Friday, April 14, 2017

SIFA ZA WATU WAENDAO JEHANNAM



Warumi 1: 26 Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile. 27 Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
28 Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya. 29 Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya, 30 na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao; 31 hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine. 32 Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.
Angalia sana ndugu usiwe na hizo sifa hapo juu. Hizo ni sifa za watu waendao Jehannam. Endelea kumtafuta Yesu ambaye ni Mungu na akulinde kwa damu yake. Endelea kufunga na kuomba bila ya kuchoka. Maana Shetani anatafuta mtu wa kummeza.
HABARI NJEMA KWA WATU WABAYA
“Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.” (Warumi 5:6)
Pengini utastaajabu vile vile kujua kwamba kuna-yo maandiko mengine yanayothibitisha ya kuwa kuna habari njema kwa watu wabaya. Hapa ni baadhi ya maandiko hayo:
Kristo Yesu alikuja ulimwenguni awaokoe wenye dhambi (1 Timotheo 1:15).
Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi (Warumi 5:8).
Kwa manna jinsi hii Mungu aliupenda ulim- wengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele (Yohana 3:16).
Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea (Luke 19:10).
Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako (Matendo 16:31).
Kila atakayeliita jina la Bwana ataokoka (Warumi 10:13).
Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na tuwe na amani kwa Mungu (Warumi 5:1).

KUMBUKA KATIKA YESU KUNA ULINZI WA DAMU YAKE.

Yesu akasema, “Ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe!” (Yohana 6:37).

Shalom,

Dr. Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW