Thursday, February 16, 2017

QURAN YAMKIRI YESU KUWA NI MUNGU WA KWELI

No automatic alt text available.
Katika vitu ambavyo waislamu huwasumbua vichwa na akili zao, ni kuhusu Uungu wa Yesu, sema vitu vyote lakini ukifika hapo kwenye Uungu wa Bwana Yesu basi mnapotezana, na kitu ambacho kinawafanya waislamu washindwe kukubali kuwa yeye ni Mungu, ni ukosefu wao wa ROHO MTAKATIFU, maana mtu hawezi kukiri kuwa Yesu ni Bwana (Mungu) kama hana ROHO MTAKATIFU, kama yasemavyo maandiko.
2 Korintho 12: 3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
Kwa hivyo Ndugu yangu Mkristo unapojadiliana na Muislamu kuhusu Habari za Uungu wa Yesu, kamwe hawezi kukubali mpaka ROHO MTAKATIFU auhusike, kinyume na hapao itakuwa ni sawa na kumpigia mbuzi Gitaa, kwa hivyo hoja zake zote zitaegemea katika hali ya Kuutazama mwili kama ambavyo Elisabeti, alimtazama Yesu kama mtu wa kawaida sana ambaye atazaliwa na Mariam, lakini mara baada ya kujazwa na Roho Matakatifu, ndipo alipokiri kuwa Yesu ni Bwana yaani Mungu wake.
Luka 1: 39 Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda,
40 akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.
41 Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
43 Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?
Hapo tumeona ni namna gani Umuhimu wa ROHO MATAKATIFU, katika kumjua Yesu kuwa ni Mungu, kwa kuwa Waislamu hawana Roho Mtakatifu, kazi yao hasa ni kumtaza Yesu alipoutwaa Mwili wa Kibinadamu, na kuwa na asili ya mtu, na kuuficha Uungu wake katika mwili, ndo maana akawa akiijita Mtume, Mwana, Kuhani, na hata Nabii, sasa leo sina lengo hasa la kuueleza Uungu hasa wa Yesu, kiundani kwa Biblia, bali nataka niitazame Quran namna ambavyo imemkiri Yesu kuwa ni Mungu, kwa kueleza Sifa za Mungu, ambazo Yesu anazo, kwa hivyo nitaeleza SIFA 5 NDANI YA QURAN ambazo zinakiri UUngu wa Yesu.

(1) Mungu ni mwenye kujua yaliyomo katika nyoyo za watu.
رَّبُّكُمْ أَعْلَمُ بِمَا فِي نُفُوسِكُمْ إِن تَكُونُواْ صَالِحِينَ فَإِنَّهُ كَانَ لِلأَوَّابِينَ غَفُورًا
Quran 17:25. Mola wenu anajua sana yaliyomo nyoyoni mwenu, kama mkiwa wema, basi hakika yeye ndiye Mwenye kusamehe wenye kurejea.
Hapo Quan inatupa habari kuwa MOla au Mungu yeye ni mwenye kujua yaliyomo katika nyoyo za wanadamu, sifa hiyo inamwendea Yesu kwani ni mwenye kujua yaliyomo ndani ya mioyo ya wanadamu.
Yohana 2: 24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote;
25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.
Kama Waislamu wangelikuwa na Roho Matakatifu, kwa ushahidi huu basi wasingeweza kupinga kuhusu UUngu wa Yesu.
(2) MUNGU NI NI MWENYE KUONGEZA IDADI YA UWEPO WA WATATU
Namaanisha kuwa pakiwa na watu wawili au watatu basi Mungu anaongezeka na kuwa wanne, kwa watu watatu, au watano kwa watu wanne, kama isimemavyo Quran
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَى ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ وَلَا خَمْسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمْ وَلَا أَدْنَى مِن ذَلِكَ وَلَا أَكْثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمْ أَيْنَ مَا كَانُوا ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّ اللَّهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Quran 57:7. Je, huoni kwamba Mwenyeezi Mungu anajua viliyomo mbinguni na viliyomo ardhini? Hawashauriani kwa siri watatu ila yeye ni wa nne wao, wala watano ila yeye ni wa sita wao, wala wachache kuliko hao wala zaidi ila yeye huwa pamoja nao popote walipo. Kisha siku ya Kiyama atawaambia waliyoyatenda hakika Mwenyeezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Hapo tunapewa sifa za Mungu, kwa uzuri kabisa, pakiwa na wawili Mungu wa tatu, wakiwa watatu, Mungu wanne, wakiwa wanne, Mungu wa watano, SIFA hizo zinamwendea Yesu Kristo mwenyewe kama alivyosema.
Mathayo 18: 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.
Hapa Yesu anatuambia sifa hiyo ya kuwa pamoja na watu wawili au watatu, sifa hiyo ni yake yeye mwenyewe Yesu…. Tatizo la kutokuwa na Roho Mtakatifu kwa waislamu ndiyo maana wanashindwa kutambua kuwa Yesu ni Mungu.
(3) Mungu yeye ni Nuru ya Mbingu na Nchi.
اللَّهُ نُورُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَاةٍ فِيهَا مِصْبَاحٌ الْمِصْبَاحُ فِي زُجَاجَةٍ الزُّجَاجَةُ كَأَنَّهَا كَوْكَبٌ دُرِّيٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ مُّبَارَكَةٍ زَيْتُونِةٍ لَّا شَرْقِيَّةٍ وَلَا غَرْبِيَّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِيءُ وَلَوْ لَمْ تَمْسَسْهُ نَارٌ نُّورٌ عَلَى نُورٍ يَهْدِي اللَّهُ لِنُورِهِ مَن يَشَاء وَيَضْرِبُ اللَّهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ وَاللَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Quran 24: 35. Mwenyeezi Mungu ni nuru ya mbingu na ardhi, mfano wa nuru yake ni kama shubaka ndani yake mna taa. Taa ile imo katika tungi, tungi lile ni kama nyota ing'aayo inayowashwa katika mti uliobarikiwa wa mzaituni, si wa mashariki wala magharibi yanakaribia mafuta yake kung'aa ingawa moto haujayagusa, nuru juu ya nuru, Mwenyeezi Mungu humuongoza kwenye nuru yake amtakaye, na Mwenyeezi Mungu hupiga mifano kwa watu, na Mwenyeezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
QURAN IMESEMA MUNGU, NI NURU YA MBINGU NA NCHI, SIFA HIYO NI YA YESU, MAANA YESU NI NURU YA ULIMWENGU.
Yohana 8: 12 Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
TENA YESU NI NURU YA MBINGU.
Matendo 26: 13 Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote.
14 Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.
15 Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.
Sifa zote hizo za kuwa Nuru ya Mbingu na aridhi, Yesu, anazo, kwa nini Waislamu wanashindwa kutambua kuwa Yesu ni Mungu? Ni kwa sababu, hawana ROHO MTAKATIFU.
(4) MWENYEZI MUNGU YEYE NI MWANZO NA WA MWISHO.
Quran inatupa habari kuwa Mwenyezi Mungu sifa yake yeye ni wa kwanza na pia ni wa Mwisho.
Quran 57: هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
3. Yeye ndiye wa Mwanzo na wa Mwisho, naye ni wa dhahiri, na wa siri, naye ni Mjuzi wa kila
Hapa Quran inasema yeye, Allah hasemi, mimi ni wa kwanza na mwisho, bali yeye, kuonesha kuwa siyo muhusika wa sifa, sasa Yesu yeye ambaye ndiye Muhusika wa sifa hizo, anasema
Ufunuo 1: 6 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake.
17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,
Yesu anasema Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, Allah yeye anasema yeye, yeye hii inamwendea Yesu, kwa kuwa ameshatangulia kusema hata kabla ya kuja Quran, kinachowafunga ni Ukosefu wa ROHO MTAKATIFU kwa waislamu.
(5) MWENYEZI MUNGU YUKO MBINGUNI.
Quran inaeleza kuwa Mungu yupo mbinguni,
Quran 67: أَمْ أَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاء أَن يُرْسِلَ عَلَيْكُمْ حَاصِبًا فَسَتَعْلَمُونَ كَيْفَ نَذِيرِ
17. Au je, mnadhani mko salama kwa (Mwenyezi Mungu) alioko mbinguni kuwa yeye hatakuleteeni kimbunga chenye changarawe? basi karibuni mtajua lilivyo onyo langu
Quran inatambua uwepo wa Mungu kuwepo mbinguni, kwani Allah yeye makao yake ni hapa Duniani, huko Makka ambako waislamu, huenda kuhiji huko, na pia kila swala huelekea kwake, Allah Makka kama alivyoema katika quran 7:29. Kwa hivyo Allah hawezi kuwa mbinguni kwa sababu yeye yupo Duniani, Sifa hiyo ipo kwa Yesu.
Matendo 1:9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,
11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
Pengine Waislamu wanaweza kujiuliza Ni vipi Yesu achukuliwe kwenda Mbinguni? Alichukuliwa na nani? Ni wingu ndilo ambalo lilimchukua, kwani Wingu ni gari la Mungu.
Zaburi 104: 3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,
KWA HIVYO NIMEWEKA HIVYO VIPENGELE VICHACHE ILI ANGALAU NIWEZE KUWATOA WAISLAMU GIZANI KUHUSU UUNGU wa Yesu, japo kuwa siyo rahisi wao kukubali kuwa Yesu ni Mungu, hata kama maandiko wanayaona dhahiri, ila kwa sababu hawana ROHO MTAKATIFU, wataendelea kupinga kuwa siyo Mungu, wakati Quran imekubali, na isitoshe mungu wa dunia hii (shetani) amezifunga fahamu na akili zao kwa kumkosa ROHO MTAKATIFU, isiwazunukie Nuru ya Injili ya Kristo aliye Sura yake Mungu.
2 Korintho 4: 3 Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;
4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.
Waislamu Mtafuteni ROHO MTAKATIFU, ili muweze kumjua Yesu na UUngu wake…. Muislamu tambua kuwa Quran imetumika tu kama kibao kukuonesha njia, yaani inakuelekeza pa kumpaa Mungu, ukifika sehemu ukakuta kibao kimekuelekeza kwa mshare, Muhumbili ni kule, wewe usikae kwenye hicho Kibao, hapo siyo Muhimbili, fuata Ramani ya Hicho kibao, utafika Muhimbili, Quran ni kibao, kinakuelekeza kwenye Biblia, huko ndo unampata Mungu wa kweli Yesu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW