Wednesday, April 26, 2017

YESU ANASEMA MPENDE JIRANI YAKO

Image may contain: 2 people, text and outdoor
“[Amri] ya pili ni hii, ‘Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’”—Mathayo 22:39.
PINDI moja, Farisayo alimjaribu Yesu kwa kumuuliza hivi: “Mwalimu, amri iliyo kuu katika ile Sheria ni gani?” Kama ilivyotajwa katika makala iliyotangulia, Yesu alijibu kwamba “amri iliyo kuu na ya kwanza” ni hii: “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” Yesu akaongezea hivi: “Ya pili, kama hiyo, ni hii, ‘Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’”—Mathayo 22:34-39.
Yesu alisema kwamba ni lazima tumpende jirani yetu kama tunavyojipenda wenyewe. Hivyo, tunapaswa kujiuliza hivi: Ni nani kwa kweli aliye jirani yetu? Tunawezaje kuonyesha kwamba tunampenda jirani?
Huenda tukafikiri kwamba jirani ni mtu anayeishi karibu nasi ambaye ni rafiki wa karibu anayetusaidia. (Met. 27:10) Hata hivyo, ona alivyosema Yesu alipoulizwa hivi na mtu aliyejiona kuwa mwadilifu: “Ni nani kwa kweli aliye jirani yangu?” Yesu alimjibu kwa kusimulia mfano wa Msamaria mwema. (Soma Luka 10:29-37) Tungetarajia kwamba kuhani Mwisraeli na Mlawi wangetenda kama majirani wema walipomwona mtu aliyekuwa ameibiwa, akapigwa, na kuachwa karibu kufa. Hata hivyo, walipita bila kumsaidia kwa njia yoyote. Mtu huyo alisaidiwa na Msamaria—na Wasamaria waliheshimu Sheria ya Musa lakini walidharauliwa na Wayahudi.—Yohana 4:9.
Ili kumsaidia mtu huyo apone, Msamaria huyo alimwaga mafuta na divai juu ya majeraha yake. Alimpa mtunza-nyumba ya wageni dinari mbili ambazo ni sawa na mshahara wa siku mbili hivi ili amtunze mtu huyo. (Mathayo 20:2) Hivyo, ni rahisi kuona ni nani aliyethibitika kuwa jirani wa kweli wa mtu huyo aliyejeruhiwa. Kwa kweli, mfano wa Yesu unatufundisha kwamba tunapaswa kumpenda na kumhurumia jirani yetu.
Kwa nini tunapaswa kuwapenda adui zetu, na huenda matokeo yakawa nini?
Wapende adui zako. Yesu alisema hivi: “Ninyi mlisikia kwamba ilisemwa, ‘Mpende jirani yako na kumchukia adui yako.’ Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Endeleeni kuwapenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi; ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni.” (Mathayo 5:43-45) Mtume Paulo alirudia jambo hilo alipoandika hivi: “Ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe.” (Roman- 12:20; Met. 25:21) Kulingana na Sheria ya Musa, mtu alipaswa kumsaidia adui kumfungua punda wake aliyeangushwa na mzigo. (Kutoka 23:5) Kwa kufanya kazi pamoja kwa njia hiyo, huenda wale waliokuwa maadui wakawa marafiki wakubwa. Kwa kuwa tunawapenda watu tukiwa Wakristo, adui zetu wengi wamebadili maoni yao kutuhusu. Tukiwapenda adui zetu, hata wale wanaotutesa vikali, tutapata shangwe kama nini kuona baadhi yao wakikubali Ukristo wa kweli!
NJIA YA PEKEE YA KUONYESHA UPENDO KWA JIRANI
Tunahubiri habari njema ya Ufalme kama Yesu alivyofanya. (Luka 8:1) Yesu aliwaagiza wafuasi wake ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mathayo 28:19, 20) Tunatimiza agizo hilo kwa kujitahidi kuwasaidia jirani zetu kutoka katika barabara pana na kubwa inayoongoza kwenye uharibifu na kutembea kwenye barabara yenye nafasi ndogo inayoongoza kwenye uzima. (Mathayo 7:13, 14) Bila shaka Yehova anabariki jitihada hizo.
Tunapofanya marudio na kuongoza mafunzo ya Biblia kwa ustadi, tunawasaidia watu kuishi kupatana na viwango vya uadilifu vya Mungu na hilo hutuletea uradhi. Kufanya hivyo kunaweza kumsaidia mwanafunzi wa Biblia afanye mabadiliko makubwa katika maisha yake. (1 Korintho 6:9-11) Kwa kweli, inatia moyo sana kuona jinsi Mungu anavyowasaidia watu wenye “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele” kufanya mabadiliko yanayohitajika na kuwa na uhusiano wa karibu pamoja naye. (Matendo. 13:48) Wengi waliokuwa wamekata tamaa hupata shangwe, na badala ya kuwa na mahangaiko yasiyo ya lazima, wanamtumaini Baba yetu wa mbinguni. Inapendeza kama nini kuona wapya wakifanya maendeleo ya kiroho! Je, si kweli kwamba ni baraka kuwaonyesha jirani zetu upendo kwa njia ya pekee tukiwa wahubiri wa Ufalme?
ENDELEA KUMPENDA JIRANI YAKO KAMA WEWE MWENYEWE
‘Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Upendo haumfanyii uovu jirani ya mtu; kwa hiyo upendo ndio utimizo wa sheria.” (Rom. 13:8-10) Hivyo, tunapaswa kuendelea kumpenda jirani yetu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW