU YA KWANZA

Image may contain: one or more people, ocean and text

Baada ya kujipatia maarifa makini juu ya nafsi tatu Mungu mmoja;
Ni vyema sasa tukapiga hatua nyingine ya ufahamu kwa kuangalia swali hili makini ambalo kwa kiasi kikubwa pia huchanganya hisia za watu wengi katika ulimwengu wa imani, ambapo kile kinachoonekana kuwachanganya watu wengi hapa ni uelewa juu ya ukweli kuhusu chimbuko la Uungu wa Bwana Yesu na hivyo watu wengi kuhoji kuwa Yesu anapataje sasa kuwa Mungu?.
Ni wazi kuwa swali hili hasa hulenga kutafut kujua asili au chimbuko la mamlaka ya Kiuungu ya Yesu anayotajwa kuwa nayo hasa kutokana na kile kinachoonekana kuwa Bwana Yesu alikuwa na mwonekano unaoonyesha kuwa huenda naye alikuwa na asili au chimbuko la dunia hii.
Hivyo ili kupata majibu ya msingi ya hili ni vyema kwanza tuanze na hoja juu ya asili ya Yesu na ndipo tunaweza kufunguka zaidi kiufahamu na kuelewa mengi zaidi juu ukweli kuhusu Uungu wa Yesu.
Ufahamu juu ya asili ya Yesu
Kile kilichoongeza upinzani mkubwa wa Mafarisayo na baadhi ya Wayahudi juu ya Uungu wa Yesu ni uelewa usiyo sahihi juu ya asili ya Yesu.
Ufahamu wa wengi kati ya Wayahudi uligotea katika dhana ya mwonekano wa ubinadamu wa Yesu na historia yake ya uzazi wa kidunia toka katika tumbo la Mariam, ambapo kama matokeo ya hili Wayahudi walisikika wakati fulani wakitamka:-
Yahana 6:42
Wakasema, Je! Huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?
Unaweza sasa kupata pichani juu ya mzizi wa hoja hii, na ni kama tunavyoona katika nukuu hiyo ya kitabu cha Yohana kuwa hoja kuu ya Wayahudi ilikuwa ni kile walichoona kuwa haikuwa sahihi kwa Yesu kusema ameshuka toka mbinguni maana kile wao wanachojua ni kuwa alizaliwa na bi’Mariam na baba yake ni Yusufu kwahivyo asili yake ni duniani tu.
Hivyo kwa hali hiyo iliwapa ugumu kukubali pale Yesu alipojitaja kuwa na asili ya mbinguni na kimsingi ndicho kilichokuwa chanzo kikubwa cha upinzani wao dhidi ya matamko ya Yesu.
Habu ona tena hoja ya Wayahudi pale Yesu alipoeleza uwepo wake wa milele’
Yohana 8: 56-58
Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Katika andiko hilo tena Wayahudi walipingana na Yesu kutokana na tamko lake lililoonyesha uhusiano wake na ukaribu na mzee Ibrahimu, kitendo ambacho kilifanya Wayahudi hao kumhoji kwa madai kuwa yeye ni kijana mdogo hasiyepata hata miaka hamsini anawezaje kuwa amemwona Ibrahimu?, na ndipo Yesu anajibu na kuwaambia bayana kuwa uwepo wake ni wa kabla ya Ibrahimu’ 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Hivyo kwa mtazamo wangu binafsi ninaona kuwa tatizo la Wayahudi au wale wanaopinga Uungu wa Yesu kwasababu ya ubinadamu alokuwa nao au sababu ya kuzaliwa na Mariam tatizo lao kuu si hilo bali zaidi ni kutolewa kabisa msingi mzima wa asili ya Yesu kabla ya kuzaliwa kwake na Mariam.
Je’ Asili ya Yesu ni wapi?
Katika kujibu swali hili Bwana Yesu mwenyewe mara kadhaa aliwaelimisha Wayahudi juu ya ukweli kuhusu asili yake ili kuwasaidia kuondokana na dhana au mtazamo wa kumchukulia kama mtu mwenye asili ya kidunia na badala yake alitaka waone kuwa yeye alikuwako kabla ya kuja duniani kama mwanadamu kwa kusudi la ukombozi wa watu. Soma kwa makini maandiko haya:-
Yohana 8:23
Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu
Yahana 6:62
Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?
Katika maandiko hayo yote mawili, Bwana Yesu kwa uwazi kabisa anaweka bayana juu ya asili yake ya mbinguni kabla ya kufanyika mwanadamu na kuzaliwa na bi’ Mariam, katika andiko lile la kwanza Bwana Yesu anaweka utaofauti wa wazi baina yake na wanadamu wa kawaida kwa kusema ‘Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
Na katika tamko jingine Yesu anawauliza Wayahudi kuwa Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?, kwahivyo Yesu anaonyesha kuwa kabla ya ujio wake duniani kuna mahali (mbinguni) alikokuwako kwanza.
Asili ya Yesu na msingi wa mamlaka yake ya Uungu
Uelewa juu ya asili ya Yesu linakuwa ni jambo rahisi tu sasa kadri ya msingi mzuri tuloujenga tangu mwanzo wa uchanbuzi wa mada hii na hususani kupitia matamko mbalimbali hata yale ya Yesu mwenyewe yanayotoa picha ya wazi kuwa Yesu hakuwa kamwe na asili ya dunia hii ya ubinadamu licha ya kwamba alizaliwa na Mariam kwakuwa pale alipozaliwa na Mariam haukua ndiyo mwanzo wa kuwepo kwakwe, bali kupitia kuzaliwa na Mariam alikuwa tu akitengenezewa njia ya kufunika mamlaka yake ya kuu ili aweze kumfikia mwanadamu kama tutakavyoona katika kipengele kinachofuata.
Hatahivyo kanuni za msingi zinazofanya Yesu kuwa mwanadamu wa asili ya kawaida hazikufikiwa katika mchakato wa kuzaliwa kwake, hebu tusome kidogo andiko hili’
Mathayo 1:18
Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Hivyo kuzaliwa kwa Yesu kunatofautiana kabisa na kanuni ya kawaida ya uzazi wa wanadamu wengine ambapo kadri ya andiko hilo Biblia inaweka bayana kuwa Mariam alipata mimba ya kumzaa Yesu kabla hajakaribiana na mwanamume na yakuwa mimba hiyo ni kwa uwezo wa roho mtakatifu.
Kwa hali hiyo katika uzazi wa Yesu hapakuwepo kamwe na mfumo wa kawaida wa kibaolojia unaohusisha hatua mbalimbali za Kisayansi za uzazi kama ambavyo hata maandiko ya Qur an yanavyoainisha katika sura mojawapo ya kitabu cha msaafu wa Qur an kama tunavyosoma hapo chini:-
Qur an 22:5
Enyi watu! Kama mumo katika shaka juu ya ufufuo; (mnaona haimkiniki kufufuliwa), basi (tazameni namna Tulivyokuumbeni); kwa hakika Tulikuumbeni kwa udongo. (Mzee wenu Nabii Adamu),kisha (Tukawa Tunakuumbeni ninyi) kwa manii, (mbegu ya uhai)
Msahafu wa Quran hapo unaweka bayana hatua hizo za uumbaji na inazitaja kama kanuni zilizo na zinazotumika kuibua mwanadamu na kuendeleza kizazi cha wanadamu huyo, ambapo njia hizo mbili yaani ile awali ya kuumbwa kwa udongo (Nabii Adam na Hawa) na ile ya mbegu ya uzazi (Viumbe wengine).
USIKOSE SEHEMU YA PILI
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW