Saturday, May 27, 2017

SIMAMA IMARA KATIKA IMANI

Image may contain: one or more people and text
Mtume Petro alikuwa na imani yenye nguvu. Ni kwasababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu wakati Yesu alimuita, alitoka katika mashua na kuanza kutembea juu ya maji. Aliamini kwamba Mungu angempatia uwezo wa kutembea juu ya maji kama vile Yesu. Vilevile, wakati Yesu alituita tuwe wafuasi wake, tulijitoa kwa Mungu katika sala na kubatizwa. Kwa sababu tulikuwa na imani katika Mungu, na tulitumaini kwamba Mungu atatusaidia.—Yohana 14:1; soma 1 Petro 2:21.
Petro alikuwa anajua vizuri sana kuogelea, kwa hiyo, angeamua kuogelea ili kurudi kwenye mashua. (Yohana 21:7) Lakini, sababu gani hakufanya hivyo? Kwa sababu hakujitegemea yeye mwenyewe ili kupata msaada. Alikaza tena akili yake juu ya Yesu na alikubali amsaidie. Ikiwa tunatambua kwamba imani yetu imeanza kuwa dhaifu, tunapaswa kumuiga Mtume Petro na kumtegemea Mungu wakati wa tumeshindwa au tunahitaji msaada.
Kama vile tu Mtume Petro alikaza tena akili yake juu ya Yesu, sisi pia tunapaswa kumtazama Yesu ‘kwa makini [kwa uangalifu].’ (Soma Waebrania 12:2, 3.) Lakini, tofauti na Mtume Petro, sisi hatuwezi kumuona Yesu kwa macho yetu leo. Kwa hiyo, namna gani tunaweza ‘kumtazama’ Yesu kwa uangalifu? Tunaweza kujifunza mambo yenye alifundisha na kufanya. Kufanya hivyo kunaweza kutusaidia tumuige kwa uaminifu. Hilo litatusaidia kutia nguvu imani yetu.
Usikate tamaa, simama imara katika Imani. Mtazame Yesu na amini kuwa alisha maliza yote pale Msalabani.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW