Sunday, February 12, 2017

KUMBE MUHAMMAD KARUHUSU KUVAA VIATU MSIKITI

Image may contain: one or more people and text
MUHAMMAD AWAAGIZA WAISLAM WOTE KUVAA VIATU WAKATI WANASWALI MSIKITINI
KUMBE KUVUA VIATU NI UTAMADUNI WA WAYAHUDI.
Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujikumbushe na kujifunza kuhusu kusali na viatu katika nyumba za ibada. Hususan Msikitini.
Waislam mara nyingi wamekuwa wakiwashutumu Wakristo na kuwakejeli kuwa, eti wanasali na viatu Kanisani.
Je, Mtume wa Allah aitwaye Muhammad alivaa viatu alipo kuwa anaswali Msikitini?
Hebu tuangalie ushahidi huu hapa:
Ukisoma kitabu cha Al-u-lu wal-marjan Uk. 179
14. Mlango:
Ruhusa ya kusali na Viatu.
325. Hadithi ya Anas Bin Malik (R.a) kutoka kwa Said Bin Yazid Al-Azid (r.a) amesema, Nilimuuliza Anas Bin Malik (r.a) “Hivi Mtume (s.a.w) alisali huku amevaa viatu vyake?” Akanijibu, “Ndiyo” (Bukhari, Hadithi N. 383, Juzuu ya 1)
Hapo tunamuona Muhammad akisali na Viatu, na mlango hapo umesema, Ruhusa ya kusali na Viatu, maana yake waislamu hapo wameruhusiwa kusali na Viatu, pia haikuishia hapo, Muhammad akasema tena kuwaambia Waislamu.
Ukisoma kitabu kinachoitwa “TAFSIRI YA BULUGH AL-MARAM MIN JAM’I ADILLATIL AHKAM
Ukurasa wa 101 Hadithi Na. 171
Abu Said (r.a) amesimulia: Mtume (S.a.w) amesema: “Ye yote miongoni mwenu atakapoenda msikitini kusali, basi atizame, akiona uchafu au najisi katika viatu vyake aondoe kisha aswali navyo”. Abu Dawud Ibnu Khuzaimah ameipa daraja ya Sahih.
*Murad wa kutwaharisha viatu:

Iwapo mtu amekanyaga najisi kwa kiatu, atakitwaharisha kwa kusugua chini mchangani*
Image may contain: one or more people, text and indoor

Hapo kwa mtu mwenye akili zake timilifu, hawezi kukomaa na kuanza kuwalaumu Wakristo, eti kwa nini wana Sali na viatu? Wakati Muhammad mwenyewe, alisali huku amevaa viatu, na pia akawaambia waislamu wanapoenda kusali, basi watazame viatu vyao kama kuna najisi, basi wavisugue chini mchangani, labda waislamu watuambie wao kusali na viatu, ni Uviviu wa kusugua viatu mchangani? Au mazingira yao wanayoishi hayana mchanga?

Tena Muhammad akakazia zaidi kuhusu Viatu, aliponukuliwa katika Hadithi hii.
Kasema Mtume (S.a.w) “Atakaepata (ona) nge nae anasali, basi amuue kwa kiatu cha kushoto” (Mkweli Mwaminifu, Juzuu ya 1-2, Hadithi Na. 188, Uk, 88)
Muhammad anawataka Waislamu wakimuona Nge basi wamuue kwa kiatu cha kushoto, sasa jiulize, wewe umevua viatu, unaswali peku peku (kama bata) Halafu amekatiza nge, unaweza kweli kumkanyaga kwa mguu? Nachoweza kusema ni uvivu tu wa waislamu katika kusugua mchangani viatu vyao vilivyo na najisi, kwani wameshapewa ruhusa ya kusali navyo.
Kumbe Mtume Muhammad alikuwa anavaa viatu alipo kuwa ndani ya Msikiti.
“Nabii wa Allah akatuambia: Msiwe kama Wayahudi wanao Swali bila ya Viatu au viatu vyao vya ngozi (khufoof).” (Abu Dawood, 652; classed as saheeh by al-Albaani in Saheeh Abi Dawood, 607).
Kumbe utamaduni wa kuvua viatu ni wa Wayahudi na sio WAISLAM WANAO KOPIA KILA KITU.
Huu ni MSIBA MKUBWA SANA.
SASA TUMSOME NABII WA ALLAH:
SOMA UTHIBITISHO HAPA:
Anas ibn Maalik (may Allaah be pleased with him) aliuiza, Je, Mtume Muhammad (PBUH) aliomba huku akiwa amevaa Viatu? Alinijibu NDIO” (al-Bukhaari, 386; Muslim, 555).
Endelea uone kwanini Muhammad alivua viatu mara moja:
Ngoja niwaletee hadith ya Abu Saeed al Khudri alisema: Wakati nabii wa Allah alipo kuwa anaongoza swala kwa Maswahiba wake, alivua viatu vyake na akaviweka upande wa kushoto. Maswahiba wake walipo muona, nao wakavua viatu vyao. Nabii wa Allah alipo maliza kuongoza swala, akawauliza Maswahiba wake, kwanini walivua viatu vyao? Wakamjibu, sisi tumekuona wewe ukivua viatu vyako, na sisi tukafanya hivyo. Nabii wa Allah (amani iwe juu yake) akasema: Jibril (PBUH) alikuja na akaniambia kuwa kulikuwa na uchafu kwenye viatu vyangu. Lakini nyie mnapo kuja Msikitini, vichunguzeni Viatu vyenu na kama mkiona uchafu kwenye Viatu vyenu, basi, safisheni au toeni huo uchafu na muombe huku mkiwa mmevaa Viatu. (Abu Dawood, 650; classed as saheeh by al-Albaani in Saheeh Abi Dawood, 605).
Kumbe basi Muhammad alikuwa anavaa viatu alipo kuwa Msikitini isipokuwa mara moja tu alipo ambiwa na Jibril kuwa viatu vyake vina uchafu.
WAISLAM, KWANINI HAMFUATI MAAMRISHO YA MUHAMMAD YA KUVAA VIATU MSIKITINI NA MNAENDELEA KUFUATA UTAMADUNI WA WAYAHUDI WA KUTO VAA VIATU?
Natanguliza pole kwa Waislam.
Kumbe Mtume Muhammad alisali na viatu Msikitini.
Hakika Uislam ni dini bandia.
Max Shimba Ministries Org

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW