Wednesday, May 3, 2017

UTATA MKUMBWA NDANI YA KORAN Nini kitaingia PEPONI: Roho/Nafsi au Mwili au zote mbili?




Somo letu la leo ni la swali kwa Allah ambaye ameshindwa kujieleza, kuwa ni kipi kinaingia Peponi kati ya Roho/Nafsi au Mwili?

Koran inadai kuwa, baada ya ufufuo, ni mwili (baada ya kuungana na roho?) Ambayo inaingia peponi. Haya madai yamewekewa mkazo katika Koran. Angalia mistari ifuatayo 13:05, 17:98-99, 20:55, 34:7, 75:3-4.

Hata hivyo mistari ya 27-30 kwenye Sura 89 ipinga aya zilizo pita kwa kusema kuwa ni nafsi (Nafs) tu ambayo inaingia Peponi!

Quran 17:99. Kwani hawakuona ya kwamba Mwenyezi Mungu aliye umba mbingu na ardhi ni Mwenye kuweza kuumba mfano wao? Na Yeye amewawekea muda usio na shaka yoyote. Lakini madhaalimu hawataki ila ukafiri. 

Quran 75:3. Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?  4. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake! 

Aya hizo hapo juu, zinadai kuwa Nafsi na Mwili vitaungana na kuingia Peponi, hayo ni maneno ya Allah kama alivyo yashusha kupitia Quran yake. Lakini Allah huyohuyo anabadilika na kusema kuwa Nafsi ndio itaingia Peponi. Hebu soma aya zifuatazo.

Quran 89 27. Ewe nafsi iliyo tua! 28. Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. 

Katika aya hapo juu, Allah anaiamuru Nafsi irejee kwake. Sasa ni ipi kati ya Nafsi na Mwili vitaingia Peponi? Utata huu ni Msiba Mkubwa kwa Allah ambaye hafamu nini kati ya Nafsi na Mwili vitaingia Peponi.

Quran 31:28. Hakukuwa kuumbwa kwenu, wala kufufuliwa kwenu ila ni kama nafsi moja tu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kuona. 

Allah anaendelea kusema kuwa ni Nafsi ndio itaingia Peponi. Aya hizi zinapingana na maneno yake ya kwanza kuwa ni Nafsi pamoja na Mwili vinaingia Peponi. Hivi Allah ni kweli aliumba Binadamu? Mbona hafahamu nini kati ya Nafsi na Mwili itaingia Peponi?

Katika Uislamu, neema ya peponi haikamiliki bila raha ya pamoja ya Mwili na akili, maana Allah katoa ahadi ya wake 72 kwa wale wote watakao ingia Peponi. Vinginevyo, mtu atawezaje kunywa Zanzabil (76:17), na kuifurahia hicho kinywaji (76:13), kufurahia wanawali (55:56) na kunywa asali na maziwa (47:16-17) bila ya kuwa na Mwili?

Yousuf Ali (Nakala 6128 kwa aya 89:27-30) pia anasema kwamba ni roho ambayo inaingia mbinguni, na si mwili ambao utaharibika (Maoni yake ni kupingana na aya 75:3-4 zinavyo sema!). Soma aya 31:28 pia. Inasema kuundwa kwa mtu au ufufuo ni katika nafsi.

Ndugu wasomaji, Allah anaendelea kutoa utata katika uumbaji wake. Allah kwa mara nyingine tena ameshindwa kuufahamisha umma wake kuwa, ni nini kati ya Nafsir na Mwili vitaingia Peponi.

Koran si kitabu cha Mungu bali ni maneno ya Muham-mad ambayo alindika ili kukuza maono yake ya kisiasa. Kama Allah ni mungu, basi ifahamike leo kuwa Allah si Mungu aliye umba Mbingu na Nchi. Si Mungu aliye muumba Adamu na Hawa, bali ni Mpinga Mungu.

Katika huduma Yake.

Max Shimba

Copyright © Max Shimba Ministries 2013

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW