Friday, September 2, 2016

Kwanini waislamu mnakula ngamia?

Swali,

Kwanini waislamu mnakula ngamia wakati Biblia imekataza, mnaishia kutusema sisi wakristo tuu kwamba tunakula Nguruwe?
Jibu:
Andiko linasema hivi;
Walawi 11:3-4:

3-Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu ya kupasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndio mtakaowala.

4-Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.
Hapo katika suala la Ngamia ndipo mwandishi wa mambo ya walawi alipofanya typing error.
Ngamia ana kwato (hooves) na zimegawanyika katikati (rejea hizo picha juu)Hivyo waislamu tunakula Ngamia kwa sababu anacheua na anakwato zilogawanyika (zinazofanana na vidole/toenail).

Typing error nyingine katika andiko la walawi ni kuwa Sungura hucheua (Mambo ya Walawi 11:6). Lakini ukweli ni kwamba Sungura hacheui kabisa.

No comments:

Mohammad’s Myths vs. Biblical and Scientific Reality: A Scholarly Debate on Laughter, Heart, and Divine Truth

By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction In evaluating the truth-claims of any religion, the alignment between i...

TRENDING NOW