Friday, July 14, 2017

ISIS WALIPUA MSIKITI WA KIHISTORIA NCHINI IRAQ.

No automatic alt text available.


Jeshi nchini Iraq limethibitisha kwamba wanamgambo wa dola ya kiislam Islamic State wameulipua msikiti mkuu wa Al-Nuri ulioko mjini Mosul .
Msikiti huo unaaminika ndimo kiongozi wa wanamgambo wa ISIS Abu Bakr al-Baghdadi alitoa hotuba yake miaka mitatu iliyopita wakati alipokuwa akitangaza "ukhalifa" mpya.
Wakati hayo yakijiri, wanamgambo hao wa ISIS wao wanadai kwamba ndege za jeshi la Marekani ndiyo zilizo zilizousambaratisha msikiti huo.
Mapema leo, Kamanda wa majeshi ya Iraq aliiambia BBC kwamba walikuwa mita kadhaa kutoka msikitini hapo, walipokuwa katika harakati zao za kusonga mbele kwenye mapambano lengo likiwa ni kuteka ngome kuu ya wanamgambo hao wa kiislam wa Is nchini Iraq.
Source: BBC Swahili.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW