Saturday, April 8, 2017

MPENDWA UWE MACHO—SHETANI ANATAKA KUKUMEZA




“Iweni wenye kulinda. Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama Simba anayenguruma, akitafuta kummeza mtu.”—1 Petro 5:8.

Muwe macho masaa yote, maana Shetani anatafuta wa kummeza.

Hata hivyo, kiumbe huyu wa roho alianza kutamani wanadamu wamwabudu. Badala ya kuing’oa tamaa hiyo mbaya, aliisitawisha hivi kwamba ikakua na kuzaa dhambi. (Yakobo 1:14, 15) Kiumbe huyo ni Shetani, ambaye “hakusimama imara katika kweli.” Alimwasi Mungu na kuwa “baba ya uwongo.”—Yohana 8:44.

Mtume Petro alimfananisha Shetani na “simba anayenguruma.” Kitabu kimoja kinasema kwamba neno la Kigiriki linalotafsiriwa “anayenguruma” linamaanisha “sauti kubwa ya mnyama mwenye njaa kali sana.” Maana hiyo inafafanua vizuri sana ukatili wa Shetani! Ingawa tayari ulimwengu mzima unakaa katika nguvu zake, bado Shetani ana njaa ya kupata mawindo zaidi. (1 Yohana 5:19) Kulingana na Shetani, ulimwengu ni kama tu “kitu cha kuamsha hamu ya kula.” Kwa sababu hiyo, Shetani ameelekeza fikira zake kwenye “chakula chenyewe,” yaani, watiwa-mafuta walio duniani na waandamani wao, “kondoo wengine.” (Yohana 10:16; Ufunuo 12:17) Shetani ana lengo la kuwameza watu wa Mungu. Mateso mengi aliyowasababishia wafuasi wa Kristo kuanzia karne ya kwanza hadi leo yanafunua wazi ukatili wake.

Mpendwa, usilale wala usichoke kuomba, maaana Shetani anakuwinda ili akumeze.

Shalom,
Dr. Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW