Friday, April 14, 2017

JE, YESU ALISULUBIWA SIKU YA IJUMAA?

Image may contain: one or more people and text
Kama ni hivyo, ni namna gani alimaliza siku tatu kaburini kama alifufuka Jumapili?"
Yesu alisema katika Mathayo Mtakatifu 12:40, “Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi” wale wanaoshikilia kuwa Ijumaa ndio ilikuwa siku ya kusulubiwa, wanasema kuna hali halisi amboyo Yesu anakisiwa kuwa kaburini siku tatu.
Katika fikira ya Kiyahudi katika karne ya kwanza, sehemu ya siku ilichukuliwa kuwa siku nzima. Jinsi Yesu alikuwa kaburini sehemu ya siku ya Ijumaa, Jumamosi nzima na sehemu ya siku ya Jumapili anachukuliwa kuwa kaburini siku tatu.
Mojawapo ya dhana kuu ya Ijumaa inapatikana katika Mariko Mtakatifu 15:42, ambayo inasema kuwa Yesu alisulubiwa “siku iliyo kabla ya sabato” Kama hiyo ilikuwa sabato ya kila juma, kwa mfano Jumamosi, kwa hivyo hiyo hoja huasiria Ijumaa kuwa siku halisi ya kusulubiwa.
Fundisho lingine kuhusu siku ya Ijumaa lasema kifungo kama Mathayo Mtakatifu 16:21 na Luka Mtakatifu 9:22, zatufundisha kwamba Yesu angefufuka siku ya tatu; kwa hivyo, hangehitaji kuwa kaburini siku tatu mchana na usiku. Tafsiri zingine zinapotafusiri “katika siku ya tatu” kwa hizi aya, si zote, na si kila mmoja anakubaliana kwamba “siku ya tatu” ndio njia nzuri ya kutafusiri aya hizi. Zaidi ya hayo, Mariko Mtakatifu 8:31 yasema kwamba Yesu atafufuliwa “baada” ya siku tatu.
Kwanini inatupasa kukumbuka kifo cha Yesu?
Yesu aliwaambia wafuasi wake wakumbuke kifo chake kwa kula mlo wa mfano, wakitumia mkate na divai. Mkate unawakilisha mwili wa Yesu nayo divai inawakilisha damu yake.—Soma Luka 22:19, 20.
Mkate ambao Yesu alitumia haukuwa na chachu. Katika Biblia, mara nyingi chachu hutumiwa kufananisha dhambi. Kwa hiyo, mkate ulikuwa mfano unaofaa wa mwili mkamilifu wa Yesu. Alitoa mwili wake uwe dhabihu, ambayo iliondolea mbali dhabihu za wanyama zilizotolewa kulingana na Sheria ya Musa. (Waebrania 10:5, 9, 10) Divai ilikuwa mfano wa damu ya Yesu yenye thamani iliyomwagwa ili kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi zetu.—Soma 1 Petro 1:19; 2:24; 3:18.
Kukumbuka kifo cha Yesu kunafaida gani?
Kukumbuka kifo cha Yesu kila mwaka huimarisha uthamini wetu kwa upendo wa Mungu usio na kifani. Alimtuma Mwana wake ili afe kwa ajili ya dhambi zetu. Kwa hiyo, tunapohudhuria Ukumbusho, tunapaswa kutafakari kifo cha Yesu kinamaanisha nini kwetu. Tunapaswa kufikiria jinsi tunavyoweza kuonyesha uthamini kwa yale ambayo Yehova na Yesu wametufanyia.—Soma Yohana 3:16; 2 Wakorintho 5:14, 15.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW