Wednesday, April 12, 2017

DALILI ZA MWANAMKE ALIYEOLEWA NA JINI

Image may contain: 1 person, text and closeup
1. Hapendi kabisa kuwa karibu na wanaume, kwa kuwa tayari ana mume wa kiroho
2. Akichumbiwa lazima aharibu uchumba mwenyewe , lazima atabadilisha mawazo na kusema simtaki mwaume huyo tena, yule jini ndiye anamletea mawazo ya kukataa mwenyewe. Huyu ni JINI TWAYR {qarnail}.
3. Kama akikaribia kuolewa lazima atakataa lakini baadaye umri ukienda anajisikia vibaya
4. Kama aking’anga’ana na kuolewa hawezi kuifurahia ndoa yake kabisa ataona ndoa kama ni mateso, vile vile hawezi kumpenda mume wake kabisa , mumewe akiwa mbali anamumiss akija anajisikia kumchukia kabisa, kumchukia mwenza wako pindi anapo kuwa karibu na wewe. Huyu ni JINI SUBIANI.
5. Kama ameolewa hawezi kupata mtoto kwa maana Yule mume anaona wivu kuona mkwewe anazaa na mume mwingine, Hata kama akifanya biashara hawezi kufanikiwa kabisa kwa maana jini yule anammiliki.
6. Kua na hasira sana bila hata sababu za msingi
7. Kuwa na hali ya kutojali au kuthaminni wengine umimi na kujiona wa thamani peke yako kuliko wengine.
8. Kuchukiwa na ndugu jamaa na marafiki anakufanya ufanye mambo yakuchukiza wengine
9. Kujiona mtu mwenye mikosi nuksi na balaa tupu
10. Kuvurugika kwa mipango/ mambo yako/ hasa ya maendeleo na kila unachopanga hushindikana hata kama ukisaidiwa na mwisho hujiona hufai
11. Kuumwa kichwa pindi wakat unasoma Biblia au masomo ya kawaida
12. Kutokujisikia kuomba au kusinzia pindi unapotaka kuanza maombi, huishiwa nguvu kabisa, Na kuishia kuhangaika kama mtu asiyejua lakufanya
Kwa hiyo inawezekana jini anapoanza kumfuata mtu na kufanya mapenzi naye, mtoto anaweza kuzaliwa. Nje ni mtu lakini kwa ndani siyo mtu ni shetani. Kuna mtu yuko hapa ni zao la ndoa za rohoni ndiyo maana unajiona ni wa ajabu ajabu, kuna wengine usiku unaota amezaa watoto siyo kwamba umeota ni kweli umezaa watoto wa kijini, na wale wanaporudi ujijini wanakurudi na kukuletea wewe matatizo.
Mwanamke aliyeolewa na jini huwa anawekewa alama zifuatazo ili aendelea kumilikiwa na huyo jini
1. Na kila mwanamke anayeolewa anakuwa na cheti cha ndoa, huwezi kukiona rohoni lazima kinakuwepo kama hati ya kumilikiwa.
2. Alama nyingine ni alama ya ndoa ambayo ni pete ya kiroho, mtu anaweza kuokota pete au kuota anafunga ndoa na kuvalishwa pete
3. Alama kama chapa au chata , mtu anaweza kuwekewa alama kama chata /chapa rohoni na hiyo alama inampa mamlaka jini kummiliki mtu.
Matendo 16:13
Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.
Mungu huwa anaweka maelekezo ndani ya moyo wa mtu, sasa moyo wa mtu unaweza kuibiwa na kupewa moyo wenye maelekezo tofauti, maana yake umewekewa alama moyoni ya kushindwa, ndiyo maana ukisema huyo hawezi kuwa kiongozi maana yake ni maelekezo hasi, kwa jina la Yesu leo nakataa moyo wa kushindwa , kuanzia leo nitakuwa mbunge , nitasafiri nje ya nchi, nitaolewa na kuwa na ndoa njema,
Usikate tamaa, Yesu anaweza kukufungua sasa hivi kutoka kwenye hii ndoa ya majini.
Kwa jina la Yesu leo nafanya vita na kila mtu wa uzao wa kishetani namung’oa kwa jina la Yesu. Nakataa kwa jina la Yesu kama kuna mtu yeyote aliyezaliwa rohoni kutoka tumboni kwangu leo namteketeza kwa jina la Yesu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW