Saturday, May 13, 2017

ROHO MTAKATIFU NA KAZI ZAKE KWETU SOMO LA 6

Image may contain: 3 people, text
JE, NINI MAANA NA FAIDA YA KUNENA KWA NDIMI?
Tuanze kwa kusoma Biblia:
“Hata ilipotimia Siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine [zingine – KJV], kama Roho alivyowajalia kutamka.
Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja ALIWASIKIA WAKISEMA KWA LUGHA YAKE MWENYEWE. Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? Imekuwaje basi SISI KUSIKIA KILA MTU LUGHA YETU TULIYOZALIWA NAYO? Waparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia [Libya] karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na Waongofu, Wakrete na Waarabu; TUNAWASIKIA HAWA WAKISEMA KWA LUGHE ZETU matendo makuu ya Mungu.” Matendo 2:1-
11.
Siku ya Pentekoste, mitume walizungumza kwa lugha. Matendo sura ya 2 inaweka wazi kwamba mitume walikuwa wakisema kwa lugha ya binadamu (Matendo 2:6-8). Neno lilotafsiriwa "lugha" katika zote Matendo sura ya 2 na 1 Wakorintho sura ya 14 ni glossa/ndimi ambalo lina maana ya "lugha."
Kuzungumza katika lugha ilikuwa ni uwezo wa kuongea katika lugha ambayo msemaji haijui, ili kutangaza injili kwa mtu ambaye anazungumza lugha hiyo. Katika eneo la kitamaduni la Korintho, inaonekana kwamba Karama ya lugha ilikuwa ya thamani na maarufu. Waumini Wakorintho walikuwa na uwezo bora wa kuwasilisha injili ya Neno la Mungu kama matokeo ya karama ya lugha. Hata hivyo, Paulo aliiweka wazi kwamba hata katika matumizi ya hii lugha, ilikuwa ya kutafsiriwa au "imetafsiriwa" (1 Wakorintho 14:13, 27). Muumini Mkorintho atanena kwa lugha ngeni, kutangaza ukweli wa Mungu kwa mtu ambaye alizungumza lugha hiyo, na pia huyo muumini, au muumini mwingine katika kanisa, alikuwa atafsiri yale aliyosemwa ili mkutano wote uweza kuelewa kile ambacho alisema.
KUNENA KWA LUGHA NI USHAHIDI WA KUPOKEA ROHO MTAKATIFU:
Kuna matukio matatu katika kitabu cha Matendo ya Mitume ambapo kunena katika lugha kunafuatana na kupokea Roho Mtakatifu- Matendo 2:4, 10:44-46, na 19:06. Hata hivyo, hafla hizi tatu ndio sehemu pekee katika Biblia ambapo kunena kwa lugha ni ushahidi wa kupokea Roho Mtakatifu. Katika kitabu cha Matendo, maelfu ya watu wanamwamini Yesu na hakuna mahali kumesungumziwa kuhusu kunena kwa lugha (Matendo 2:41, 8:5-25, 16:31-34, 21:20). Katika Agano Jipya inafundishwa kwamba kunena kwa lugha ni ushahidi tu mtu imepokea Roho Mtakatifu. Kwa kweli, Agano Jipya hufundisha kinyume. Tunaambiwa kwamba kila muumini katika Kristo ana Roho Mtakatifu (Warumi 8:9, 1 Wakorintho 12:13; Waefeso 1:13-14 ), lakini si kila muumini hunena lugha ngeni (1 Wakorintho 12:29-31).
Hivyo, kwa nini kuzungumza katika lugha kulikuwa ushahidi wa Roho Mtakatifu katika hivyo vifungu vitatu katika Matendo? Matendo 2 yanakili mitume wanabatizwa kwa Roho Mtakatifu na kuwezeshwa na Yeye kwa kutangaza habari njema. Mitume kuliwezeshwa kusema kwa lugha nyingine (lugha ) ili waweze kushiriki kweli na watu katika lugha yao wenyewe. Matendo 10 imerekodi Mtume Petro kupelekwa kushiriki injili na watu wasio Wayahudi.
Matendo 10:44-47 inaeleza hiya: "Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.
FAIDA YA KUNENA KWA LUGHA:
Kunena na au kuomba kwa lugha mpya kuna faida sana katika maisha yako. Shetani anajua umuhimu na nguvu ya maombi kupitia ndimi/lugha. NI rahisi sana kwa Shetani kukutibua ukiwa unaomba kwa akili, lakini Shetani hana ujanja wa kukutibua ukiwa unaomba kwa roho nikimaanisha kwa lugha/ndimi. Mtume Paulo katika Wakirontho alisema, "Nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. Imekuwaje basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia....." (1 Wakorintho 14:14,15).
Hivyo basi, mtu akiomba kwa roho yaani kwa lugha, ni Roho Mtakatifu anayetoa hiyo lugha (Anaye kuongoza katika Maombi), hivyo ni Roho Mtakatifu atakayekusaidia ni jambo gani kuombea sawasawa na uhitaji wako. Zaidi ya hapo, Roho Mtakatifu atakusaidia kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu juu ya jambo hilo. (Warumi 8:26, 27).
Kuomba kwa akili (sio kwa lugha) kunachosha mapema na huwa kuna kurudiarudia maneno, mwishowe inakuwa upayukaji tu ili uombe muda mrefu, lakini mtu anapoomba kwa lugha panakuwa na uwezesho wa ajabu wa kudumu katika maombi kwa muda mrefu bila kuchoka, maana si akili inayoomba bali ni roho ya mtu, na roho haijui uchovu wa mwili, (Yesu alisema roho i radhi lakini mwili huu dhaifu, akawauliza yaani mmeshindwa kuomba hata kwa lisaa limoja?) Unaona tatizo la kuomba kwa ktumia akili?
JE, LUGHA ZILIZONENWA ZILIJULIKANA AU HAZIKUJULIKANA?
Lugha iliyotumika kuelezea Matendo 2:4 inasema kwamba wale walioipokea karama ile ya lugha walisema “kwa lugha nyingine [zingine – KJV],” yaani, walisema kwa lugha zaidi ya zile walizozitumia kwa kawaida kama lugha zao za kuzaliwa nazo.
Wakati ule wa Pentekoste walikuwapo “Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu.” Fungu la 5. Wayahudi wale walikuwa wametawanyika miongoni mwa mataifa kwa kipindi kirefu sana, na wengi wao hawakuweza kusema tena Kiebrania au Kiaramu. Karama ile ya lugha iliwawezesha kutoa hotuba na ushuhuda kuhusu “matendo makuu ya Mungu” (fungu la 11) aliyotenda kwa njia ya Yesu wa Nazareti, kiasi kwamba Wayahudi wale waliokuwa si wa nchi ile ya Palestina, yaani, wahujaji wale waliokuja katika Mji ule Mtakatifu wa Yerusalemu, waliweza kuelewa yote yaliyosemwa katika lugha za mahali kwao walikotoka.
Ni dhahiri kwamba lugha zilizonenwa pale ni zile tu zilizojulikana na watu. Wasikilizaji wale walishangaa sana “kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.” Matendo 2:6.
“Kila lugha inayojulikana ilikuwa imewakilishwa na wale waliokusanyika pale. Lugha zile mbalimbali zingekuwa kipingamizi kikubwa kwa utangazaji wa injili ile; kwa hiyo Mungu kwa njia ya mwujiza aliujazia upungufu waliokuwa nao wale mitume. Roho Mtakatifu aliwafanyia kile ambacho wasingeweza kukipata katika maisha yao yote. Kuanzia sasa [wakati ule] wangeweza kuzitangaza mbali kweli zile za injili, wakisema kwa usahihi lugha za wale waliokuwa anawahudumia.”
Kuomba katika lugha si kitu ambacho huamua wokovu wako, la hasha. Zaidi ya hapo, Kuomba katika lugha si kitu kiinamtofautisha Mkristo kukomaa kutoka kwa Mkristo machanga. Kwahiyo, usijisikie vibaya kama bado haujaanza kunena kwa lugha.
USIKOSE SEHEMU YA SABA: Matunda ya Roho Mtakatifu ni gani?
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW