Sunday, April 23, 2017

KAINI ALIPATA WAPI MKE WAKE?

Image may contain: text
HOJA YA MSINGI:
“Ikiwa Adamu na Hawa walikuwa na wana wawili, Kaini na Abeli, na baadae Seth, Je, mke wa Kaini alitoka wapi?”
Biblia ina habari za kutosha kujibu swali hilo kwa njia inayofaa, na kwenye hii mada tutajibu hili swali linalo wachanga sana watu.
MUKTASARI:
Katika Mwanzo sura ya 3 na ya 4 tunapata habari zifuatazo:
(1) Hawa alikuwa “mama ya kila mtu anayeishi.”
(2) Muda fulani ulipita kuanzia wakati Kaini alipozaliwa mpaka wakati alipotoa dhabihu ambayo ilikataliwa na Mungu.
(3) Baada ya kufukuzwa na kuwa “mwenye kutanga-tanga na mkimbizi,” Kaini alikuwa na wasiwasi kwamba huenda ‘mtu yeyote akakutana naye’ na kujaribu kumuua. [Angalia hoja hapa "Kaini anaogopa kuuwawa na watu wengine"] Hapa panaonyesha kuwa Kaini alikuwa na ndugu wengine.
(4) Mungu aliweka ishara ya kumlinda Kaini, jambo lililoonyesha kwamba ndugu au dada zake, au watu wengine wa ukoo wangejaribu kumuua. Kumbe basi Kaini alikuwa na ndugu wengine zaidi ya Abel na Seth.
(5) “Baadaye” Kaini alilala na mke wake “katika nchi ya Ukimbizi.”—Mwanzo 3:20; 4:3, 12, 14-17.
UTHIBITISHO:
Kutokana na habari hizo za kwenye Kitabu cha Mwanzo hapo juu, tunaweza kusema kwamba mke wa Kaini, ambaye haijulikani alizaliwa wakati gani, alikuwa mzao wa Hawa.
Andiko la Mwanzo 5:4 linasema kwamba katika miaka 930 ambayo Adamu aliishi, ‘alizaa wana na mabinti.’
Hivyo basi, kwa kuwa mke wa Kaini anatajwa baada ya Kaini kufukuzwa, jambo hilo linaonyesha kwamba wakati wa kutosha ulikuwa umepita na angeweza kuwa mmoja wa watoto au wajukuu wa Adamu na Hawa. Kwa hiyo, tafsiri ya Biblia The Amplified Old Testament inasema tu kwamba mke wa Kaini alikuwa “mmoja wa watoto wa Adamu.”
Wazo la kwamba Kaini alimwoa dada yake au uzao wa baadaye wa Adamu kupitia mmoja wa wana au mabinti zake, ni jambo lisilokubalika katika jamii fulani/mbalimbali leo. Sababu ni kuwa jamii hizo huliona hilo kuwa jambo lisilokubalika au huogopa kwamba litasababisha kasoro za kimaumbile kwa mtu kuoa dada yako au ndugu yako.
Hata hivyo, inaelekea kwamba ndugu na dada (Kaini na Mkewe) walioana ingawa ndoa kama hiyo ingeonekana kuwa jambo lisilofaa katika vizazi vya baadaye.” Inafaa kuzingatia kwamba ngono kati ya watu wa ukoo haikukatazwa waziwazi mpaka Musa alipopokea sheria za Mungu kwa ajili ya taifa la Israeli mwaka wa 1513 K.W.K.—Mambo ya Walawi 18:9, 17, 24.
Hivyo leo kwa kifupi tumejaribu kujibu hili swali kuhusu wapi Kaini alipata mke wake.
SWALI: Baada ya mafuriko ya NOA, ambayo yalisamilisha familia moja tu ya Noa. Je, watoto na wajukuu wa Noa walio nani?
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW