Friday, September 2, 2016

KUMBE MALAIKA WANA AKILI KULIKO ALLAH WA ISLAM!


Malaika Watabiri Mwenendo wa Binadamu kabla ya kuumbwa. Allah atumia hila kuficha udhaifu wake.
Katika somo letu la leo, tutajifunza kuwa Malaika wa Allah wana Akili na ufahamu wa mambo ya baadae kuliko Allah wa Islam.
Quran Surah 2:
30. Na pale Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyo yajua. ***
KATIKA AYA YA 30. Tunasoma kuwa Malaika wanampa darsah Allah, jinsi gani Mtu atakuwa kabla ya uumbaji wake. Malaika wameonyesha upeo mkubwa kwa kufahamu maisha ya baada ya Adam/binadamu kabla ya hata kuumbwa.
31. Na akamfundisha Adam majina ya vitu vyote, kisha akaviweka mbele ya Malaika, na akasema: Niambieni majina ya hivi ikiwa mnasema kweli. ***
Kwenye aya 31 hapo juu, tunasoma kuwa Allah anamfundisha kwa siri Adam ili aweze kuwazima mdomo Malaika. Kitendo cha Allah kumfudisha Adam ili kushindana na Malaika haikuwa haki kwani Malaika walimpa changamoto Allah, Je, Allah ni mwenye ufahamu wa yote?
32. Wakasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hatuna ujuzi isipokuwa kwa uliyo tufunza Wewe. Hakika Wewe ndiye Mjuzi Mwenye hikima. ***
Je, Allah alipo tumia udanganyifu na uongo ili kujitetea mwenyewe dhidi ya mashtaka kwa Adamu kama yalivyo letwa na Malaika (mashtaka ambayo aligeuka kuwa ni sahihi) ni sahihi?
33. Akasema: Ewe Adam! Waambie majina yake. Basi alipo waambia majina yake alisema: Sikukwambieni kwamba Mimi ninajua siri za mbinguni na za duniani, na ninayajua mnayo yadhihirisha na mliyo kuwa mnayaficha? ***

34. Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipo kuwa Iblis, alikataa na akajivuna na akawa katika makafiri. ***
35. Na tulisema: Ewe Adam! Kaa wewe na mkeo katika Bustani, na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu tu; mkawa katika wale walio dhulumu. ***
36. Lakini Shet'ani aliwatelezesha hao wawili na akawatoa katika waliyo kuwamo, na tukasema: Shukeni, nanyi ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Katika ardhi yatakuwa makaazi yenu na starehe kwa muda. ***
37. Kisha Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi alimkubalia toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kukubali toba na Mwenye kurehemu. ***
38. Tukasema: Shukeni nyote; na kama ukikufikieni uwongofu utokao kwangu, basi watakao fuata uwongofu wangu huo haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika. ***
Katika vifungu hapo juu, tumesoma kuwa Malaika wanaufahamu kama Mungu (Omniscient) na ua wa Kimungu. Malaika waliweza kufahamu maisha ya Mwandamu kabla ya hata kuumbwa. Jambo ambalo Allah wa Islam hakulifahamu na hakuwa na ufahamu huo.
Kwanza, jinsi gani Malaika walijua hali ya mtu itakuwa kabla ya uumbaji wake? Malaika walifahamuje kabla ya uumbaji kuwa, binadamu watakuwa na vurugu? Nani aliwaambia? Nakala haisemi chochote juu ya Allah kuwapa kipande hiki cha habari. Je, Malaika anayajua yote kama Mungu (Omniscient)?
Pili, Mwenyezi Mungu kwa siri anafundisha Adam majina yasiyojulikana ili kuwanyamazisha Malaika kwa kulalamika dhidi ya mtu. Je, hii ni haki? Kwa nini Allah anatumia hila na hujmah, ili kuwafanya Malaika waonekane hawana ufahamu?
Je, Allah alipo tumia udanganyifu na uongo ili kujitetea mwenyewe dhidi ya mashtaka kwa Adamu kama yalivyo letwa na Malaika (mashtaka ambayo aligeuka kuwa ni sahihi) ni sahihi?
Je, si dhahiri kwamba Adamu angekuwa na ufahamu wakawaida kama Malaika kwasababu Allah alikuwa bado hajawafundisha kuhusu uumbaji wake?
Kwanini Allah wa Islam anatumia udanganyifu ili kuficha udhaifu wake katika uumbaji?
Ndugu zanguni, leo tumejifunza kuwa Allah si msema ukweli na Allah hana ufahamu wa mambo yote kama alivyo Yehova ambaye ni Mungu aliye semwa ndani ya Biblia.
Kama unataka kufahamu kweli, basi nakusihi umpokee Yesu aliye hai, yeye ndie Njia, Kweli na Uzima. Katika Yesu, hakuna udanganyifu wa Allah. Mpokee leo ili upate uzima wa milele.
Katika huduma yake.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW