Tuesday, April 11, 2017

VAENI SILAHA ZOTE ZA MUNGU

Image may contain: text
Je, umesha vaa silaha zote za Mungu?
Waefeso 6:10-12 yasema, “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” Ujumbe huu wafunza baadhi ya kweli muimu: tutaweza kuwa na uwezo kwa nguvu za Mungu, ni silaha ya Mungu ambayo yatulinda, na vita ni kupinga na nguvu za giza za ulimwengu huu.
Mfano wa nguvu sana juu ya ngunvu za Bwana ni ule wa malaika Mikaeli katika Yuda 9. Mikaeli ambaye ni mwenye nguvu zaidi ya malaika wote wa Mungu, hakumkemea Shetani kwa nguvu zake, bali alisema, “Mungu anakukemea!” Ufunuo 12:7-8 yanakiri kwamba katika nyakati za mwisho Mikaeli atamshinda Shetani. Bado, wakati inafikia mapigano yake na Shetani, Mikaeli alimkemea Shetani katika jina la Mungu na mamlaka yake, si kwa nguvu zake. Ni kupitia kwa uhusiano wetu na Yesu Kristo kuwa Wakristo wako na mamlaka yoyote juu ya Shetani na mapepo yake. Ni kupitia kwa jina lake kuwa kemeo letu liko na nguvu.
Waefeso 6:13-18 yatupa elezo la silaha za kiroho Mungu anapeana. Tunastahili kusimama dhabiti na kufunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kufuani, na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani, kuchukua ngao ya wokovu na kwa kuomba katika roho.
Kwa ufupi, njia za ufanisi wa vita vya kiroho ni zipi?
Shalom
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW