Friday, May 19, 2017

MUNGU ANAKUPIGANIA, MAADUI ZAKO WAMESHINDWA KWA JINA LA YESU

Image may contain: 1 person, text
Wana wa Israel waliteseka kwa miaka mingi katika nchi ya utumwani Misri. Walimlilia Mungu kwa muda mrefu, na wakati wa Bwana ulipofika Mungu akashuka na kuwaokoa.
Kutoka 3:7-9 
“BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.”
Baada ya Bwana kuwatoa misri bado farao aliwafuatilia, lakini muda wa Bwana kuokoa ukifika hakuna awezaye kuzuia. Bwana aliteketeza jeshi lote la wamisri baharini na kuwaokoa watoto wake.
Kutoka 14:13-15, 25
“Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya. BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele. Akayaondoa magurudumu ya magari yao, hata yakaenda kwa uzito; na Wamisri wakasema, Na tukimbie mbele ya Israeli; kwa kuwa BWANA anawapigania, kinyume cha Wamisri.”
Bwana atakupigania kinyume na adui zako wawe ni magonjwa, kukataliwa, kukosa kazi, kukosa mtoto n.k. Simama katika imani ukauone wokovu wa Bwana.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW