Sunday, May 14, 2017

NABII MIRIAM

Image may contain: one or more people
MIRIAM NABII WA ISRAEL DADA YA MUSA NA HARUNI.
Soma Kutoka 2 na 15 na Hesabu 12 na 20

Miriam alikuwa ni dada wa Musa na Haruni na Jina la Miriam linamaana ya anayempenda Bwana.
Hesabu 26:59 Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi, binti wa Lawi, ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amramu Haruni, na Musa, na Miriamu umbu lao.
Tunasoma habari za Miriam kwanza pale alipomlinda mdogo wake Musa alipokuwa amewekwa kwenye kisafina kingoni mwa mto, na ndiye aliyeongea na binti wa farao kumuelezea kuwa kuna mtu anayeweza kumnyonyesha huyo mtoto. Uwezo mkubwa wa kufikiri na kushawishi wa Miriamu ulimwezesha Musa kulelewa na kunyonyeshwa na mama yake mzazi hadi alipoacha kunyonya.
Miriam alishirikiana na Musa katika harakati za kuwatoa wana wa israeli utumwani Misri.
Mika 6:4 Kwa maana nalikupandisha kutoka nchi ya Misri, na kukukomboa utoke katika nyumba ya utumwa, nami naliwapeleka Musa, na Haruni, na Miriamu, watangulie mbele yako.
Tunasoma pia kuwa Miriamu alikuwa ni nabii katika Israeli.
Kutoka 15:20a Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake haruni, akatwaa tari mkononi mwake;
Utumishi wake ulianzia pale alipohakikisha usalama wa Musa ambaye baadaye alikuja kuwa nabii mkubwa katika israeli. Miriamu pia alikuwa muimbaji na aliwaongoza wana wa Israeli kuimba wimbo wa sifa baada ya kuvuka kwa salama bahari ya shamu na Mungu kuliteketeza jeshi la Misri.
Kutokana na Miriamu kishi na Musa alipokuwa mtoto, kukaa naye muda mrefu na kuwa mkubwa kwake, kwa kiasi fulani alisahau utumishi wa kaka yake na kuona kuwa yeye anastahili kuwa sawa naye kiutumishi. Wakati Musa alipomuoa mwanamke wa Kushi na kusema kuwa Mungu amesema naye, Miriamu hakukubaliana naye. Kwanza alimsema kwa sababu ya kuoa mke wa Kushi na pili kwa sababu alisema Mungu amesema naye na kwanini aseme naye tu na sio yeye Miriamu. Alisahau kuwa Musa ndiye aliyekuwa ameitwa na Mungu kwa ajili ya taifa la Israeli.
Hesabu 12:1-2 Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke mkushi. Wakasema, Je! ni kweli Bwana amenena na Musa tu? hakunena na sisi pia? BWANA akasikia maneno yao.
Wivu ulimpata Miriamu juu ya utumishi wa kaka yake na kusahau kuwa yeye pia ni mtumishi katika nafasi yake. Unapojisahau wewe ni nani na kudharau huduma uliyopewa na Mungu ni rahisi sana wivu kukupata juu ya huduma za watu wengine.
Vile vile Miriamu sababu anamfahamu Musa kwa undani zaidi basi kwa kuangalia udhaifu wake wa kibinadamu akadhani kuwa Mungu hawezi kumtumia bila kuwatumia na wao pia. Mara nyingi tumewanyooshea watumishi wa Mungu vidole kutokana na kuwa tunaangalia udhaifu wao na kusahau kuwa Mungu anaangalia zaidi ya sisi binadamu tunavyoangalia. Mheshimu mtumishi yeyote wa Mungu hata kama ni mdogo kwako au wewe ndiye uliyemshuhudia kuokoka. Tusiwaseme vibaya watumishi wa Mungu kwa lolote wanalolifanya maana hatujui maagano yao na Mungu.
Miriamu alimshirikisha kaka yake Haruni katika kumteta Musa na Mungu aliwasikia. Mungu alikasirika kwa tendo hili na akamwagiza Musa kuwa wote watoke nje ya hema ili akazungumze nao. Kutokana na ushawishi wake kwa Haruni katika kumteta Musa, Miriamu aliadhibiwa na Mungu pale pale. Musa alipoona Miriamu amepata ukoma akamlilia Mungu kwa ajili ya rehema kwa Miriamu, Mungu alisikia maombi yake lakini hakumponya pale pale, aliacha kwanza kwa muda wa siku saba ili iwe fundisho kwa miriamu na watu wote wakiwemo sisi tunaosoma habari hii siku ya leo.
Kama mtumishi wa Mungu, pale watu wanapokunenea vibaya usiweke kinyongo wala kulipiza kisasi, mwachie Mungu yeye ndiye mpiganaji wako na usiache kuomba rehema kwa ajili yao ili Mungu aweze kuwaponya. Hakika tumejifunza mengi kupitia maisha ya Miriamu.
Hesabu 12: 4-15 (Tafadhali soma mistari hii)
Shalom.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW